Kiungani
JF-Expert Member
- Feb 2, 2007
- 274
- 71
Kwa mara nyingine tena CCM imejikuta katika uchaguzi ambao unakifanya chama kiwe na kionyeshe msimamo wa sera zake, hasa mapambano dhidi ya ufisadi na kuvuana magamba.
Kipimo cha kwanza kilikuwa Igunga, ambapo mgombea wao Dr. Kafumu aliibuka kidedea. Kugombea na kushinda kwa Kafumu kule Igunga inaweza kutafsiriwa kama ni ushindi dhidi ya Ufisadi haswa ikitiliwa maanani kuwa Rostam Aziz, mtuhumiwa wa ufisadi CCM, ilibidi aachie hicho kiti. Hata hivyo huu mtihani wa Igunga haukuwa mgumu sana kwani ilikuwa ni rahisi kwa CCM kuonyesha kuwa katoka fisadi Rostam anaingia Kafumu, ambaye ni kitu kingine tofauti (japo kuna watakaodai kuwa naye ni fisadi pia).
Kwa Arumeru, pamoja na kuwa kiti kimekuwa wazi kwa mapenzi ya Mungu kufuatia kifo cha Mzee Jeremiah Sumari, lakini uzibaji wa pengo hilo ni mtihani mkubwa kwa CCM.
Mshindi wa kura za maoni ndani ya CCM ni Sioi Sumari, mtoto wa kiume wa Mzee Jeremiah Sumari. Kama ada, NEC ya CCM itakaa na kupitisha jina la mgombea wa CCM kama ilivyo taratibu za chama, na bila kutengua matokeo ya kura za maoni, basi mgombea wa CCM atakuwa ni Sumari.
Kwa angalizo la haraka haraka, hapa inaonekana kama siyo tatizo hata kidogo. Mzee Sumari kafariki, mtoto wake kashinda kura za maoni na kupitishwa na NEC kama mgombea halali. Hakuna shida, siyo? La hasha.
Tukiangalia kwa undani, kuna ugumu kuliko picha ya awali. Kijana Sioi Sumari, ni mkwe kwa kumuoa binti mkubwa wa Edward Lowassa. Kijana Sumari amekuwa karibu zaidi sana na wakwe zake akina Lowassa kiasi kwamba anafahamika na hata yeye kujitambulisha kama mmojawapo ya watu wachache sana ambao wana sikio la Lowassa, wakati wowote. Familia ya Lowassa imefungamana sana na familia ya Sumari, na huwezi kupenyesha hata upana wa nywele katika mfungamano huo.
Ni wazi na kwa mantiki ya kawaida kuwa Sumari alipata ushauri na pengine baraka pia za mke wake, binti Lowassa, na si ajabu pia hata wakwe zake ili aweze kugombea kiti hiki cha Arumeru. Kushinda au kushindwa itategemea pia na support anayopata kutoka kwa chama na ndugu, wakiwapo pia wakwe zake, Lowassa.
Sidhani kama CCM itafumbia macho ukweli huo, na kama ni hivyo je, CCM itasimama bega kwa bega na Sumari, Lowassa huko Arumeru? Je, ikifanya hivyo CCM itakuwa inatuma ujumbe gani kwa Lowassa na wana-CCM kuhusu suala la kuvuana gamba?
CCM inaonyesha kuelekeza nguvu zake Arumeru kwani Mwigulu Nchemba tayari katumwa kupeleka majeshi na takrima Arusha. Kwa hiyo uwezekano kuwa CCM itajitenga na Arumeru ni mdogo, ila CCM NEC bado inaweza kumuengua Sumari asiwe mgombea wa CCM. Hali hiyo ikitokea (binafsi sidhani kama itakuwa hivyo, na kauli za Tendwa ni uthibitisho kuwa Sumari anabebwa), je Lowassa atasimama kidete kutetea Arumeru kama alivyomsaidia Mzee Sumari mwaka 2010?
Arumeru ni kipimo kizuri kwa CCM kuhusu aidha kuachana na gamba, fisadi Lowassa na tawi lake Sumari au kuukumbatia u-CCM na magamba na ufisadi wake sasa na hata milele.
Kipimo cha kwanza kilikuwa Igunga, ambapo mgombea wao Dr. Kafumu aliibuka kidedea. Kugombea na kushinda kwa Kafumu kule Igunga inaweza kutafsiriwa kama ni ushindi dhidi ya Ufisadi haswa ikitiliwa maanani kuwa Rostam Aziz, mtuhumiwa wa ufisadi CCM, ilibidi aachie hicho kiti. Hata hivyo huu mtihani wa Igunga haukuwa mgumu sana kwani ilikuwa ni rahisi kwa CCM kuonyesha kuwa katoka fisadi Rostam anaingia Kafumu, ambaye ni kitu kingine tofauti (japo kuna watakaodai kuwa naye ni fisadi pia).
Kwa Arumeru, pamoja na kuwa kiti kimekuwa wazi kwa mapenzi ya Mungu kufuatia kifo cha Mzee Jeremiah Sumari, lakini uzibaji wa pengo hilo ni mtihani mkubwa kwa CCM.
Mshindi wa kura za maoni ndani ya CCM ni Sioi Sumari, mtoto wa kiume wa Mzee Jeremiah Sumari. Kama ada, NEC ya CCM itakaa na kupitisha jina la mgombea wa CCM kama ilivyo taratibu za chama, na bila kutengua matokeo ya kura za maoni, basi mgombea wa CCM atakuwa ni Sumari.
Kwa angalizo la haraka haraka, hapa inaonekana kama siyo tatizo hata kidogo. Mzee Sumari kafariki, mtoto wake kashinda kura za maoni na kupitishwa na NEC kama mgombea halali. Hakuna shida, siyo? La hasha.
Tukiangalia kwa undani, kuna ugumu kuliko picha ya awali. Kijana Sioi Sumari, ni mkwe kwa kumuoa binti mkubwa wa Edward Lowassa. Kijana Sumari amekuwa karibu zaidi sana na wakwe zake akina Lowassa kiasi kwamba anafahamika na hata yeye kujitambulisha kama mmojawapo ya watu wachache sana ambao wana sikio la Lowassa, wakati wowote. Familia ya Lowassa imefungamana sana na familia ya Sumari, na huwezi kupenyesha hata upana wa nywele katika mfungamano huo.
Ni wazi na kwa mantiki ya kawaida kuwa Sumari alipata ushauri na pengine baraka pia za mke wake, binti Lowassa, na si ajabu pia hata wakwe zake ili aweze kugombea kiti hiki cha Arumeru. Kushinda au kushindwa itategemea pia na support anayopata kutoka kwa chama na ndugu, wakiwapo pia wakwe zake, Lowassa.
Sidhani kama CCM itafumbia macho ukweli huo, na kama ni hivyo je, CCM itasimama bega kwa bega na Sumari, Lowassa huko Arumeru? Je, ikifanya hivyo CCM itakuwa inatuma ujumbe gani kwa Lowassa na wana-CCM kuhusu suala la kuvuana gamba?
CCM inaonyesha kuelekeza nguvu zake Arumeru kwani Mwigulu Nchemba tayari katumwa kupeleka majeshi na takrima Arusha. Kwa hiyo uwezekano kuwa CCM itajitenga na Arumeru ni mdogo, ila CCM NEC bado inaweza kumuengua Sumari asiwe mgombea wa CCM. Hali hiyo ikitokea (binafsi sidhani kama itakuwa hivyo, na kauli za Tendwa ni uthibitisho kuwa Sumari anabebwa), je Lowassa atasimama kidete kutetea Arumeru kama alivyomsaidia Mzee Sumari mwaka 2010?
Arumeru ni kipimo kizuri kwa CCM kuhusu aidha kuachana na gamba, fisadi Lowassa na tawi lake Sumari au kuukumbatia u-CCM na magamba na ufisadi wake sasa na hata milele.