Asante M4C, vipofu wafunguka macho - Elimu na Afya bure inawezekana, akiri Sitta!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema Serikali kutoa huduma ya Elimu na Afya bure inawezekana ikiwa tu mianya ya rushwa na ufisadi itadhibitiwa ipasavyo na wananchi wataweza kunufaika na rasilimali zilizopo nchini....

Yalisemwa na Chadema mwaka 2010 lakini wakabana, sasa joto la M4C linaanza kuwachoma...taratibu watajivua nguo moja baada ya mwingine. Kama vipofu walidai haiwezekani, M4C imewaondolea wingu lililowaziba macho...

Aliongeza, “Hatuwezi kuwa na nchi ina kila kitu, tunayo makaa ya mawe, maziwa, mito, bahari, madini, gesi, mbuga za wanyama, Mlima Kilimanjaro na tuna hekta za kilimo zaidi ya milioni 88, tunataka Watanzania muamke na muache kushabikia rushwa ndogo ndogo tuingie katika utamaduni unaotuwezesha kujenga heshima ya nchi yetu kwa kujali uongozi ulionyooka na wenye uhadilifu.”

Lahaula! masikini Sitta, alikuwa anakataa nini na sasa anakubali nini!...once he was blind but now he can see, thanx to makamanda! Mwanga wa Chadema utawatoa mkukumkuku pangoni. Kwa habari zaidi bonyeza hapa;

 
Tatizo hao jamaa wakiiga wanachanganya na sera zao za ufisdi na baadae yanawashinda,
mfano kwenye elimu ya msingi wameitangazia nchi nzima kuwa ni bure lakini leo imekuwa na gharama kubwa kuliko hata ilivyokuwa ya kulipia,
Tena juzi kati wametoa mpya mitihani ya ki muhula yote inalipiwa 1000/kila mmoja KWA KICHWA na hakuna stakabadhi inayo tolewa ni agizo toka wizara ya elimu
HAWA MUDA WAO UMEKWISHA WAONDOKE TU.
 
Sitta: Elimu na Afya bure inawezekana
Saturday, 01 September 2012 09:03
Edwin Mjwahuzi, Kagera - Mwananchi.

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema Serikali kutoa huduma ya Elimu na Afya bure inawezekana ikiwa tu mianya ya rushwa na ufisadi itadhibitiwa ipasavyo na wananchi wataweza kunufaika na rasilimali zilizopo nchini.

Sitta alisema ni lazima turudi kwenye misingi ya uadilifu, kujali wanyonge, kukataa rushwa na kukataa ufisadi wa aina yoyote ndipo tutaweza kukusanya na kuinua uchumi wa kutosha na kulipana mishahara mizuri, kumlipa pensheni mzee na kutoa huduma hizo bure.

Aliyasema hayo alipokaribishwa katika mkutano wa akinamama wajane kutoka wilayani Karagwe na Kyelwa mkoani Kagera na kuwashirikisha wazee wa Wilaya hizo uliofanyika katika ukumbi uliopo katika ofisi za CCM wilayani Karagwe.

Sitta alisema itakuwa ndoto za kupata huduma hizo bure kama nchi haitafanikiwa kuziba mianya yote ya rushwa na wananchi wataendelea kupiga kelele wakitaka kupatiwa huduma hizo bila ya mafanikio.

"Ningependa kuwaambia wananchi, najua karibu wote tunataka utoaji wa huduma ya afya, elimu ya kuanzi msingi mpaka elimu ya juu kuwa bure, ndugu zangu katika hali ambayo hata huduma ya afya ya kawaida haipatikani ni mtihani mkubwa kwa kutoa elimu ya bure," alisema.

Aliongeza, "Hatuwezi kuwa na nchi ina kila kitu, tunayo makaa ya mawe, maziwa, mito, bahari, madini, gesi, mbuga za wanyama, Mlima Kilimanjaro na tuna hekta za kilimo zaidi ya milioni 88, tunataka Watanzania muamke na muache kushabikia rushwa ndogo ndogo tuingie katika utamaduni unaotuwezesha kujenga heshima ya nchi yetu kwa kujali uongozi ulionyooka na wenye uhadilifu."

Sitta alisema wananchi wasiwe na ndoto ya maisha bora kwa kila mtanzania ikiwa rushwa na ufisadi utaendelea kutawala na kufumbiwa macho.

"Ndugu zangu hatuwezi kupata maisha bora kama kiwango cha rushwa, ufisadi na dhuluma kikiwa hivi hivi tunavyokiona hivi sasa, kwa sababu Serikali ilileta utoaji pembejeo kwa kutumia vocha sasa tutaendelea vipi kama vocha zenyewe zinachakachuliwa?" alihoji.

"Iwapo tutadhibiti mianya ya ufisadi na rushwa, nchi yetu itainuka na kuweza kuwasaidia wazee wetu, wajane, watoto yatima kwa kuwapatia huduma nyingi nzuri, ilimradi tu ufisadi unatakiwa kupigwa vita kuanzia chini huku," alisema Sitta.

Sitta pia aliwaomba wajane hao na wazee kupita kila mahali na kuwashaui wananchi wao wakiwemo na wana CCM kuwa makini wa watu wanaojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za kisiasa na kiserikali wasije wakafanya makosa kuwaweka watu wenye nia mbaya na nchi hii kwa kujali matumbo yao na familia zao.

"Sasa hivi hata kule bungeni mnaona baadhi ya mawaziri, anatokea mtu amekuwa waziri ndani ya miaka 2 au chini ya hapo unasikia kanunua nyumba Mikocheni ya mabilioni, haiwezekani na wala haingii akilini hakuwa waziri wa wananchi huyu ameingia kuchuma tu," alisema.

Waziri Sitta amemaliza juzi ziara ya kiserikali ya siku tano mkoani humo alipokuwa akiangalia miradi mbalimbali inayohusiana na muingiliano wa uchumi na kijamii kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
 
Alipokuwa Spika aliogopa kusimamia vita ya ufisadi hadi mwisho, sasa anaongelea uani kama anavyoongea January kuhusu sms za rushwa. Wamechanganyikiwa na sasa wanasema kila lijalo kinywani. Eti hata EL naye anapinga rushwa, anazunguka akikemea ufisadi! Miaka 50 ni mingi sana na kama haikuwezekana basi !
 
Alipokuwa Spika aliogopa kusimamia vita ya ufisadi hadi mwisho, sasa anaongelea uani kama anavyoongea January kuhusu sms za rushwa. Wamechanganyikiwa na sasa wanasema kila lijalo kinywani. Eti hata EL naye anapinga rushwa, anazunguka akikemea ufisadi! Miaka 50 ni mingi sana na kama haikuwezekana basi !
Mkuu Nguruvi3, kwa ukumbusho tu, hizi ndizo baadhi ya ahadi alizotoa Dr. Slaa mwaka 2010 iwapo angechaguliwa kuwa Raisi wa nchi hii;

1.Kujenga nchi isiyo na ufisadi
2.Kufufua Tanganyika ili irejee mezani kujadili muungano na Zanzibar
3.Kufufua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo
4.Kukata asilimia 20 ya mshahara wa rais
5.Kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia 15
6. Kuweka Mwenge wa Uhuru Jumba la Makumbusho
7. Kutoa huduma bora za elimu na afya bure
8. kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi
9. Kuwalipa wazee wa EAC fedha zao ndani ya siku 100
10. Kubana matuzi Ikulu (Yuko tayari kula mihogo)

Hizi ahadi zote zilipingwa na wana CCM mojawapo akiwa ni Spika wa Bunge wa wakati huo Dr. Samwel John Sitta. Leo mwaka 2012 kama vile kazinduka tu ghafla huyooo anadai elimu na afya bure inawezekana mradi mianya ya rushwa ifungwe. Swali langu la kwanza kwa fisadi Sitta ni hili, je hiyo mianya ya rushwa anayoongelea haikuwepo mwaka 2010? Swali la pili ni je hizo rasilimali anazozitaja hivi sasa, hazikuwepo mwaka 2010?
 
Mkuu Nguruvi3, kwa ukumbusho tu, hizi ndizo baadhi ya ahadi alizotoa Dr. Slaa mwaka 2010 iwapo angechaguliwa kuwa Raisi wa nchi hii;

1.Kujenga nchi isiyo na ufisadi
2.Kufufua Tanganyika ili irejee mezani kujadili muungano na Zanzibar
3.Kufufua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo
4.Kukata asilimia 20 ya mshahara wa rais
5.Kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia 15
6. Kuweka Mwenge wa Uhuru Jumba la Makumbusho
7. Kutoa huduma bora za elimu na afya bure
8. kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi
9. Kuwalipa wazee wa EAC fedha zao ndani ya siku 100
10. Kubana matuzi Ikulu (Yuko tayari kula mihogo)

Hizi ahadi zote zilipingwa na wana CCM mojawapo akiwa ni Spika wa Bunge wa wakati huo Dr. Samwel John Sitta. Leo mwaka 2012 kama vile kazinduka tu ghafla huyooo anadai elimu na afya bure inawezekana mradi mianya ya rushwa ifungwe. Swali langu la kwanza kwa fisadi Sitta ni hili, je hiyo mianya ya rushwa anayoongelea haikuwepo mwaka 2010? Swali la pili ni je hizo rasilimali anazozitaja hivi sasa, hazikuwepo mwaka 2010?
Labda niulize hivi CCM kuna watu wanajua kusoma? Nauliza hivi kwasababu kila mara vitabu vyote vinakuwa wazi 'open book' hakuna anayeweza kuchukua maarifa na kuyafanyia kazi. Kama wangefanyia kazi hayo uliyoyasema leo wasingekuwa wamechanganyikiwa kiasi hiki.

Mtu kama Sitta kula matapishi ni dhalili sana. Miaka yote serikalini hakuona kuwa hayo yanawezekana leo ayaone Karagwe! Kila mtu anaibuka na kusema lake, huku Nape kachanganyikiwa na kuacha hoja nzito, January na kutumia sms kupambana na ufisadi, EL kuona tatizo la ajira baada ya kujiuzulu, EL kupinga kilimo kwanza, ili mradi tu awaye afungue kinywa.

CCM naona muda umefika, kama kuna mtu hajachukua mafao basi huu ndio muda muafaka
 
uongo hauna maisha,yaani haudumu,na ukweli daima huwa unaishi hata kama utakua na miaka miatano utakumbuka yaliyo ya miaka kumi nyuma.huyu sita kweli ni mnafiki mkubwa,leo anongea lipi na huko nyuma alikua anapinga lipi,wanavyokaa kanisani na misikitini kwa unyenyekevu kumbe roho zao za kiuaji na kinafiki
 
Mkuu Nguruvi3, kwa ukumbusho tu, hizi ndizo baadhi ya ahadi alizotoa Dr. Slaa mwaka 2010 iwapo angechaguliwa kuwa Raisi wa nchi hii;

1.Kujenga nchi isiyo na ufisadi
2.Kufufua Tanganyika ili irejee mezani kujadili muungano na Zanzibar
3.Kufufua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo
4.Kukata asilimia 20 ya mshahara wa rais
5.Kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia 15
6. Kuweka Mwenge wa Uhuru Jumba la Makumbusho
7. Kutoa huduma bora za elimu na afya bure
8. kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi
9. Kuwalipa wazee wa EAC fedha zao ndani ya siku 100
10. Kubana matuzi Ikulu (Yuko tayari kula mihogo)

Hizi ahadi zote zilipingwa na wana CCM mojawapo akiwa ni Spika wa Bunge wa wakati huo Dr. Samwel John Sitta. Leo mwaka 2012 kama vile kazinduka tu ghafla huyooo anadai elimu na afya bure inawezekana mradi mianya ya rushwa ifungwe. Swali langu la kwanza kwa fisadi Sitta ni hili, je hiyo mianya ya rushwa anayoongelea haikuwepo mwaka 2010? Swali la pili ni je hizo rasilimali anazozitaja hivi sasa, hazikuwepo mwaka 2010?

Mag3 hawa wamezoea kuwahadaa wananchi na wamehadaika kweli kweli kwa zaidi ya miaka hamsini!! CHADEMA wamesema yale ambayo ni dhahiri kuwa yataleta maendeleo ambayo hata CCM wanayaona lakini kwa sababu za uroho wao na unafiki wametufikisha hapa tulipo. Waendelee kubwabwaja wananchi wa leo sio wale wa siku za "ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI".
 
Sitta: Elimu na Afya bure inawezekana
Saturday, 01 September 2012 09:03
Edwin Mjwahuzi, Kagera - Mwananchi.

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema Serikali kutoa huduma ya Elimu na Afya bure inawezekana ikiwa tu mianya ya rushwa na ufisadi itadhibitiwa ipasavyo na wananchi wataweza kunufaika na rasilimali zilizopo nchini.

Sitta alisema ni lazima turudi kwenye misingi ya uadilifu, kujali wanyonge, kukataa rushwa na kukataa ufisadi wa aina yoyote ndipo tutaweza kukusanya na kuinua uchumi wa kutosha na kulipana mishahara mizuri, kumlipa pensheni mzee na kutoa huduma hizo bure.

Aliyasema hayo alipokaribishwa katika mkutano wa akinamama wajane kutoka wilayani Karagwe na Kyelwa mkoani Kagera na kuwashirikisha wazee wa Wilaya hizo uliofanyika katika ukumbi uliopo katika ofisi za CCM wilayani Karagwe.

Sitta alisema itakuwa ndoto za kupata huduma hizo bure kama nchi haitafanikiwa kuziba mianya yote ya rushwa na wananchi wataendelea kupiga kelele wakitaka kupatiwa huduma hizo bila ya mafanikio.

"Ningependa kuwaambia wananchi, najua karibu wote tunataka utoaji wa huduma ya afya, elimu ya kuanzi msingi mpaka elimu ya juu kuwa bure, ndugu zangu katika hali ambayo hata huduma ya afya ya kawaida haipatikani ni mtihani mkubwa kwa kutoa elimu ya bure," alisema.

Aliongeza, "Hatuwezi kuwa na nchi ina kila kitu, tunayo makaa ya mawe, maziwa, mito, bahari, madini, gesi, mbuga za wanyama, Mlima Kilimanjaro na tuna hekta za kilimo zaidi ya milioni 88, tunataka Watanzania muamke na muache kushabikia rushwa ndogo ndogo tuingie katika utamaduni unaotuwezesha kujenga heshima ya nchi yetu kwa kujali uongozi ulionyooka na wenye uhadilifu."

Sitta alisema wananchi wasiwe na ndoto ya maisha bora kwa kila mtanzania ikiwa rushwa na ufisadi utaendelea kutawala na kufumbiwa macho.

"Ndugu zangu hatuwezi kupata maisha bora kama kiwango cha rushwa, ufisadi na dhuluma kikiwa hivi hivi tunavyokiona hivi sasa, kwa sababu Serikali ilileta utoaji pembejeo kwa kutumia vocha sasa tutaendelea vipi kama vocha zenyewe zinachakachuliwa?" alihoji.

"Iwapo tutadhibiti mianya ya ufisadi na rushwa, nchi yetu itainuka na kuweza kuwasaidia wazee wetu, wajane, watoto yatima kwa kuwapatia huduma nyingi nzuri, ilimradi tu ufisadi unatakiwa kupigwa vita kuanzia chini huku," alisema Sitta.

Sitta pia aliwaomba wajane hao na wazee kupita kila mahali na kuwashaui wananchi wao wakiwemo na wana CCM kuwa makini wa watu wanaojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za kisiasa na kiserikali wasije wakafanya makosa kuwaweka watu wenye nia mbaya na nchi hii kwa kujali matumbo yao na familia zao.

"Sasa hivi hata kule bungeni mnaona baadhi ya mawaziri, anatokea mtu amekuwa waziri ndani ya miaka 2 au chini ya hapo unasikia kanunua nyumba Mikocheni ya mabilioni, haiwezekani na wala haingii akilini hakuwa waziri wa wananchi huyu ameingia kuchuma tu," alisema.

Waziri Sitta amemaliza juzi ziara ya kiserikali ya siku tano mkoani humo alipokuwa akiangalia miradi mbalimbali inayohusiana na muingiliano wa uchumi na kijamii kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Huyu Mzee Sitta anongeaje? He is so contradictory sijui anajaribu kumzuga nani? Yeye na magamba CCM wenzake wakawang'oe magamba kwanza na kuwapeleka mafisadi wote mahakamani, wapitie mikataba mibovu na kuirekebisha, warudishe fedha zilizofichwa na mafisadi nje na wawaombe wananchi msamaha kwa kututesa miaka yote hii. So much could have been achieved but so much damage has been done. Mungu awalaani wote walioliangamiza taifa kwa matatizo yote kutokana na ubinafsi wao!!!!:angry:
 
Back
Top Bottom