sweetlady
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 16,947
- 8,409
sweetlady kuondoka rahisi dear lakini sharti lake unajua huyu bwana anasema watoto atawachukua na watoto wangu wote wa kike maskini nimewazaa kwa tabu na mama angu na ndugu zangu wote wamenisamehe mama angu ananiambia niachane nae ni mnyama huyu mara nyingi tu nimetolewa humu ndani nafukuzwa bila viatu kisa ukimtell kama y unarudi alfajiri
Anakutisha ili aendelee kukunyanyasa, ujue wanaume wengi wanatumiaga udhaifu wetu wa kuwapenda watoto kututesea, USIKUBALI, mateso yako ni makubwa mno.. Nenda kwenye vyombo vya sheria na utapata haki yako. Kwanza hakuna mwanaume mwenye ruhusa ya kuishi na watoto wenye umri chini ya miaka 7, haijalishi ni wakwake..
Nenda ustawi wa jamii, nenda hata police kamshtakie hayo mateso anayokupa, utapata msaada wa dhati.. Nshakuambia tena huyo mumeo ni muuaji, na asipokuua kwa vipigo, atakuua kwa ukimwi.. Mshirikishe mamako na ndugu zako.. Watakusaidia.. Pole sana..