Arumeru Mashariki, CHADEMA kunyakua jimbo?

Democratic, kama unadhani huo ndio ukweli, umenoa!. Ila pia nimegundua ni wanabodi wachache sana huwa wanaukubali ukweli halisi!, wengi zaidi huogopa ukweli halisi na badala yake kung'ang'ania ukweli wa kujifariji nafsi zao kwa kujipa matumaini ya uwongo na mwisho wa siku huishia kulia lia tuu!.

Baada ya kupitishwa Sioi, uchaguzi Arumeru ndio umemalizika!. Kinachoendelea sasa ni kwa NEC kukamilisha tuu taratibu kukidhi matakwa ya kidemokrasia kusubiria kumtangaza rasmi!.

Wenye akili wataisoma hii post na kujinyamazia kusubiria April 2!. Ving'ang'anizi wa maubishi mtaanza kubisha na kuendelea kujifariji kuwa mtu yule yule toka chama kile kile aliyeshindwa na mahututi kitandani, sasa anaweza kushindana na mwana mfalme wa mtu yule yule aliyewashinda mwanzo na akashinda!.

Wengi wanategemea zaidi kura za chuki za wana CCM dhidi ya siasa za uchifu, usultani na ufalme za CCM kwa mtoto kumrithi baba yake bila kutambua asili ya Wameru ni ufalme wa koo fulani fulani!. Jerry alikuwa ni mfalme wao na Sioi ndiye mwana mfalume!.
Kwa wapenzi wa demokrasia ya kweli mtanisamehe sana kwa kuwadondolea ukweli mchungu!. Ili kuupata ukombozi wa kweli, lazima tukubali kukimeza "the bitter pill"- Sioi ndiye Mbunge Mteule wa Arumeru akisubiri kuapishwa!.

Pasco (wa jf).

pasco nlikuwa nakuheshim ila sasa nakufananisha na lyatonga,huna lolote.huitendei haki democracy
 
Mkapa huku atachemsha,si ndo anatuhumiwa kuwauzia mashamba ya wameru wawekezaji wa maua.
 
Wana jf,ni muda muafaka sasa kwa wananchi wote kupitia uchaguzi wa mbunge wa AM kuacha ushabiki wa kivyama na badala yake kuisaidia ccm kwa kutoa maamuzi ya kuwavua magamba wakada wenye tabia za kifisadi ambao kwao kila jambo ni kutumia fedha chafuchafu.HEBU TUCHANGIE HAPA
 
Ni mkutano wa kihistoria ambao ulitarajiwa kufanyika Geita kuanzia 3-5 Februari 2012 ukiwahusisha wabunge wote vijana wa CDM nchini.Kwa sasa utafanyika kuanzia 16-18 April 2012.

Hii imelenga kuwapa nafasi wabunge kushiriki kikamilifu katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge kule Arumeru Mashariki na udiwani katika kata 8 kama ilivyotangazwa na NEC.

Nawasilisha.
 
Wabunge Woote vijana wa CDM, hivi wanafika wangapi vile? Na Kila siku si wanakutana pale American chipsi kinondoni?
 
Wabunge Woote vijana wa CDM, hivi wanafika wangapi vile? Na Kila siku si wanakutana pale American chipsi kinondoni?

sasa kama unawaona hapo american chips kinondoni "kila siku" kwa nini usiwahesabu wapo wangapi!!
 
Wana jf,ni muda muafaka sasa kwa wananchi wote kupitia uchaguzi wa mbunge wa AM kuacha ushabiki wa kivyama na badala yake kuisaidia ccm kwa kutoa maamuzi ya kuwavua magamba wakada wenye tabia za kifisadi ambao kwao kila jambo ni kutumia fedha chafuchafu.HEBU TUCHANGIE HAPA

Mkuu hebu kuwa wazi kidogo! Au unamaanishi ccm ipigwe chini Arumeru ili kurahisisha magamba kuvuana magamba?
 
Wanajamvi:

Habari nilizopata kutoka Arumeru kwamba vijana wengi wa CCM huko wanaona hawaafiki hatua ya chama chao kumtumia fisadi ambaye wamempachika jina la ‘baba wa ufisadi' – yaani Benjamin Mkapa kufungua na kufunga mikutano ya kampeni.


Wanasema huyu anahusika sana na kuruhusu ufisadi wa EPA, Deep Green, Radar, kuuza nyumba za serikali na mengineyo, na wanadai bila shaka alifaidika na fisidi hizo dhidi ya wananchi wa Tanzania

Wanasema pia Mkapa alijimilikisha mgodi wa makaa yam awe wa Kiwira. Hivyo wanasema ni tusi kubwa kwa wakazi wa Arumeru na Watanzania kwa ujumla kumteua fisadi huyo kuwafungulia kampeni kwani wanaona ana husika sana katika kuifilisi nchi na hivyo kuwafanya vijana wan chi hii kukosa mwelekeo – kuwapo kwa elimu duni na kuzorota kwa huduma nyingine za serikali kwa raia.

Kuna wengine wanasema siku ya mkutano wa kampeni watakwenda na mabango kuwakumbusha wananchi wa Arumeru kuhusu uovu wa mtu huyu.
 
Mkuu hao vijana wapo wangapi? Wewe ndio wamekutuma uje uwasemee humu JF? kwa nini usipeleke malalamiko yao pale Lumumba.
 
Kama hizi habari ni za kweli, it's a patriotically correct and bold move by these vijana.
 
Hawana ubavu huo wa kumkataa, sera za chama chao ni kulindana, wangemkataa SIOI ambaye kachaguliwa kwa vishawishi vya rushwa. Ila Mkapa atakumbuka machungu yaliyompata sehemu fulani Machame mwaka 1995, uchaguzi wa vyama vingi wa kwanza alipopambana na Mrema, walizomewa pamoja na Dr. Omary Juma wakaishia kusema acheni kutuchagua kwanza huyo Mrema wenu hapati urais.
 
Ni vema wameru wakaliona hilo,na kama hao vijana kweli wako serious na tuhuma hizo,je wanafanya nini bado ccm.
Kwanini wasihamasishane kuhamia ccm na kumpigia kura Kamanda Nassary ili aongeze idadi ya wapiganaji wa kweli bungeni kwetu Dodoma,dhidsi ya hao kina ndiooo¤
 
Unafiki plus wanatoa wapi nguvu ya kupinga ufisadi wa Mkapa wakati mgombea wao ni zao la ufisadi na wamempitisha?kajipange tena
 
Back
Top Bottom