Are Our Inflation Numbers Fabricated?

Hi suala ambalo tayari limeshajadiliwa mara kadhaa hapa na hata huko mtaani hakuna mtu mwenye habari na hizi takwimu zisizoakisi hali halisi. Bei za chakula zimepanda ila upandaji unatofautiana tatizo sasa linakuja katika kapu la NBS la chakula ambalo halitoi uzito kwa bidhaa nyingi ambazo wananchi wa mijini wanatumia kwa wingi. Pia uzito wa chakula umeshashushwa toka kwenye asilimia zaidi ya 50 mpaka kwenye kama 44 hivi. Kuna mabandiko yangu ya siku za nyuma ambayo niliongelea suala la hili kwa undani kidogo.

Ukweli ni kwamba kwa nchi yetu mtu unahitaji takwimu za mfumuko wa bei za zaidi ya nchi moja kwa ujumla, wangejitahidi watoe takwimu kwa Dar, Halmashauri zingine za mijini kwa ujumla na kwa ajili ya Vijijini.

Katika ambatanisho lako, lile ongezeko la asilimia 93 toka mwaka 2001 lililobainishwa na HBS linatoa akisi nzuri zaidi ya gharama za maisha kushinda mapishi ya serikali ya asilimia 43.

Lakini mwisho wa siku mfumuko wa bei ni relative. Ni relative kwa kipato chako. Kwa kila mimi na wewe tunaopiga kelele kwamba mambo magumu kuna wengine wengi ambao mambo ni mazuri
 
Back
Top Bottom