Are you In? Oktoba 5, 2012.... SIKU YA KUWASOMEA WATOTO VITABU

unajua ndio maana nataka tuanze hivi vitu sisi wenyewe; kuangalia taasisi na serikali imeshindikana. Kwa miaka 6 iliyopita ulimuona wapi Kikwete akikaa kumsomea mtoto kitabu? au Mbunge mwingine yeyote? Lakini kukosekana kwa vitabu vya Kiswahili siyo sababu ya wazazi kutokusoma na watoto wao. Na siyo lazima usomee watoto wako peke yako. Kwenye hili zoezi tunachofanya ni kufanya sisi wenyewe.

Tayari kuna watu wameshawasiliana na shule ili waende wakasomee watoto; kuna mtu tayari kapata watoto 12 wa jirani kuwasomea jioni ile

Kuna sehemu nilimsoma Prof. Mbele akisema kuwa japokuwa hili ni jambo zuri lakini lina utata pia. Alieleza matatizo ya kimazingira kwa watoto hasa wa vijijini kuweza kujisomea vitabu ambapo upatikanaji wake ni wa shida. Hata kwa maeneo ya mijini inaweza kuwa shida kimazingira pia ukiondoa familia ambazo zina wazazi wenye uwezo na mwamko. Wapo watoto wenye moyo wa kupenda kusoma lakini hawapati changamoto.

Lakini kama alivyosema cha muhimu ni vitendo hasa kutoka kwa watoto, wazazi wa leo na wazazi watarajiwa wa kizaji kijacho. Kinachohitajika ni kujaribu kujitengenezea tena utamaduni wa kusoma vitabu, japokuwa inaweza kuwa ngumu katika ulimwengu wa sasa ambao umetawaliwa na teknologia mpya. Wapo watu watalalamikia sana ukosefu wa umeme lakini wapo waliosoma vitabu kwa kutumia koroboi na kufanya vizuri tuu.

Labda kwa kupiga hatua moja mbele zaidi ingekuwaje kama waliobahatika kufika angalao chuo kikuu wangeji-organise na kuanzisha kijimaktaba kadogo kwenye vijiji wanavyotoka au kwenye shule zao za msingi walizosomea hata kama ni kabati moja tu? Nina imani kuwa watoto wataingia humo kusoma. Nimekuwa nikifikiria hili suala kwa kina sana lakini wapo wengine pia wanaosema kuwa miaka ijayo maktaba zitakuwa "digitalised". Hata hivyo, kwa mazingira yetu naona bado tuko mbali sana, japokuwa "digitisation" inaweza kusabisha kuwepo kwa uhaba wa vitabu ambavyo ni "hard copies".

Nafikiri badala ya kuongelea sijui matatizo ya umeme, serikali mbovu, ukosefu wa vitabu vya kusoma, mawasiliano, n.k. sisi wenyewe ambao tumefanikiwa kwenda shule na kufika hapa tulipo tujaribu kufanya mikakati wa kuanzisha kijimaktaba kadogo kwenye vijiji vyetu halafu tuangalie matokeo. Nimeshaona baadhi ya watu waki-fundraise kujenga darasa kwenye shule za vijiji wanavyotoka. Hata hivyo, nimekuwa nikijiuliza which comes first. Darasa la kusomea au kitabu cha kusoma?
 
Nafikiri badala ya kuongelea sijui matatizo ya umeme, serikali mbovu, ukosefu wa vitabu vya kusoma, mawasiliano, n.k. sisi wenyewe ambao tumefanikiwa kwenda shule na kufika hapa tulipo tujaribu kufanya mikakati wa kuanzisha kijimaktaba kadogo kwenye vijiji vyetu halafu tuangalie matokeo. Nimeshaona baadhi ya watu waki-fundraise kujenga darasa kwenye shule za vijiji wanavyotoka. Hata hivyo, nimekuwa nikijiuliza which comes first. Darasa la kusomea au kitabu cha kusoma?

mzee wenzio tumeshaanza; nimetambua - baada ya muda mrefu wa kuzama katika siasa za Tanzania - hatuwezi kutegemea wanasiasa kutuletea mabadiliko na hata kutuongoza kulleta mabadiliko. Maana kama ingekuwa inawezekana kwa kweli tungekuwa mbali sana. Hivyo, sisi baadhi yetu ambao tunatambua hili tumeamua kuanza kuunganisha nguvu zetu mmoja mmoja na kuanza kuleta mabadiliko tunayoyataka.
 
...Wengine wakikurupuka alfajiri hawarudi majumbani mwao mpaka usiku wa manane watoto wameshalala na hii ndivyo ilivyo kila siku iendayo kwa Mungu. Hawana hata muda wa kukaa na watoto kuongea nao, kuangalia shule wamefanya nini, kuwasaidia homework zao, kukaa nao mezani kula pamoja nao hata mlo wa jioni. Matokeo yake watoto wanakuwa hawana table manners. Kula na wanae mpaka sikukuu tena kama hana mning'inio alioamka nao baada ya kuutwika jana yake, vinginevyo ikifika saa ya kifungua kinywa au chakula cha mchana utamsikia, "nyie endeleeni tu mie sijisikii kula."

Wengine wana watoto hata hawajui wako wapi na mamazao saivi.
Kaazi kweli kweli,inaniuma kuandika hivi maana............
 
Kama Nyerere alivyosema mwaka 1967:

"...books are a very important way to knowledge and to self-improvement; from them we can learn new ideas; new techniques of working and new methods. We can learn about the development of men in all its different aspects; we can broaden our understanding of other peoples and even of ourselves. All the experiences of mankind, all his discoveries and his inventions can be learned about through reading...."

Utamaduni wa kujisomea unajengeka vizuri kuanzia utotoni. Agosti mwaka juzi Google walisema kuna vitabu 129,864,880. I am sure vitakuwepo zaidi ya hivyo. Labda suala linakuja ni vitabu vipi kwa kusoma hasa kwa watoto wa Kitanzania? Kipi cha kusoma ni kipi cha kuacha?
 
Kama Nyerere alivyosema mwaka 1967:

"...books are a very important way to knowledge and to self-improvement; from them we can learn new ideas; new techniques of working and new methods. We can learn about the development of men in all its different aspects; we can broaden our understanding of other peoples and even of ourselves. All the experiences of mankind, all his discoveries and his inventions can be learned about through reading...."

Utamaduni wa kujisomea unajengeka vizuri kuanzia utotoni. Agosti mwaka juzi Google walisema kuna vitabu 129,864,880. I am sure vitakuwepo zaidi ya hivyo. Labda suala linakuja ni vitabu vipi kwa kusoma hasa kwa watoto wa Kitanzania? Kipi cha kusoma ni kipi cha kuacha?
Moyo umestuka paaaaaa! EMT is back???
Kongosho umemuona mtoro karudi???
 
Last edited by a moderator:
Noted ..vitabu vya Tusome kwa Bidii siku hizi havipo?
Watoto utakuta wamebebana na vijitabu vya udaku abavyo ndo vimejaa mtaani
 
IMGA0689.JPG

Baadhi ya vitabu nitakavyosomea watoto.................nimeamua kuanza na watoto wadogo kabisa, lugha isiwe barrier ya kusoma vitabu. Vitabu husaidia katika ujuzi wa lugha.
 
mzee wenzio tumeshaanza; nimetambua - baada ya muda mrefu wa kuzama katika siasa za Tanzania - hatuwezi kutegemea wanasiasa kutuletea mabadiliko na hata kutuongoza kulleta mabadiliko. Maana kama ingekuwa inawezekana kwa kweli tungekuwa mbali sana. Hivyo, sisi baadhi yetu ambao tunatambua hili tumeamua kuanza kuunganisha nguvu zetu mmoja mmoja na kuanza kuleta mabadiliko tunayoyataka.

Umeona eehhhh???
Hope na wenzako wameliona hilo.
Vichwa vipo vya utaalamu, kuongoza, kushawishi na kusukumu mambo yakaenda mbele.
Achaneni na maneno matupu ya kwenye siasa.Elekezeni nguvu zenu pale mtakapoleta tofauti chanya kwenye jamii.

Wengine wengi walishaliona hili zamaniiii wakajikita kwenye shughuli ziletazo tija badala ya kukalia politiki!
Kuna mgahawa pale Regent Estate wa mama Chachage ulianza kama miaka 3-4 iliyopita.Huo mgahawa "Book cafe" azma yake ni kujenga tabia ya watu kujisomea vitabu badala ya kuzurura na kupiga porojo zisizo na tija. Wako watu wengine wanazo "clubs" zao wenyewe za kusoma na kubadilishana vitabu. Aidha kuna wazazi mmoja mmoja wana kawaida ya kuwasomea watoto wao vitabu kila usiku.Wapo pia wenyewe kuwasomea watoto walio tumboni (mimba) ,alimradi zipo jitihada mbalimbali zinaendelea kimya kimya.
Umefanya la maana Mzee Mwanakijiji kusema kwa sauti ili wale ambao bado hawajafanya wafanye.
 
Na katika bidii hiyo, tusisahau kusomea watoto vitabu ambavyo picha zake au maudhui yatamsaidia kujikubali na kujipenda yeye alivyo

Vitabu vya Kizungu vinavyosifia uzuri wa Wazungu, vinaweza kupelekea watoto kutojipenda walivyo na kuishia kwenye mikorogo, weaves, wigs, colored contacts na huko tunakolekea hata kutengeneza baadhi ya viungo vya mwili

Mfano wa vitabu vinavyomsifu Caitlin kuwa ni mzuri kwa sababu ana blue eyes, long straight brown hair, and the fairest of skin huku anaesomewa akiwa hajawahi kusifiwa kwa jinsi alivyo vinaweza kuzaa matunda hasi.
 
Tumeanza movement ya kujiletea mabadiliko...

So... Ijumaa tumeamua (wale ambao tumekubaliana) kuwa itakuwa siku ya kuwasomea watoto wetu; kama shuleni hawasomi vya kutosha we will do it at home...
hiyo ni nzuri sana na inasaidia kujua mwanao kama anajua kusoma vizuri au la. mtoto wangu wa 2 sasa yupo darasa la 2, lakini toka akiwa la kwanza shuleni kwao walikuwa wanapewa vitabu vya hadithi (vya kiingereza) na wanaandikia wazazi kwenye diary zao tuwasaidie kusoma. mimi nilikuwa namsikiliza mwanangu anavyosoma, maneno ambayo hayawezi namsaidia, ilimsaidia sana kujua kusoma kwa ufasaha. baadae nikaanza kumnunulia vya kiswahili (kuna bookshop pale upanga, nimesahau kidogo jina) wana vitabu vingi sana vya hadithi na masomo. mpaka sasa tuna huo utaratibu wa kusomeana vitabu siku za weekend maana siku zingine wanakuwa busy na homework na sisi busy na kazi, imekuwa kama mchezo fulani wa familia....... inapendeza sana
 
mimi naona vitabu vyetu vya siku hizi hazina mvuto kama kipindi cha nyuma ukiangali vitabu tulivyotumia kwenye kiingereza na kiswahili zilikuwa na mvuto kuliko leo hii. mitaaala nayo ni sababu ya kuharibu au kuwafanya watu wasipende kusoma vitabu na watunzi wetu siku hizi ni njaa zinawasumbua havina madhari ya kuvutia wasomaji
 
Na katika bidii hiyo, tusisahau kusomea watoto vitabu ambavyo picha zake au maudhui yatamsaidia kujikubali na kujipenda yeye alivyo

Vitabu vya Kizungu vinavyosifia uzuri wa Wazungu, vinaweza kupelekea watoto kutojipenda walivyo na kuishia kwenye mikorogo, weaves, wigs, colored contacts na huko tunakolekea hata kutengeneza baadhi ya viungo vya mwili

Mfano wa vitabu vinavyomsifu Caitlin kuwa ni mzuri kwa sababu ana blue eyes, long straight brown hair, and the fairest of skin huku anaesomewa akiwa hajawahi kusifiwa kwa jinsi alivyo vinaweza kuzaa matunda hasi.

mwalimu, tatizo ni wapi pa kupata hivyo vitabu? Mwanakijiji aliandika kitabu cha kiswahili hapa, sijui hata kama kimeuzika manake aliweka post ya kukitangaza akarushiwa mawe. Watanzania wachache sana wanaandika vitabu kwa sababu ya gharama za uchapaji na usambazaji kuwa juu, lakini pia kwa sababu walengwa hawako tayari kununua kwa bei ya sokoni.
 
View attachment 66845

Baadhi ya vitabu nitakavyosomea watoto.................nimeamua kuanza na watoto wadogo kabisa, lugha isiwe barrier ya kusoma vitabu. Vitabu husaidia katika ujuzi wa lugha.

Kweli lugha isiwe kizuizi cha kusoma vitabu lakini kama alivyosema Gaijin vipi maudhui ya vitabu? Nafikiri hilo ndilo tatizo kubwa linalotukabili. Ingawa kwa sababu ya utandawazi, lugha huathiriana duniani kote, wapo watakaosema kuwa lugha za kigeni katika mfumo wa elimu hunuia kuendeleza maadili na utamaduni wa kigeni ambao mengi hayaambatani wala kulingana na matarajio na mahitaji ya kimaendeleo ya utamaduni wetu.

Sijui kama imefika Tanzania, lakini huko Kenya imedaiwa kuwa wanaoteua vitabu vya kutumika mashuleni huchagua majina ya waandishi na wala sio yaliyomo kwenye vitabu hivyo hata kama maudhui yaliyomo katika vitabu hivyo yamepitwa na wakati. Pia kutokana na biashara huria wapo wanaozisha biashara ya kuagiza vitabu vya watoto nje ya nchi na kuongea na wanaoteua vitabu vya kutumika mashuleni ili wapate "dili" la kusambaza hivyo vitabu.

Hivi ile change ya radar ilikuwa kwa ajili ya kuchapisha vitabu vya aina gani?
 
J Mzee, nimtoto mdogo au hata hawa wenye ndevu??

Neno "mtoto" linaweza kumaanisha "kuanzia mtu wa umri wa kwenda shule ya chekechea hadi kufikia anapohitimu elimu ya shule ya msingi, yaani darasa la saba. Kwa tarakimu kipindi hiki katika maisha ya mwanadamu, hususan Tanzania, ni kati ya miaka 3 hadi 15.

Hiki ni kipindi muhimu sana katika maisha ya mwanadamu, kwani ni kipindi ambapo binadamu hujenga msingi wa utu wake katika mazingira ya kisaikolojia, kijamii na kilimwengu. Jamii inaposhindwa kujenga msingi huu, mtoto hungia katika uga wa kiutu-uzima ama kwa mashaka, ama kwa namna isiyoendana vema na mazingira yake.

"Baada ya kujua mtoto ni nani basi vitabu vya watoto ni maandiko ambayo yanakidhi watoto hao. Kwa maneno mangine, vitabu hivyo ni vile vinavyoendana na watoto wa umri wa baina ya miaka 3-15."

Chanzo: Madumulla, J.S. "Hali ya Vitabu vya Watoto Katika Tanzania" (2001) 68 APP - Swahili Forum VIII 171-183, 171
 
Hivi naweza kukusanya watoto wa kitaa nikawasomea eeh?
Ngoja niangalie jinsi ya kuandaa somo

Hata kama sijajiandaa kununua vitabu vingi, si naweza print mtandaoni na kwenda kuwakusanya watoto wa mtaani kama 20, nawagawia nakala, tunasoma pamoja? Baada ya kusoma juisi za vijoti box 1 na pocorn za namanga tosha kabisa.

Tena hii ni assigment yangu wiki hii

kumbe ni majumbani? Na tusio na watoto majumbani je? I planned kuenda hospitali, ward ya watoto na kusoma nao. . . .
 
Inasikitisha unajua. Mimi nataka zile adithi za mama na mwana...hivyo vingereza wache wajifunze mashuleni..lakini ikija kwenye story napenda za kitanzania au niseme za kiafrika au basi za kidini zaidi. Nataka adithi zenye mafunzo yanayoendana na culture zetu.

Kuna nchi kama Japan ukipanda treni kila mtu ana comic book...nasikia kuna za age group tofauti..watoto vijana na wazee. Inasaidia kweli watoto kupenda kusoma. Huku mtoto unakuta ameshika KIU, afanyeje sasa na hakuna vya age yao.
nyumba kubwa umenikumbusha hadithi za mama na mwana nilikuwa nikisikia chei chei shangazi daaah raha
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom