Mimi nimebahatika kuishi Arusha, Mwanza na Dar-es-salaam . Lakini nimekulia Arusha na naomba niweke hilo wazi.
Arusha ni sehemu tofauti sana Tanzania kwa mawazo yangu na kuna mengi mazuri Arusha kwa nchi kuliko tunavyojua. Dar imeendelea zaidi lakini kuna serikali, Bandari, bahari n.k ambazo ni muhimu sana kwa nchi lakini naomba nieleze mazuri ya Arusha.
1. Kutokuwa na Serikali: Kwasababu hakuna wafanyakazi wengi wa serikali kama Dar rushwa sio nyingi sana. Dar wafanyakazi wengi wa serikali wamakuwa wakitafuta pesa za rushwa kama biashara vile hivyo kila unachofanya kuanzia kupima viwanja mpaka kuweka maji inakuwa kama ni vigumu lakini ni kwasababu ya serikali kuwa kwenye kila kitu (Too much regulations). Hii imesaidia kupunguza gharama za biashara
2. Jasirimali: Nenda Arusha leo uangalie Majengo ya Mjini ni nani anayamiliki si serikali wala NSSF bali ni Watanzania wa kawaida wafanya biashara. Hii inatokana na ukweli kwamba kwasababu hakuna serikali watu wengi wakikua hata mimi binafsi nilikuwa sitegemei kufanya kazi serikalini kwasababu hizo kazi hazipo na kama zipo mwajiri yupo Dar na siyo Arusha. Vilevile kuna mwamko kwamba huhitaji kutegemea mtu unaweza kufanya mwenyewe ukiwa Arusha. Vijana wengi wameanzisha vi kampuni vya kuetembeza wageni, kukata ticket, kuuza vitu vya sanaa, kuuza madini na kukata madini. Kwa ujumla serikali kutokuwepo Arusha ni kitu kizuri na sio kitu kibaya kwa wafanyabiashara kwani Dar ukisha pandisha ghorofa TRA wanaona deal.
3. Serikali: Serikali ni tatizo mfano serikali ilichukua viwanja vya madini ya Tanzanite na kuwapa wawekezaji hivyo serikali inachopata hatukioni ni bora ingewaachia wananchi tungeona maghorofa zaidi mijini, shule za binafsi, na biashara nyingi za wazawa badala ya sasa wameua soko la Tanzanite, hakuna ushindani kama zamani na gharama za biashara zimeenda juu. Kwa ujumla serikali yetu ni tatizo kwa nchi ni bora wangewaachia wananchi wajenge nchi yao.
4. Mashamba: Wakati tumeanza kuona sehemu chache nchini zimeanza kilimo cha kisasa Arusha wameanza kilimo cha kisasa sikunyingi sana kuanzia mashamba ya kahawa, maua, miwa, karanga na ngano. Wakina Mzee Mtei wa chadema na Mzee wa Prec Air wamepata utajiri kwenye kilimo. Sasa tuangalie sehemu nyingine za nchi serikali ndiyo inataka isaini mikataba ya Kilimo kuanzia Kigoma, Morogoro, na Kagera wakati hayo mashamba Watanzania wenyewe wangeweza kuingia mikataba moja kwa moja na wawekezaji au hata wakafanya wenyewe. Kama unataka kujua kuna watanzania wanaweza kulima kisasa bila mikataba ya serikali basi nenda Arusha. Tatizo kubwa la serikali na hawa wawekezaji ni kwamba si wenyeji na hawata wekeza pale. Serikali ina viongozi wanaotafuta 10% na wawekezaji wanatafuta materials wapeleke nje. Na hii ni tatizo kubwa kwenye madini pia.
Mwanza ineweka ikawa zaidi ya Arusha lakini bahati mbaya ndugu zetu kule walisahaulika kwenye miundo minu kwa muda na serikali imeingia kwa kasi sana kwenye maisha yao hasa madini na samaki.
Mimi kwa mawazo yangu Arusha ilikuwa inaenda vizuri na ni mfano mzuri wa serikali kuwa ndogo na kuwaachia wananchi walete maendeleo yao wenyewe. Watanzania wanajipenda na wanapenda maendeleo na kitu kikubwa ni kwamba serikali iko sana kwenye maisha yao. Serikali ya Tanzania inatakiwa kutoa huduma muhimu na biashara iachie wananchi wenyewe wafanye. Huwezi kuzuia watu wa Mwanza kufanya biashara ya uvuvi halafu ukategemea kuendeleza Mwanza, huwezi kunyanganya watu wa Arusha Tanzanite na tukategemea maendeleo, hatuwezi kunyanganya watu washamba na tukategemea maendeleo. Kuna vitu kama Kuchimba mafuta na gas ambavyo vinahitaji kampuni kubwa lakini vitu ambavyo wananchi wanaweza kufanya serikali inabidi iondoke na kuwaachia wananchi. Kwani serikali ijiingize kwenye mikataba ya mashamba!
Arusha ni sehemu tofauti sana Tanzania kwa mawazo yangu na kuna mengi mazuri Arusha kwa nchi kuliko tunavyojua. Dar imeendelea zaidi lakini kuna serikali, Bandari, bahari n.k ambazo ni muhimu sana kwa nchi lakini naomba nieleze mazuri ya Arusha.
1. Kutokuwa na Serikali: Kwasababu hakuna wafanyakazi wengi wa serikali kama Dar rushwa sio nyingi sana. Dar wafanyakazi wengi wa serikali wamakuwa wakitafuta pesa za rushwa kama biashara vile hivyo kila unachofanya kuanzia kupima viwanja mpaka kuweka maji inakuwa kama ni vigumu lakini ni kwasababu ya serikali kuwa kwenye kila kitu (Too much regulations). Hii imesaidia kupunguza gharama za biashara
2. Jasirimali: Nenda Arusha leo uangalie Majengo ya Mjini ni nani anayamiliki si serikali wala NSSF bali ni Watanzania wa kawaida wafanya biashara. Hii inatokana na ukweli kwamba kwasababu hakuna serikali watu wengi wakikua hata mimi binafsi nilikuwa sitegemei kufanya kazi serikalini kwasababu hizo kazi hazipo na kama zipo mwajiri yupo Dar na siyo Arusha. Vilevile kuna mwamko kwamba huhitaji kutegemea mtu unaweza kufanya mwenyewe ukiwa Arusha. Vijana wengi wameanzisha vi kampuni vya kuetembeza wageni, kukata ticket, kuuza vitu vya sanaa, kuuza madini na kukata madini. Kwa ujumla serikali kutokuwepo Arusha ni kitu kizuri na sio kitu kibaya kwa wafanyabiashara kwani Dar ukisha pandisha ghorofa TRA wanaona deal.
3. Serikali: Serikali ni tatizo mfano serikali ilichukua viwanja vya madini ya Tanzanite na kuwapa wawekezaji hivyo serikali inachopata hatukioni ni bora ingewaachia wananchi tungeona maghorofa zaidi mijini, shule za binafsi, na biashara nyingi za wazawa badala ya sasa wameua soko la Tanzanite, hakuna ushindani kama zamani na gharama za biashara zimeenda juu. Kwa ujumla serikali yetu ni tatizo kwa nchi ni bora wangewaachia wananchi wajenge nchi yao.
4. Mashamba: Wakati tumeanza kuona sehemu chache nchini zimeanza kilimo cha kisasa Arusha wameanza kilimo cha kisasa sikunyingi sana kuanzia mashamba ya kahawa, maua, miwa, karanga na ngano. Wakina Mzee Mtei wa chadema na Mzee wa Prec Air wamepata utajiri kwenye kilimo. Sasa tuangalie sehemu nyingine za nchi serikali ndiyo inataka isaini mikataba ya Kilimo kuanzia Kigoma, Morogoro, na Kagera wakati hayo mashamba Watanzania wenyewe wangeweza kuingia mikataba moja kwa moja na wawekezaji au hata wakafanya wenyewe. Kama unataka kujua kuna watanzania wanaweza kulima kisasa bila mikataba ya serikali basi nenda Arusha. Tatizo kubwa la serikali na hawa wawekezaji ni kwamba si wenyeji na hawata wekeza pale. Serikali ina viongozi wanaotafuta 10% na wawekezaji wanatafuta materials wapeleke nje. Na hii ni tatizo kubwa kwenye madini pia.
Mwanza ineweka ikawa zaidi ya Arusha lakini bahati mbaya ndugu zetu kule walisahaulika kwenye miundo minu kwa muda na serikali imeingia kwa kasi sana kwenye maisha yao hasa madini na samaki.
Mimi kwa mawazo yangu Arusha ilikuwa inaenda vizuri na ni mfano mzuri wa serikali kuwa ndogo na kuwaachia wananchi walete maendeleo yao wenyewe. Watanzania wanajipenda na wanapenda maendeleo na kitu kikubwa ni kwamba serikali iko sana kwenye maisha yao. Serikali ya Tanzania inatakiwa kutoa huduma muhimu na biashara iachie wananchi wenyewe wafanye. Huwezi kuzuia watu wa Mwanza kufanya biashara ya uvuvi halafu ukategemea kuendeleza Mwanza, huwezi kunyanganya watu wa Arusha Tanzanite na tukategemea maendeleo, hatuwezi kunyanganya watu washamba na tukategemea maendeleo. Kuna vitu kama Kuchimba mafuta na gas ambavyo vinahitaji kampuni kubwa lakini vitu ambavyo wananchi wanaweza kufanya serikali inabidi iondoke na kuwaachia wananchi. Kwani serikali ijiingize kwenye mikataba ya mashamba!