Elections 2010 Arusha ubunge bado uko wazi kwa batilda,lema na lyimo

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,895
31,106
:peep: Wakuu baada ya kufanya tathimini nzito na yakina si kama zile Synovate na REDET nimebaini bila shaka yoyote wala ushabiki nafasi ya ubunge Arusha bado iko wazi kwa wagombea watatu Bwana G Lema CHADEMA,Bwana M Lyimo wa TLP na Mama Batilda Buriani wa CCM wote wana nafasi kubwa kuibuka na ushindi jimbo la Arusha mjini.

{1} Mama Batilda Buriani kwa wiki mbili sasa amekuwa akifanya kampeni za nguvu kubwa sana,ameweza kuwafikia wapiga kura wengi kwa mtindo wa nyumba kwa nyumba.CCM kiasi fulani wameweza kuwarejesha kundini baadhi ya wanachama wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakimsumbua Batilda.Batilda anategemea kupata kura nyingi kata ya Kati,kata za pembezoni zamani zilikuwa kata za wilaya ya Arumeru.Wapiga kura wazee ,wasiopenda fujo na wanaCCM wanategemewa kumpa kura Dr Batilda Buriani.Idadi ya wapiga siku ya uchaguzi ikiwa ndogo Dr Batilda atashinda kwakuwa atapata kura za wazee ambao si wengi kama wapiga kura vijana wenye mwamko mkubwa wa mageuzi.

{2] Bwana Macmillan Lyimo amejitahidi sana kuwafikia wapiga kura wengi hasa kata za Ungalimited,Sokoni 1,Sinoni,Lemara,Sombetini,Elerai,Matevesi na Terati [chuo cha VETA].Wananchi wengi hata wanachama wa vyama vya CCM na CHADEMA wanakubali bila ubishi Lyimo ni kichwa hana ubisho wala hatukani mtu kwenye mikutano yake.Bwana Lyimo anategemea kupata kura nyingi kwa watu wenye kupima uwezo wa mgombea kujenga hoja na kuitetea.Kampeni zake za nyumba kwa nyumba kwenye kata nilizozitaja zinaweza kumsaidia kupata kura nyingi.Wakongwe wa siasa za upinzani Arusha Mzee Kivuyo [diwani kata ya Sokoni 1 tangu 1995]na Meagie wamemsaidia Lyimo kuvuka viunzi vingi.TLP na CHADEMA wanaweza kugawana kura nyingi na kutoa mwanya mgombea wa CCM kushinda kwa ulaini.

{3} Bwana Godbless Lema amejitahidi sana kuwafikia wapiga kura wengi hasa kata za Kimandolu,Themi,Kaloleni,Levolosi,Ngarenaro.Lema anategemea kupata kura nyingi kutoka kwa vijana na watu wazima wanaotaka mabadiliko kwa namna yoyote[wapo watu wako tayari kupigia kura jiwe kuliko CCM].Hawajui kama yuko mpinzani mwingine wa kumpa kura zaidi ya Lema.Lema angekuwa na nusu ya uwezo wa Lyimo hakika Mama Batilda angefungasha virago siku nyingi.Mikutano mingi ya Lema imejaa balah blah na pumba nyingi kiasi nashindwa kuamini wapo watu wenye akili nzuri watakao mpigia kura.Elimu ya Bwana Lema imeendelea kumwangusha sana hasa siasa za majukwaani ameshindwa kujenga hoja za msingi badala yake amejikita zaidi kumshambulia Dr Batilda maisha yake binafsi na Lyimo ametumwa kumvurugia ? ?.Vipo vipeperushu ambavyo Lema amevitoa kwaajili ya kumsaidia kwenye kampeni zake taarifa za ndani [kanzi] zinachakachuliwa kuelezea ukihiyo wa Lema vinatarajiwa kutawanywa leo muda wowote kuanzia sasa.Wapiga kura wengi wakijitokeza Lema atashinda.TLP na CHADEMA wangekaa meza moja kazi ya kuiondoa CCM ingekuwa rahisi sana.

Kamanda PakaJimmy huo ndio utafiti wangu usishangae sana Mama akiibuka ushindi hatujawatendea haki waTanzania wapinzani lazima wajue watabeba zigo la lawama Arusha ikiangukia tena CCM.
 
Thanx for information, umetulia kweli kweli!! Ila watu wengi saizi wanataka mabadiliko, ningependa Dr Slaa aibuke mara moja awaonyeshe kazi kidogo hata nusu saa hivi ili amalize kazi kabisa.
 
Ngongo una nini na CHADEMA?

Subiri nije kivyengine, lakini elewa wazi kwamba utafiti wako si reality, na hujaweka wazi method uliyotumia kudadavua na kufikia hitimisho hilo!
Unajua upenzi ukimzidi mtu anakuwa kama kipofu...Ngongo hukuwepo Alhamisi pale NMC?...Ni nani aliyewahi kukusanya watu wengi vile?

Mimi nimeenda mbali zaidi kwa kuongea na watu mmojammoja, hakika nashangaa ni wapi ulikofanyia huo utafiti-kongwe!
 
Umejiuliza kwanini akina mama waliofanya Mkutano wao wa Saccos pale Metropole walimzomea na kumzodoa Batilda AMBAYE alijikaribisha bila mwaliko, na kisha kwa hasira wakampigia simu Lema aje kuongea nao, na ikaishia kuwa aibu kwa Mama?
Jiulize kwanini hawakumwita JAMAA YAKO KIPENZI LYIMO?
 
Ngongo una nini na CHADEMA?

Subiri nije kivyengine, lakini elewa wazi kwamba utafiti wako si reality, na hujaweka wazi method uliyotumia kudadavua na kufikia hitimisho hilo!
Unajua upenzi ukimzidi mtu anakuwa kama kipofu...Ngongo hukuwepo Alhamisi pale NMC?...Ni nani aliyewahi kukusanya watu wengi vile?

Mimi nimeenda mbali zaidi kwa kuongea na watu mmojammoja, hakika nashangaa ni wapi ulikofanyia huo utafiti-kongwe!

Kamanda soma tena na tena utanielewa mkubwa.Jana nilikuwa Mbuga ya chumvi hakuna niliongea na watu zaidi ya kumi hakuna aliyekuwa na habari ya mkutano wa NMC !.Halafu kuna suala la kuchakachua vipeperushi vya mgombea wako kabla siajenda kuswali vitakuwa tayari mitaani.Mkuu CCM wabaya wanatumia mbinu zozote ili kufanikisha malengo yao.
 
:peep: Wakuu baada ya kufanya tathimini nzito na yakina si kama zile Synovate na REDET nimebaini bila shaka yoyote wala ushabiki nafasi ya ubunge Arusha bado iko wazi kwa wagombea watatu Bwana G Lema CHADEMA,Bwana M Lyimo wa TLP na Mama Batilda Buriani wa CCM wote wana nafasi kubwa kuibuka na ushindi jimbo la Arusha mjini.

{1} Mama Batilda Buriani kwa wiki mbili sasa amekuwa akifanya kampeni za nguvu kubwa sana,ameweza kuwafikia wapiga kura wengi kwa mtindo wa nyumba kwa nyumba.CCM kiasi fulani wameweza kuwarejesha kundini baadhi ya wanachama wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakimsumbua Batilda.Batilda anategemea kupata kura nyingi kata ya Kati,kata za pembezoni zamani zilikuwa kata za wilaya ya Arumeru.Wapiga kura wazee ,wasiopenda fujo na wanaCCM wanategemewa kumpa kura Dr Batilda Buriani.Idadi ya wapiga siku ya uchaguzi ikiwa ndogo Dr Batilda atashinda kwakuwa atapata kura za wazee ambao si wengi kama wapiga kura vijana wenye mwamko mkubwa wa mageuzi.

{2] Bwana Macmillan Lyimo amejitahidi sana kuwafikia wapiga kura wengi hasa kata za Ungalimited,Sokoni 1,Sinoni,Lemara,Sombetini,Elerai,Matevesi na Terati [chuo cha VETA].Wananchi wengi hata wanachama wa vyama vya CCM na CHADEMA wanakubali bila ubishi Lyimo ni kichwa hana ubisho wala hatukani mtu kwenye mikutano yake.Bwana Lyimo anategemea kupata kura nyingi kwa watu wenye kupima uwezo wa mgombea kujenga hoja na kuitetea.Kampeni zake za nyumba kwa nyumba kwenye kata nilizozitaja zinaweza kumsaidia kupata kura nyingi.Wakongwe wa siasa za upinzani Arusha Mzee Kivuyo [diwani kata ya Sokoni 1 tangu 1995]na Meagie wamemsaidia Lyimo kuvuka viunzi vingi.TLP na CHADEMA wanaweza kugawana kura nyingi na kutoa mwanya mgombea wa CCM kushinda kwa ulaini.

{3} Bwana Godbless Lema amejitahidi sana kuwafikia wapiga kura wengi hasa kata za Kimandolu,Themi,Kaloleni,Levolosi,Ngarenaro.Lema anategemea kupata kura nyingi kutoka kwa vijana na watu wazima wanaotaka mabadiliko kwa namna yoyote[wapo watu wako tayari kupigia kura jiwe kuliko CCM].Hawajui kama yuko mpinzani mwingine wa kumpa kura zaidi ya Lema.Lema angekuwa na nusu ya uwezo wa Lyimo hakika Mama Batilda angefungasha virago siku nyingi.Mikutano mingi ya Lema imejaa balah blah na pumba nyingi kiasi nashindwa kuamini wapo watu wenye akili nzuri watakao mpigia kura.Elimu ya Bwana Lema imeendelea kumwangusha sana hasa siasa za majukwaani ameshindwa kujenga hoja za msingi badala yake amejikita zaidi kumshambulia Dr Batilda maisha yake binafsi na Lyimo ametumwa kumvurugia ? ?.Vipo vipeperushu ambavyo Lema amevitoa kwaajili ya kumsaidia kwenye kampeni zake taarifa za ndani [kanzi] zinachakachuliwa kuelezea ukihiyo wa Lema vinatarajiwa kutawanywa leo muda wowote kuanzia sasa.Wapiga kura wengi wakijitokeza Lema atashinda.TLP na CHADEMA wangekaa meza moja kazi ya kuiondoa CCM ingekuwa rahisi sana.

Kamanda PakaJimmy huo ndio utafiti wangu usishangae sana Mama akiibuka ushindi hatujawatendea haki waTanzania wapinzani lazima wajue watabeba zigo la lawama Arusha ikiangukia tena CCM.
hebu jifunze kuandika kwenye public forum, hayo maandihi yanaumiza macho tu hapa... ushakua redet na wewe
 
Umejiuliza kwanini akina mama waliofanya Mkutano wao wa Saccos pale Metropole walimzomea na kumzodoa Batilda AMBAYE alijikaribisha bila mwaliko, na kisha kwa hasira wakampigia simu Lema aje kuongea nao, na ikaishia kuwa aibu kwa Mama?
Jiulize kwanini hawakumwita JAMAA YAKO KIPENZI LYIMO?


Hawakuwa na namba yake ya simu bwaha ha ha.
 
Ngongo kwa contradictions!

Ni nani waliokuwa wakisambaza vipeperushi vya kumkashifu Lema? Tena vilikuwa vinasambazwa na watu wa CCM [habari hizo ziliandikwa mpaka kwenye gazeti la Raia Mwema] na wewe mwenyewe uliandika hapa.

Ajabu ni kwamba unaona mashambulizi ya Lema majukwaani lakini hayo yaliyoandikwa kwenye vipeperushi huyaoni. Tena wewe ulikuwa mstari wa mbele kushabikia habari hizo, mara Lema tapeli, mara sijui shule yake imefanyaje, mara Lema aliuza ubunge. Kama ni tapeli na waliotapeliwa wapo kwanini hawampeleki mahakamani? Kama ni Kihiyo unadhani CCM wangehangaika kumaliza hela wakati kuna short cut ya kummaliza na hivyo kushinda kilaini?

Swali la mwisho kwako Bwana Ngongo, katika kasheshe zote sijasikia Dr. Burian akimtaja Lyimo au CCM wakilia na TLP, siku zote hapo Arusha Mjini tangu kampeni zimeanza wanalia na CHADEMA na Lema, hiyo ni dalili kwamba upinzani ambao CCM wanauogopa kwa hapo Arusha Mjini ni wa kutoka kwa Lema na siyo kwa Bwana Lyimo. So, utafiti wako una walakini.
 
NGONGO,
Agenda yako iko wazi kabisa ,umejitahidi kui'comouflage kwa siku nyingi, lakini mwishowe imekuwia ngumu kuificha!...ni kama mvi, utazipaka piko wee, lakini zinaonekana tu.
Wewe jitihada zako zote hapa mtandaoni ni kuhakikisha unampa jina baya Lema, kumpa kesi ambazo hata hivyo haziendi mahakamani wala hukumu zake kujulikana zimeishia wapi.
Mara kaiba gari, kakamatwa na polisi, katukana...aisee, we are now fed up, na jaribu kuficha kisasi!
Lema atakuwa Mbunge wako, na ni bora ukajifunza kumzowea na kumkubali!
 
Kamanda soma tena na tena utanielewa mkubwa.Jana nilikuwa Mbuga ya chumvi hakuna niliongea na watu zaidi ya kumi hakuna aliyekuwa na habari ya mkutano wa NMC !.Halafu kuna suala la kuchakachua vipeperushi vya mgombea wako kabla siajenda kuswali vitakuwa tayari mitaani.Mkuu CCM wabaya wanatumia mbinu zozote ili kufanikisha malengo yao.
Shida yako unaongea na watu ambao unajua kabisa wameenda pale mnadani kuuza "lukaria" (dawa zakimasai) ili wapate buku-jero wachape mwendo vijijini...
Wale unaoongea nao hawana hata shahada, wanachojali ni kuswaga punda aliyebeba mkaa ---basi!

Nijuacho mimi ni kwamba Mbuga ya Chumvi pako active sana ukiongea na watu sahihi...Najua kuna jamaa yako pale anaitwa CHIPAKA, ndiye unaemuuliza mambo yako, wakati unajua kabisa kuwa ni mgombea udiwani wa TLP, na hivyo atakudanganya ufurahi...Yule jamaako anatuhumiwa kuuza vibanda vile kinyume na taratibu, na yeye binafsi kajiuzia zaidi ya vibanda 20!...imagine, na bado anataka udiwani!

Endelea kudanganyika broda, you are entitled to that!
 
Shida yako unaongea na watu ambao unajua kabisa wameenda pale mnadani kuuza "lukaria" (dawa zakimasai) ili wapate buku-jero wachape mwendo vijijini...
Wale unaoongea nao hawana hata shahada, wanachojali ni kuswaga punda aliyebeba mkaa ---basi!

Nijuacho mimi ni kwamba Mbuga ya Chumvi pako active sana ukiongea na watu sahihi...Najua kuna jamaa yako pale anaitwa CHIPAKA, ndiye unaemuuliza mambo yako, wakati unajua kabisa kuwa ni mgombea udiwani wa TLP, na hivyo atakudanganya ufurahi...Yule jamaako anatuhumiwa kuuza vibanda vile kinyume na taratibu, na yeye binafsi kajiuzia zaidi ya vibanda 20!...imagine, na bado anataka udiwani!

Endelea kudanganyika broda, you are entitled to that!

Heshima kwako PakaJimmy,


Mkuu umefuatilia post vizuri ukisoma bandiko langu bila shaka utabaini nimeweka wazi kabisa,Wagombea wote wana nafasi ya kushinda ubunge Arusha mjini inategemea mbinu zitakazotumiwa na wagombea ubunge siku za mwisho.Majibu ya baadhi ya wachangiaji yanatia shak na kusikitisha sana wengine wanajibu utafikiri nimesema Lema atashindwa au hana nafasi ya kushinda.Wengine wanataka kulazimisha ushindi wa Lema kwasababu ya mkutano wa NMC.Wachangiaji hawa wanajua Lema hana shule wanajua Lema anatukana kwenye mikutano yake ya kampeni wanadhani mkutano mmoja wa NMC unatosha kuondoa dosari zote.

Narudia tena na tena Batilda B,Lyimo M na G Lema wote wana nafasi ya kushinda ubunge jimbo la Arusha.Inaelekea baadhi ya member JF wanataka kusikia habari za upande mmoja tu.Wakuu nimesema na nitaendelea kusema wapinzania wanaweza kukwaruzana na kusababisha mgombea wa CCM kushinda.
 
Ngongo kwa contradictions!

Ni nani waliokuwa wakisambaza vipeperushi vya kumkashifu Lema? Tena vilikuwa vinasambazwa na watu wa CCM [habari hizo ziliandikwa mpaka kwenye gazeti la Raia Mwema] na wewe mwenyewe uliandika hapa.

Ajabu ni kwamba unaona mashambulizi ya Lema majukwaani lakini hayo yaliyoandikwa kwenye vipeperushi huyaoni. Tena wewe ulikuwa mstari wa mbele kushabikia habari hizo, mara Lema tapeli, mara sijui shule yake imefanyaje, mara Lema aliuza ubunge. Kama ni tapeli na waliotapeliwa wapo kwanini hawampeleki mahakamani? Kama ni Kihiyo unadhani CCM wangehangaika kumaliza hela wakati kuna short cut ya kummaliza na hivyo kushinda kilaini?

Swali la mwisho kwako Bwana Ngongo, katika kasheshe zote sijasikia Dr. Burian akimtaja Lyimo au CCM wakilia na TLP, siku zote hapo Arusha Mjini tangu kampeni zimeanza wanalia na CHADEMA na Lema, hiyo ni dalili kwamba upinzani ambao CCM wanauogopa kwa hapo Arusha Mjini ni wa kutoka kwa Lema na siyo kwa Bwana Lyimo. So, utafiti wako una walakini.


Heshima kwako Keil,

Mkuu Lema ni tapeli hilo halina ubishi wala mjadala kinachomsaidia sasa ni busara na msimamo wa kamanda wa polisi mkoa Arusha B Matei kwamba hatamfungulia Lema mashitaka kipindi cha uchaguzi labda kama atapatikana na kosa la mauaji.Kesi nyingi ziko polisi nina hakika hata viongozi wakuu wa CHADEMA wanajua mwisho wa mgombea wao si mzuri [akishinda au akishindwa lazima ataburuzwa mahakamani].

Batilda hawezi kumgusa mgombea wa TLP kwasababu hajawahi kumtukana wala kumzushia kashfa ya aiana yoyote.Kwa taarifa yako CCM wanatumia mbinu mbali mbali wafuasi wao wasihudhurie mikutano ya Bwana Lyimo kwakujua watapata darsa zuri la maendeleo yao.CCM wanawaimiza wafuasi wake kuhudhuria mikutano ya Lema kwakujua watapata misamiati mipya ya matusi.

Mkuu umeshindwa kuelewa kitu kimoja muhimu sana.Nilisema kanzi kamenasa habari za ndani za CCM kuvichakachua vipeperushi rasmi vya Lema kwa kuongeza kigezo cha elimu [vipeperushi rasmi vya Lema havijagusia suala la Elimu]
 
Umejiuliza kwanini akina mama waliofanya Mkutano wao wa Saccos pale Metropole walimzomea na kumzodoa Batilda AMBAYE alijikaribisha bila mwaliko, na kisha kwa hasira wakampigia simu Lema aje kuongea nao, na ikaishia kuwa aibu kwa Mama?
Jiulize kwanini hawakumwita JAMAA YAKO KIPENZI LYIMO?

Saccos ngapi bwana.

Kila la kheri Batilda.
 
.Wengine wanataka kulazimisha ushindi wa Lema kwasababu ya mkutano wa NMC.Wachangiaji hawa wanajua Lema hana shule wanajua Lema anatukana kwenye mikutano yake ya kampeni wanadhani mkutano mmoja wa NMC unatosha kuondoa dosari zote.[/B][/SIZE][/FONT]

Narudia tena na tena Batilda B,Lyimo M na G Lema wote wana nafasi ya kushinda ubunge jimbo la Arusha.Inaelekea baadhi ya member JF wanataka kusikia habari za upande mmoja tu.Wakuu nimesema na nitaendelea kusema wapinzania wanaweza kukwaruzana na kusababisha mgombea wa CCM kushinda.
Alimtukana nani?

anayedai kutukanwa Dar-Mwembeyanga hujamsikia?..ni matusi yale?(Asiyefunzwa na mamaye...!)..kama ndivyo kwanini asishtakiwe?

Lakini hujanijibu kuwa kesi zote za Lema unazodai ameshitakiwa au amewekwa polisi, zinaishia wapi?
Ngongo kuwa objective, wewe ndiye unalazimisha watu wakuamini wakati unaelewa kuwa unafosi!
Lakini pia hilo suala la shule(najua ni hoja-pandikizi tu), hukumsikia Dr Slaa juzi?...WEnye PHD akina Balali wameishia wapi?...DrKikwete?...Dr Batilda?...unakiona wanachokifanya na doctorate zao?

Tunataka mtendaji Arusha..NIMEMALIZA!
 
Alimtukana nani?

anayedai kutukanwa Dar-Mwembeyanga hujamsikia?..ni matusi yale?(Asiyefunzwa na mamaye...!)..kama ndivyo kwanini asishtakiwe?

Lakini hujanijibu kuwa kesi zote za Lema unazodai ameshitakiwa au amewekwa polisi, zinaishia wapi?
Ngongo kuwa objective, wewe ndiye unalazimisha watu wakuamini wakati unaelewa kuwa unafosi!
Lakini pia hilo suala la shule(najua ni hoja-pandikizi tu), hukumsikia Dr Slaa juzi?...WEnye PHD akina Balali wameishia wapi?...DrKikwete?...Dr Batilda?...unakiona wanachokifanya na doctorate zao?

Tunataka mtendaji Arusha..NIMEMALIZA!


Heshima kwako PakaJimmy,

Soma post # 17 utaelewa kesi zimeishia wapi na lini zitaanza kunguruma bila kujali matokeo ya uchaguzi,sijui wakati huo itakuwa mbunge wa Arusha ashitakiwa kwa kosa la kutapeli au itakuwa Bwana Godbless Lema ashitakiwa kwa kosa la .............Mkuu subira yavuta heri leo ni tarehe 29/10/2010 bado siku mbili masuala ya uchaguzi yatakuwa history,makosa yaliyotendwa na wagombea yatachukua nafasi yake bila shaka utakuja kiri siku moja kwamba kuna jamaa JF aliwahi kutuambia tukabisha.
 
Back
Top Bottom