Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Usajili Updates: Arsenal waingia Leicester City wanamtaka Jamie Vardy.

2717.jpg


Klabu ya Arsenal leo wameingia Leicester na kuweka mezani pauni milioni 20 kutaka kumsajili Jamie Vardy.

Arsenal wamevunja sera yake ya kusajili wachezaji ambao wana umri zaidi ya miaka 29 na wamemtambua Jamie Vardy kama mshambuliaji ambae wanataka kumsajili akiwa na uzoefu wa kufunga magoli kwa timu yake ya Leicester ambayo ni mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza.

Arsene Wenger jana alikuwepo kumuangalia Jamie Vardy uwanjani Wembley wakati akichezea timu ya taifa ya Uingereza ambayo ilikuwa ikichuana na timu ya taifa ta Portugal.

34DCA4ED00000578-3623387-image-a-19_1464941769751.jpg

Arsene Wenger akiangalia mechi ya kujipima nguvu kati ya Uingereza na Portugal iliyofanyika jana kwenye uwanja wa Wembely. Pembeni yake ni David Dein ambae ni makamu mwenyekiti wa zamani wa Arsenal na ndie aliemleta Wenger kwenye klabu ya Arsena: Picha ni kutoka Reuters

Kama mipango ikienda sawa Jamie Vardy atazungumza na Arsenal ambao wanafahamu kwamba Vardy analipwa pauni 80,000 kwa wiki na Arsenal wapo tayari kuongeza pesa hiyo.

Ikiwa Vardy atakubaliana na Arsenal, basi atafanyiwa "Medical" na kukamilisha taratibu zote kabla ya kuondoka na timu ya Uingereza kwenda France.

Hata hivyo Arsene Wenger anataka mambo yafanyike kwa haraka na wepesi kutokana na ugumu uliowekwa na meneja wa Uingereza Roy Hodgson ambae amepiga marufuku majadiliano ya usajili wakati wa Euro 2016

Habari zaidi kufuatia.
 
Strikers wepi ambao wako proven wanapatikana kirahis? can you mention one or two?

usitutajie danny sturidge please
Laccazette, Icardi, Bacca, Chicharito, Nolito etc

I'd choose them over Vardy.

And am not denying kuwa Vardy ni good ST..
 
Back
Top Bottom