Are you In? Oktoba 5, 2012.... SIKU YA KUWASOMEA WATOTO VITABU

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
375946_10151182119796156_75347272_n.jpg


MIKOA AMBAPO WATU WATASHIRIKI IJUMAA HII KUWASOMEA WATOTO:

Mwanza (Mjini)
Morogoro
Dar
Arusha
...
 
Tunapoteza mno muda na watoto na TV, mpira, hakunaga, n.k.. can't we set time for reading.. au na sisi wazazi hatujui kusoma au hatupendi kusoma? So far.. kuna mtu kanifurahisha leo anasema yeye tayari anakusanya watoto 12 mtaani kwao that day na kuwasomeaaa..
 
Jana nilicheki muvi ya Eddie Murphy - A thousand words! jamaa alikua akiona choo cha mtoto wake anaona kinyaa sana na kuna siku akaambiwa amuimbie mtoto wake shuleni (kindergaten).. hahaha kweli jamaa comedian.
:focus: Mzee, nimtoto mdogo au hata hawa wenye ndevu??
 
Hakuna kitu chenye faida ya kudumu kwa mtoto kama kumsomea mara kwa mara....


true, na kama hatutawajengea tabia hii mapema basi watapata tabu kujisomea ukubwani. Mtu mwenye desturi/ walau hobbie ya kusoma huwa na maarifa sana na anaweza akapambanua mambo mengi kwa undani. Wazazi -tuwajengee watoto wetu tabia ya kusoma. Wazoeshe walau kuwasomea paragraph moja ya hadithi zenye mafunzo. TV na video hazimsaidii mtoto chochote zaidi ya kumpreempty ubongo wake. My teacher alwayz told me-when you watch TV, you are actually watching other people making money (in talk shows, soaps ect) but when you read you slowy learn how to discern on how to make your life better!
 
Vitabu vyenyewe viko wapi...labda mtupe link.

Maana mi nilisoma sana vitabu (siyo kusomewa) nikiwa mdogo; lakini leo hii vinapatikana wapi...sijuhi.

Kitabu cha Abunuasi hivi kinauzwa wapi?

Kulikuwa na vitabu vya adithi za Biblia my dad alikuwa anatununulia...hizi adithi sijuhi za Yusufu na nduguze mi nilisoma kama novel. herufi kubwa na picha juu;


Maana si kusoma vitabu vya kidhungu...kutakuwa hakuna tofauti na kutazama katuni. Lol.
 
Vitabu vyenyewe viko wapi...labda mtupe link.

Maana mi nilisoma sana vitabu (siyo kusomewa) nikiwa mdogo; lakini leo hii vinapatikana wapi...sijuhi.

Kitabu cha Abunuasi hivi kinauzwa wapi?

Kulikuwa na vitabu vya adithi za Biblia my dad alikuwa anatununulia...hizi adithi sijuhi za Yusufu na nduguze mi nilisoma kama novel. herufi kubwa na picha juu;


Maana si kusoma vitabu vya kidhungu...kutakuwa hakuna tofauti na kutazama katuni. Lol.

TZ hata maduka ya vitabu hakuna kwa kweli
 
Nyumba Kubwa na The Boss.. mwamko ambao tumeauanzisha unataka kubadilisha hilo; u c tayari mmesema kitu ambacho nataka wengi wakioneshe kuwa kuna hitaji (demand) ya vitabu vya aina hiyo. Vitabu vipo na vinapatikana wapi? Ni matangazo mangapi kwenye radio na luninga yanatangaza vitabu vya watoto?
 
Mzee Mwanakijiji mimi nadhani umeniacha, naona kicwa cha habari tu na michango ya watu, sasa nahisi tu kuna kusomea watoto vitabu, kivipi! sijui

Tumeanza movement ya kujiletea mabadiliko...

So... Ijumaa tumeamua (wale ambao tumekubaliana) kuwa itakuwa siku ya kuwasomea watoto wetu; kama shuleni hawasomi vya kutosha we will do it at home...
 
Inasikitisha unajua. Mimi nataka zile adithi za mama na mwana...hivyo vingereza wache wajifunze mashuleni..lakini ikija kwenye story napenda za kitanzania au niseme za kiafrika au basi za kidini zaidi. Nataka adithi zenye mafunzo yanayoendana na culture zetu.

Kuna nchi kama Japan ukipanda treni kila mtu ana comic book...nasikia kuna za age group tofauti..watoto vijana na wazee. Inasaidia kweli watoto kupenda kusoma. Huku mtoto unakuta ameshika KIU, afanyeje sasa na hakuna vya age yao.
 
"Alinijia na kupanda kwenye mapaja yangu akiburuta kitabu chake kilichochakaa chenye kurasa zilizopakwa . . . siagi ya karanga, na kunisihi . . . , ' Baba, nisaidie kukisoma; nisaidie kukisoma.'"-Dakt. Clifford Schimmels, profesa wa elimu.

Sijui kama bado yanafanyika ila mwanzoni mwa miaka ya 2000 kulikuwa na maonyesho ya vitabu. Watoto walikuwa wakihudhuria ambapo walikuwa wakifanya michezo ya kuigiza na kuimba nyimbo kuhusu umuhimu wa kusoma vitabu wakiwahamasisha wazazi kuweka vitabu nyumbani na kuwa na utaratibu wa kusoma pamoja na watoto. Lakini, ujumbe wao uliishia hewani, kwani wazazi wenyewe hawakuwepo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi wa Vitabu Tanzania (TBST), Kajia Mjema kasema juzi kuwa hata wazazi wamekuwa wakiwapelekea magazeti watoto wao pindi warudi nyumbani badala ya vitabu na wakati mwingine magazeti siyo yale yanayoandika habari uyakinifu bali ni magazeti pendwa kama vile ya udaku. "Unajua hata sisi wazazi tunachangia kudumaza maarifa ya mtoto, unakuta baba au mama anaporudi nyumbani, anarudi na magazeti pendwa sasa unafikiri huyu mtoto tunamjenga?"anahoji Mjema.

Katika jarida la Tanzania Schools Collection, toleo la kwanza, Moris Mwavizo anaripoti, ukurasa wa 12, kuwa katika maonesho fulani ya vitabu Dar es Salaam, mratibu mmoja alimwona mtoto akizunguka mwenyewe katika viwanja. Alipomwuliza kwa nini baba yake hakuja naye, mtoto alijibu kuwa baba yake angekuja kama kungekuwa na bia hapa kwenye maonesho. Je, hii si aibu?
 
Inasikitisha unajua. Mimi nataka zile adithi za mama na mwana...hivyo vingereza wache wajifunze mashuleni..lakini ikija kwenye story napenda za kitanzania au niseme za kiafrika au basi za kidini zaidi. Nataka adithi zenye mafunzo yanayoendana na culture zetu.

Kuna nchi kama Japan ukipanda treni kila mtu ana comic book...nasikia kuna za age group tofauti..watoto vijana na wazee. Inasaidia kweli watoto kupenda kusoma. Huku mtoto unakuta ameshika KIU, afanyeje sasa na hakuna vya age yao.


unajua ndio maana nataka tuanze hivi vitu sisi wenyewe; kuangalia taasisi na serikali imeshindikana. Kwa miaka 6 iliyopita ulimuona wapi Kikwete akikaa kumsomea mtoto kitabu? au Mbunge mwingine yeyote? Lakini kukosekana kwa vitabu vya Kiswahili siyo sababu ya wazazi kutokusoma na watoto wao. Na siyo lazima usomee watoto wako peke yako. Kwenye hili zoezi tunachofanya ni kufanya sisi wenyewe.

Tayari kuna watu wameshawasiliana na shule ili waende wakasomee watoto; kuna mtu tayari kapata watoto 12 wa jirani kuwasomea jioni ile
 
Mama wa Ben Carson japo hakuwa anajua kusoma, alihimiza watoto wasome vitabu na kutoa ripoti. Leo hii jamaa anatisha. Google habari zake-ana honorary doctorates za medicine 65! Asante Mzee Mwanakijiji.
 
Back
Top Bottom