manuu
JF-Expert Member
- Apr 23, 2009
- 4,064
- 10,723
Wananchi wa Jimbo la Arumeru waishio pembezoni mwa eneo la Dolly (eneo ambalo wazungu wamemilikishwa)kuanzia jana jioni wameandamana kuelekea eneo hilo na kuanza kungoa fensi inayozunguka eneo hilo.Na hali ilizidi kuwa mbaya pale polisi wa kutuliza ghasia walipo fika eneo lile bila hata kuwauliza wananchi nini hoja yao wakaanza kuwarushia mabomu ya machozi wananchi waliokuwa kwenye eneo hilo na hapo ndipo na wananchi wakaanza kuwajibu kwa mawe maaskari wale hali iliyopelekea idadi ya maaskari kuongezeka na wananchi nao kuongezeka.
Na hoja au madai ya wananchi wa eneo lile kwanza kabisa wanataka barabara iliyokuwa ikitumika kuunganisha kijiji cha MAJI YA CHAI na Maroroni iliyofungwa baada ya hao wazungu kuchukua eneo hilo ifunguliwe kwani imekuwa ikiwalazima kuzunguka mbali sana baada ya barabara hiyo kufungwa.
2.Kulikuwa na shule ya msingi ndani ya eneo hilo wazungu walio milikishwa ambapo baada ya wazungu kuchukua eneo hilo na kulifensi shule iliamishwa na kupelekwa eneo ambalo ni mbali na makazi hivyo kuwasababishia usumbufu watoto.
3.Wanadai baada ya muafaka wa barabara na shule kupatikana watataka sasa wajue nini muafaka hiyo ardhi iliyomilikishwa kwa mzungu mmoja huku wananchi wa eneo husika wakiteseka kwa kukosa ardhi.
4.Wanasema huu ndiyo wakati muafaka wa wao kudai haki yao ya msingi na kufanya hivyo ni kumkumbusha Mheshiwa Nassary kuanza kufanyia kazi ahadi alizozitoa kwenye kampeni kubwa likiwa ni hili swala la ardhi kubwa kumilikiwa na watu wachache.Na wanamatumaini huu sasa ndio wakati wao wa kukomboa ardhi zao umefika.
Nipo maeneo ya hapa nitajitahidi niane kama naweza nikawaletea na picha ili mueze kuona huu umati wa wananchi ulivyumkubwa hapa.
Na hoja au madai ya wananchi wa eneo lile kwanza kabisa wanataka barabara iliyokuwa ikitumika kuunganisha kijiji cha MAJI YA CHAI na Maroroni iliyofungwa baada ya hao wazungu kuchukua eneo hilo ifunguliwe kwani imekuwa ikiwalazima kuzunguka mbali sana baada ya barabara hiyo kufungwa.
2.Kulikuwa na shule ya msingi ndani ya eneo hilo wazungu walio milikishwa ambapo baada ya wazungu kuchukua eneo hilo na kulifensi shule iliamishwa na kupelekwa eneo ambalo ni mbali na makazi hivyo kuwasababishia usumbufu watoto.
3.Wanadai baada ya muafaka wa barabara na shule kupatikana watataka sasa wajue nini muafaka hiyo ardhi iliyomilikishwa kwa mzungu mmoja huku wananchi wa eneo husika wakiteseka kwa kukosa ardhi.
4.Wanasema huu ndiyo wakati muafaka wa wao kudai haki yao ya msingi na kufanya hivyo ni kumkumbusha Mheshiwa Nassary kuanza kufanyia kazi ahadi alizozitoa kwenye kampeni kubwa likiwa ni hili swala la ardhi kubwa kumilikiwa na watu wachache.Na wanamatumaini huu sasa ndio wakati wao wa kukomboa ardhi zao umefika.
Nipo maeneo ya hapa nitajitahidi niane kama naweza nikawaletea na picha ili mueze kuona huu umati wa wananchi ulivyumkubwa hapa.