Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,848
- 2,669
Opportunity cost ni the next best alternatiive. Cdm wana mawili; kutaka rufaa ama kukubali matokeo na kurudia uchaguzi. Kwa mtazamo wangu, kurudia uchaguzi ni gharama sana kwa upande wa muda na fedha, pengine hata maisha pia. Cdm mfanye tathmini ni gharama kiasi gani zilitumika Igunga, Arumeru, na sasa Arusha mjini. Kadhalika watazame na gharama za kurudia kesi.
Awali, kesi ya Lema haikupewa sana maana na wananchi kote Tanzania. Hukumu ya kesi imefungua masikio ya watanzania kote nchini na nje ya nchi. Kwa maana hii hata serikali imeshaona mwitikio wa watanzania katika kesi hii.
Kwa mujibu wa mawakili waliokuwa wakiendesha kesi hii upande wa Lema, wanasema kuwa kesi ilikuwa na dosari nyingi (sina sababu ya kuzirudia hapa). Sasa kwa mwendo huu ni wazi kuwa marudio ya kesi yatavuta hisia za watanzania kwa kiasi kikubwa zaidi na kupelekea serikali na mahakama kufikiria mara ya pili. Kwa hiyo wito wangu, kateni rufaa na mwisho wa siku jimbo litarudi cdm
Awali, kesi ya Lema haikupewa sana maana na wananchi kote Tanzania. Hukumu ya kesi imefungua masikio ya watanzania kote nchini na nje ya nchi. Kwa maana hii hata serikali imeshaona mwitikio wa watanzania katika kesi hii.
Kwa mujibu wa mawakili waliokuwa wakiendesha kesi hii upande wa Lema, wanasema kuwa kesi ilikuwa na dosari nyingi (sina sababu ya kuzirudia hapa). Sasa kwa mwendo huu ni wazi kuwa marudio ya kesi yatavuta hisia za watanzania kwa kiasi kikubwa zaidi na kupelekea serikali na mahakama kufikiria mara ya pili. Kwa hiyo wito wangu, kateni rufaa na mwisho wa siku jimbo litarudi cdm