Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Hakimu 'wa Liyumba' atupwa mkoaniNI ALIYEMPA DHAMANA YA SH882M KATI YA SH55BILIONI
HAKIMU Hadija Msongo, aliyewahi kutoa dhamana katika mazingira ya utata kwa mtuhumiwa Amatus Liyumba, amehamishwa kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kupelekwa mkoani Pwani.
Uamuzi huo wa Ofisi ya Jaji Kiongozi kumhamisha hakimu huyo, umetolewa katika kipindi ambacho mahakama ya Kisutu imekuwa ikiangaliwa kwa karibu na Watanzania wengi, kutokana na kuwa sehemu kuu ya usikilizaji wa kesi nyingi za ufisadi.
Msongo alimpa dhamana Liyumba Februari 17 mwaka huu, kwa kutumia hati moja moja ya nyumba ya Liyumba yenye thamani ya Sh882 milioni huku hati nyingine zikiendelea kuhakikiwa baada ya ofisa huyo mwandamizi wa zamani wa Benki Kuu (BoT), kutakiwa kutoa dhamana yenye thamani ya Sh55 bilioni.
Liyumba alipewa dhamana hiyo wakati akiwa ameshtakiwa kwa mara ya kwanza kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi, yaliyoisababishia serikali hasara ya Sh 221 bilioni, ambazo ni tofauti ya gharama halisi ya ujenzi wa majengo ya minara pacha kwenye makao makuu ya benki hiyo ,kulinganisha na gharama inayodaiwa kukuzwa kifisadi.
Kwa mujibu wa habari za kuaminika, uhamisho wa hakimu huyo umekuwa kama adhabu kutokana na kufanya uamuzi wa dhamana hiyo, ambayo pia ilihusisha hati ya kusafiria iliyoisha muda.
Hata hivyo, Jaji Kiongozi Fakhi Jundu aliliambia gazeti hili ofisini kwake jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita kwamba, uhamisho huo ni sehemu ya utaratibu wa kawaida tu.
Akitoa dhamana hiyo, Msongo ambaye baadaye alijitoa kwenye kesi hiyo, alisema hati nyingine 10 zilizokuwa zimewasilishwa na Liyumba kwa ajili ya dhamana, ziendelee kuhakikiwa na mahakama.
Hata hivyo, hati hizo zilipingwa na upande wa mashtaka kutokana na baadhi kuwa mali zinazohamishika kama ng'ombe, kuku na matrekta.
Baada ya kutolewa kwa dhamana hiyo, upande wa serikali ulidai kutoridhishwa na uamuzi huo. Jalada la kesi hiyo lilitakiwa Mahakama Kuu na siku iliyofuata wadhamini wa Liyumba walikamatwa na kushikiliwa mahakamani.
Mahakama hiyo ilifuta dhamana hiyo Februari 24 na Hakimu Msongo alijitoa kusikiliza kesi hiyo Machi 20. Kesi hiyo sasa inasikilizwa na Hakimu Wariyalwande Lema.
Lakini Jaji Kiongozi Jundu alisisitiza kwamba, uamuzi wa kumhamisha hautokani na adhabu ya kutoa dhamana hiyo kwa Liyumba.
"Ni uhamisho ambao umefanyika chini ya utaratibu wa kawaida, kwa maana hata barua yake haisemi kwamba, amehamishwa kutokana na kutoa dhamana kwa Liyumba," alifafanua.
Alisema ni kweli uamuzi huo ulifanyika baada ya dhamana hiyo, lakini haukuwa adhabu na kwamba, kazi ya kuadhibu hufanywa na jopo maalumu la nidhamu la mahakama.
Jundu aliongeza kwamba, mahakama ina utaratibu wake wa kufanya uhamisho kila mara ili kuweza kuongeza tija na ufanisi katika mahakama zake mbalimbali nchini kote.
Lakini habari ambazo Mwananchi imezipata zinasema kuwa, hakimu huyo alihamishwa kwa lengo la kumwondoa mahakamani Kisutu, ambako kesi nyingi za ufisadi zimekuwa zikipelekwa.
Kwa mujibu wa habari hizo, upande wa serikali ulichukizwa na maamuzi hayo ya kumwachia Liyumba ambaye alishinda kesi ya awali kutokana na hoja za kiufundi, lakini akafunguliwa tena kesi baada ya serikali kurekebisha hati ya mashtaka.
Hadi sasa Liyumba yuko ndani baada ya majaribio yake yote ya kutaka sheria imuokoe na kiwango kikubwa cha dhamana kugonga mwamba. Baada ya kushtakiwa upya akiwa peke yake, Liyumba sasa anatakiwa kuwasilisha dhamana yenye thamani ya zaidi ya Sh100 bilioni.
Wanasheria wake walifanikiwa kuishawishi mahakama kuwa, kipengele kinachotaka mtuhumiwa atoe dhamana yenye thamani ya nusu ya fedha anazodaiwa kuiba, hakitakiwi kutumika kwenye kesi ya kigogo huyo wa zamani wa BoT kwa kuwa hashtakiwi kwa wizi.
Mahakama ilipunguza kiwango hicho cha dhamana hadi Sh300 milioni. Lakini siku ambayo alitakiwa kuachiwa huru, upande wa mashtaka haukuwa tayari kuhakikisha hati za mali na hivyo kusababisha aendelee kukaa mahabusu.
Baadaye upande wa mashtaka ulikata rufaa Mahakama Kuu, ambayo iliagiza tena kuwa mshtakiwa awasilishe dhamana ambayo ni nusu ya mali anayodaiwa kuisababishia serikali hasara.
Hata hivyo, wanasheria wa Liyumba bado hawajanyoosha mikono juu kukubali kushindwa katika kuhakikisha mteja wao anakuwa nje kwa dhamana. Wiki moja iliyopita alishindwa kujitokeza mahakamani baada ya kuelezwa kwamba alikuwa mgonjwa huko mahabusu anakoshikiliwa hadi sasa.
Source: Tanzania daima
HAKIMU Hadija Msongo, aliyewahi kutoa dhamana katika mazingira ya utata kwa mtuhumiwa Amatus Liyumba, amehamishwa kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kupelekwa mkoani Pwani.
Uamuzi huo wa Ofisi ya Jaji Kiongozi kumhamisha hakimu huyo, umetolewa katika kipindi ambacho mahakama ya Kisutu imekuwa ikiangaliwa kwa karibu na Watanzania wengi, kutokana na kuwa sehemu kuu ya usikilizaji wa kesi nyingi za ufisadi.
Msongo alimpa dhamana Liyumba Februari 17 mwaka huu, kwa kutumia hati moja moja ya nyumba ya Liyumba yenye thamani ya Sh882 milioni huku hati nyingine zikiendelea kuhakikiwa baada ya ofisa huyo mwandamizi wa zamani wa Benki Kuu (BoT), kutakiwa kutoa dhamana yenye thamani ya Sh55 bilioni.
Liyumba alipewa dhamana hiyo wakati akiwa ameshtakiwa kwa mara ya kwanza kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi, yaliyoisababishia serikali hasara ya Sh 221 bilioni, ambazo ni tofauti ya gharama halisi ya ujenzi wa majengo ya minara pacha kwenye makao makuu ya benki hiyo ,kulinganisha na gharama inayodaiwa kukuzwa kifisadi.
Kwa mujibu wa habari za kuaminika, uhamisho wa hakimu huyo umekuwa kama adhabu kutokana na kufanya uamuzi wa dhamana hiyo, ambayo pia ilihusisha hati ya kusafiria iliyoisha muda.
Hata hivyo, Jaji Kiongozi Fakhi Jundu aliliambia gazeti hili ofisini kwake jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita kwamba, uhamisho huo ni sehemu ya utaratibu wa kawaida tu.
Akitoa dhamana hiyo, Msongo ambaye baadaye alijitoa kwenye kesi hiyo, alisema hati nyingine 10 zilizokuwa zimewasilishwa na Liyumba kwa ajili ya dhamana, ziendelee kuhakikiwa na mahakama.
Hata hivyo, hati hizo zilipingwa na upande wa mashtaka kutokana na baadhi kuwa mali zinazohamishika kama ng'ombe, kuku na matrekta.
Baada ya kutolewa kwa dhamana hiyo, upande wa serikali ulidai kutoridhishwa na uamuzi huo. Jalada la kesi hiyo lilitakiwa Mahakama Kuu na siku iliyofuata wadhamini wa Liyumba walikamatwa na kushikiliwa mahakamani.
Mahakama hiyo ilifuta dhamana hiyo Februari 24 na Hakimu Msongo alijitoa kusikiliza kesi hiyo Machi 20. Kesi hiyo sasa inasikilizwa na Hakimu Wariyalwande Lema.
Lakini Jaji Kiongozi Jundu alisisitiza kwamba, uamuzi wa kumhamisha hautokani na adhabu ya kutoa dhamana hiyo kwa Liyumba.
"Ni uhamisho ambao umefanyika chini ya utaratibu wa kawaida, kwa maana hata barua yake haisemi kwamba, amehamishwa kutokana na kutoa dhamana kwa Liyumba," alifafanua.
Alisema ni kweli uamuzi huo ulifanyika baada ya dhamana hiyo, lakini haukuwa adhabu na kwamba, kazi ya kuadhibu hufanywa na jopo maalumu la nidhamu la mahakama.
Jundu aliongeza kwamba, mahakama ina utaratibu wake wa kufanya uhamisho kila mara ili kuweza kuongeza tija na ufanisi katika mahakama zake mbalimbali nchini kote.
Lakini habari ambazo Mwananchi imezipata zinasema kuwa, hakimu huyo alihamishwa kwa lengo la kumwondoa mahakamani Kisutu, ambako kesi nyingi za ufisadi zimekuwa zikipelekwa.
Kwa mujibu wa habari hizo, upande wa serikali ulichukizwa na maamuzi hayo ya kumwachia Liyumba ambaye alishinda kesi ya awali kutokana na hoja za kiufundi, lakini akafunguliwa tena kesi baada ya serikali kurekebisha hati ya mashtaka.
Hadi sasa Liyumba yuko ndani baada ya majaribio yake yote ya kutaka sheria imuokoe na kiwango kikubwa cha dhamana kugonga mwamba. Baada ya kushtakiwa upya akiwa peke yake, Liyumba sasa anatakiwa kuwasilisha dhamana yenye thamani ya zaidi ya Sh100 bilioni.
Wanasheria wake walifanikiwa kuishawishi mahakama kuwa, kipengele kinachotaka mtuhumiwa atoe dhamana yenye thamani ya nusu ya fedha anazodaiwa kuiba, hakitakiwi kutumika kwenye kesi ya kigogo huyo wa zamani wa BoT kwa kuwa hashtakiwi kwa wizi.
Mahakama ilipunguza kiwango hicho cha dhamana hadi Sh300 milioni. Lakini siku ambayo alitakiwa kuachiwa huru, upande wa mashtaka haukuwa tayari kuhakikisha hati za mali na hivyo kusababisha aendelee kukaa mahabusu.
Baadaye upande wa mashtaka ulikata rufaa Mahakama Kuu, ambayo iliagiza tena kuwa mshtakiwa awasilishe dhamana ambayo ni nusu ya mali anayodaiwa kuisababishia serikali hasara.
Hata hivyo, wanasheria wa Liyumba bado hawajanyoosha mikono juu kukubali kushindwa katika kuhakikisha mteja wao anakuwa nje kwa dhamana. Wiki moja iliyopita alishindwa kujitokeza mahakamani baada ya kuelezwa kwamba alikuwa mgonjwa huko mahabusu anakoshikiliwa hadi sasa.
Source: Tanzania daima