Yo Yo
JF-Expert Member
- May 31, 2008
- 11,217
- 1,702
- Thread starter
- #21
Na Maimuna Kubegeya(Mwananchi.co.tz)
UONGOZI wa shule ya msingi Philadephia iliyopo mkoani Pwani, umedaiwa kuwalazimisha wafanyakazi wake kupima ukimwi na kupeleka matokeo ya vipimo hivyo kwake.
Habari hizo, zimethibitishwa na baadhi ya wafanyakazi hao zimesema kuwa uamuzi huo umetokana na agizo maalum lililotolewa serikalini.
Wafanyakazi hao kwa nyakati tofauti walisema mkuu wa shule hiyo, alitoa agizo kwa wafanyakazi wote kupima ukimwi huku akidai ni agizo serikali.
Walisema kuwa wao walikubali kutekeleza agizo hilo ili kulinda ajira zao.
?Si hivyo tu mkuu wa shule yetu alisema kuwa ni lazima tupime ukimwi kwani ni agizo ambalo limetoka serikalini,? alisema mmoja wao kwa masharti ya kutotajwa jina.
Walisema kinachowasikitisha, upimaji huo uliendeshwa kibaguzi na kwamba baadhi ya wafanyakazi raia wa Uganda hawakuhusishwa kabisa katika mpango huo.
Walisema licha ya kukubali kupima, wenzao
wamepinga kupimwa na wamesusia kwenda kupima.
Shule hiyo, ipo Mkuranga chini ya ?Tanzania Presbyterian Church? na inamilikiwa na raia wa Korea, chini ya uongozi wa mwalimu mkuu ambaye ni raia wa Uganda.
Mwananchi Jumapili ilishuhudia baadhi ya wafanyakazi hao wakiwa katika foleni ya kwenda kupima katika chumba cha Zahanati ya Zakheem Mbagala jijini Dar es Salaam wiki iliyopita.
Mmoja wa wafanyakazi katika shule hiyo, alisema kupima ukimwi ni agizo la serikali.
?Unajua mama kwa Mtanzania wa kawaida suala la kupima ukimwi ni gumu sana lakini linapokuja suala la ajira, aaah ndio hivyo tena hakuna jinsi,? alisema mfanyakazi huyo.
Hata hivyo, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Chiza, alithibitisha kufanyika kwa mpango wa kupima ukimwi.
Mwalimu huyo alisema kupima ukimwi ni agizo la Wilaya ya Mkuranga na alikiri kuwepo ubaguzi katika kupima ukimwi.
?Tuliamua kuendesha zoezi hilo kwa Watanzania na kuwaacha Waganda kwa kuwa zoezi la kupima linawahusu Watanzania tu na sio watu wa mataifa mengine,? alisema mwalimu huyo.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, Henry Orauya Clemens alisema sera za serikali zipo wazi kwamba hakuna mtu anayelazimishwa kupima ukimwi.
?Nikiwa kiongozi wa serikali nina hakika na haiwezekani serikali kuagiza wananchi wake kupima ukimwi kwa lazima,? alisisitiza Clemens.
Clemens alisema mikataba ya ajira ni nyenzo muhimu katika kulinda masilahi ya mwajiri na mwajiriwa hivyo wafanyakazi hao pia walitakiwa kuipitia mikataba hiyo ili kutokwenda kinyume na haki zao.
Pia Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Abdalah Kihato alikanusha kutoa agizo la kuwalazimisha wafanyakazi hao kupima ukimwi.
?Serikali inaendesha kampeni ya kuhamasisha na sio kulazimisha wananchi wake kupima ukimwi. Sifahamu kabisa na wala sijatoa agizo hilo,? alisema Kihato.
Hii ni kinyume na haki za binadamu......enhe wakishajua wanafukzua kazi au?
UONGOZI wa shule ya msingi Philadephia iliyopo mkoani Pwani, umedaiwa kuwalazimisha wafanyakazi wake kupima ukimwi na kupeleka matokeo ya vipimo hivyo kwake.
Habari hizo, zimethibitishwa na baadhi ya wafanyakazi hao zimesema kuwa uamuzi huo umetokana na agizo maalum lililotolewa serikalini.
Wafanyakazi hao kwa nyakati tofauti walisema mkuu wa shule hiyo, alitoa agizo kwa wafanyakazi wote kupima ukimwi huku akidai ni agizo serikali.
Walisema kuwa wao walikubali kutekeleza agizo hilo ili kulinda ajira zao.
?Si hivyo tu mkuu wa shule yetu alisema kuwa ni lazima tupime ukimwi kwani ni agizo ambalo limetoka serikalini,? alisema mmoja wao kwa masharti ya kutotajwa jina.
Walisema kinachowasikitisha, upimaji huo uliendeshwa kibaguzi na kwamba baadhi ya wafanyakazi raia wa Uganda hawakuhusishwa kabisa katika mpango huo.
Walisema licha ya kukubali kupima, wenzao
wamepinga kupimwa na wamesusia kwenda kupima.
Shule hiyo, ipo Mkuranga chini ya ?Tanzania Presbyterian Church? na inamilikiwa na raia wa Korea, chini ya uongozi wa mwalimu mkuu ambaye ni raia wa Uganda.
Mwananchi Jumapili ilishuhudia baadhi ya wafanyakazi hao wakiwa katika foleni ya kwenda kupima katika chumba cha Zahanati ya Zakheem Mbagala jijini Dar es Salaam wiki iliyopita.
Mmoja wa wafanyakazi katika shule hiyo, alisema kupima ukimwi ni agizo la serikali.
?Unajua mama kwa Mtanzania wa kawaida suala la kupima ukimwi ni gumu sana lakini linapokuja suala la ajira, aaah ndio hivyo tena hakuna jinsi,? alisema mfanyakazi huyo.
Hata hivyo, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Chiza, alithibitisha kufanyika kwa mpango wa kupima ukimwi.
Mwalimu huyo alisema kupima ukimwi ni agizo la Wilaya ya Mkuranga na alikiri kuwepo ubaguzi katika kupima ukimwi.
?Tuliamua kuendesha zoezi hilo kwa Watanzania na kuwaacha Waganda kwa kuwa zoezi la kupima linawahusu Watanzania tu na sio watu wa mataifa mengine,? alisema mwalimu huyo.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, Henry Orauya Clemens alisema sera za serikali zipo wazi kwamba hakuna mtu anayelazimishwa kupima ukimwi.
?Nikiwa kiongozi wa serikali nina hakika na haiwezekani serikali kuagiza wananchi wake kupima ukimwi kwa lazima,? alisisitiza Clemens.
Clemens alisema mikataba ya ajira ni nyenzo muhimu katika kulinda masilahi ya mwajiri na mwajiriwa hivyo wafanyakazi hao pia walitakiwa kuipitia mikataba hiyo ili kutokwenda kinyume na haki zao.
Pia Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Abdalah Kihato alikanusha kutoa agizo la kuwalazimisha wafanyakazi hao kupima ukimwi.
?Serikali inaendesha kampeni ya kuhamasisha na sio kulazimisha wananchi wake kupima ukimwi. Sifahamu kabisa na wala sijatoa agizo hilo,? alisema Kihato.
Hii ni kinyume na haki za binadamu......enhe wakishajua wanafukzua kazi au?