Arusha kwa sasa KWISHNEY!

GeniusBrain

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
4,315
306
Nashukuru na nimeliona limeandikwa pia kwenye blog ya michuzi. Tuacheni utani na masihara mji wa Arusha kwa sasa una hali mbaya sana. Hali ya mji wa Arusha kiuchumi kwa sasa sio maridhawa kabisa. Nilijaribu kutembelea maeneo mengi ya kibiashara km sokoni ambapo kuna maduka mbali mbali . Ikifika saa 10 tu jioni wanaanza kufunga hakuna wateja, hata zile siku za kawaida za kazi. Biashara za taxi , ma-bus ndio usiseme, karibia 90% ni mbovu mbovu sana. Hali ya usafi wa mji ni mbaya sana. Kwa kweli , wana JF tuna haja yakuutizama upya mji huu, GENEVA OF AFRICA INAPOTEA KWENYE RAMANI
 
We unasema Arusha. Nchi imekwisha hii, kila kona ukienda watua ni wakali kweli. Hali ni mbaya kweli kweli. Utapeli umezidi, yaani nashukuru tu kuna amani.
 
Watajuta kwanini walimchagua yule kichaa, sasa hawana hata wa kuwa wakilisha Bungeni
 
Maisha ni magumu, watu hawana fedha. Ni tatizo la uchumi wa nchi. Nahisi wewe unataka kuunganisha Arusha na siasa za CDM. Mtwara kuna maisha mazuri? Kuna biashara nzuri toka asubuhi hadi usiku?
 
hali ni mbaya nchi nzima. wewe unashangaa arusha. hata hayo unayosema sii sahihi hali ipo kama kawaida.
 
Maisha ni magumu, watu hawana fedha. Ni tatizo la uchumi wa nchi. Nahisi wewe unataka kuunganisha Arusha na siasa za CDM. Mtwara kuna maisha mazuri? Kuna biashara nzuri toka asubuhi hadi usiku?
Sio watu hawana hela, sema wewe huna hela.
 
Kamradi ka matofali toka bmoyo kataleta tofali kuanzia kesho, si umemwona jakaya alivyoanzisha bonge la mradi wa matofali huko bmoyo!
 
kuzorota kwa biashara ya Tanzanite kwa KIASI kikubwa imeathiri Hali ya uchumi katika jiji la Arusha, na hili limetokea baada ya mwekezaji..... Lakini pia utalii kwa Sasa sio kiviile na low season ndo hiyo inaishia na pia kukosekana kwa viwanda vingi IDADI Kubwa ya watu haina ajira.... Lingine pia ni Kuwa Sasa upatikanaji wa bidhaa umekua rahisi zaidi unamfikia Mtu hadi nyumbani so watu hawana time ya kwenda madukani mjini, tembelea katika viunga vya mji wa Arusha Kama kijenge zote Mwanama na ya juu, ngarenaro, sekei, ngulelo, kwa mrefu, sakina, kwa iddy, ilboru...... Kote huko Unakuta "Visuper Market" pamoja na vihardware, so tathimini yako ya kuangalia maduka ni irrelevant ingawa kiukweli uchumi wa Arusha umeshuka
 
Sinafuu ya Arusha je moshi maisha kwa kweli yamekaba na sio miji hii tu karibia nchi nzima
 
Watajuta kwanini walimchagua yule kichaa, sasa hawana hata wa kuwa wakilisha Bungeni

Acha ushamba mkuu si vyema kumwita mh. Mbunge G. Lema Kichaa. Je walikochagua wenye akili timamu hali za majimbo yao zikoje ukilinganisha na Arusha? Hivi huyu anayelalamika alitaka akipita mjini watu wamnunulie soda na chips ndo ajue hali ya Arusha ni nzuri? hli ya Arusha haina tofauti kiuchumi na mikoa mingine. Kigezo ambacho angekitumia ni kwenda TRA kuangalia kama mapato yameshuka kwa kiasi gani kutokana na watu kufunga biashara. Ujinga alioleta hapa hatujui unalengo gani kwani hata mikoa kama Mwanza, Morogororo na Dar hali sio nzuri je huko nako kuna Vichaa wabunge?
 
Acha ushamba mkuu si vyema kumwita mh. Mbunge G. Lema Kichaa. Je walikochagua wenye akili timamu hali za majimbo yao zikoje ukilinganisha na Arusha? Hivi huyu anayelalamika alitaka akipita mjini watu wamnunulie soda na chips ndo ajue hali ya Arusha ni nzuri? hli ya Arusha haina tofauti kiuchumi na mikoa mingine. Kigezo ambacho angekitumia ni kwenda TRA kuangalia kama mapato yameshuka kwa kiasi gani kutokana na watu kufunga biashara. Ujinga alioleta hapa hatujui unalengo gani kwani hata mikoa kama Mwanza, Morogororo na Dar hali sio nzuri je huko nako kuna Vichaa wabunge?

Rekebisha kidogo hapo, ni Lema sio mheshimiwa mbunge. Halafu hivi wewe umeenda Mwanza hivi karibuni? Nakushauri uende ukaone biashara inavyo kwenda.
 
kuzorota kwa biashara ya Tanzanite kwa KIASI kikubwa imeathiri Hali ya uchumi katika jiji la Arusha, na hili limetokea baada ya mwekezaji..... Lakini pia utalii kwa Sasa sio kiviile na low season ndo hiyo inaishia na pia kukosekana kwa viwanda vingi IDADI Kubwa ya watu haina ajira.... Lingine pia ni Kuwa Sasa upatikanaji wa bidhaa umekua rahisi zaidi unamfikia Mtu hadi nyumbani so watu hawana time ya kwenda madukani mjini, tembelea katika viunga vya mji wa Arusha Kama kijenge zote Mwanama na ya juu, ngarenaro, sekei, ngulelo, kwa mrefu, sakina, kwa iddy, ilboru...... Kote huko Unakuta "Visuper Market" pamoja na vihardware, so tathimini yako ya kuangalia maduka ni irrelevant ingawa kiukweli uchumi wa Arusha umeshuka

I support you 100% kama mkazi wa Arusha. Uchumi umeshuka kutokana na machimbo ya Tanzanite kupewa Makaburu tofauti na zamani wakati wazawa ndo walikuwa wachimbaji kiasi kwamba impact ya wao kuwa na kipato ilionekana mji mzima . Makaburu wanapeleka hela zote SA kwa hiyo asilaumiwe Mbunge kwani yeye si TIC wanaouza nchi.
 
Rekebisha kidogo hapo, ni Lema sio mheshimiwa mbunge. Halafu hivi wewe umeenda Mwanza hivi karibuni? Nakushauri uende ukaone biashara inavyo kwenda.

Whatever you call it ukweli unajulikana kwani hata waalimu na mabalozi wastaafu huendelea kuitwa Mabalaozi why don't we respect our MP ambaye rufaa yake haijamtupa. Chuki binafsi zitakupunguzia umri mkuu try to show love even to your enemy
 
Kwa hiyo mnataka kusema shauri ya CHADEMA ili musikilize watu wanasemaje? Hali ni mbaya kote sababu ya CCM.
 
Nashukuru na nimeliona limeandikwa pia kwenye blog ya michuzi. Tuacheni utani na masihara mji wa Arusha kwa sasa una hali mbaya sana. Hali ya mji wa Arusha kiuchumi kwa sasa sio maridhawa kabisa. Nilijaribu kutembelea maeneo mengi ya kibiashara km sokoni ambapo kuna maduka mbali mbali . Ikifika saa 10 tu jioni wanaanza kufunga hakuna wateja, hata zile siku za kawaida za kazi. Biashara za taxi , ma-bus ndio usiseme, karibia 90% ni mbovu mbovu sana. Hali ya usafi wa mji ni mbaya sana. Kwa kweli , wana JF tuna haja yakuutizama upya mji huu, GENEVA OF AFRICA INAPOTEA KWENYE RAMANI


Mbona juzi juzi tuu jiji la Arusha na Manispaa ya Moshi imetajwa kama miji misafi hapa nchini? Huwezi kupima uchumi wa Arusha kwa kuangalia uchangamfu wa biashara katika maduka ya stendi ndogo hasa msimu huu ambao siyo wa sikukuu.
 
Uchafu ni sahihi ila swala la ugumu wa maisha ni tz nzima.
Swala la maduka eti kukosa wateja labda utruelezee umetumia analysis ipi kufanya hiyo research.
Kuhusu swala usafiri naamini umepotoka, sasa watu wasipo safiri shuhuli za kawaida za maisha zinaendaje?
Mwisho, hapa kwetu pesa ni ngumu na maisha ni juu siku zote tumezoea wewe unashangaa coz ni mgeni hapa.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom