X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Daktari mtaalamu wa kutoa mimba za miezi zaidi ya mitano wa nchini Marekani ameuliwa kwa kupigwa risasi akiwa kanisani.
Dokta George Tiller, 67, aliuliwa kwa kupigwa risasi moja asubuhi ya jumapili katika kanisa la kilutheri la mjini Wichita, Kansas.
Dokta Tiller alikuwa mtaalamu wa kutoa mimba za miezi mingi ambazo kwa kawaida kichanga kilichopo tumboni huwa kina uwezo wa kuendelea kukua hata kikiwa nje ya tumbo la uzazi kwa msaada wa mashine.
Polisi wa Marekani wamesema kwamba wamemkamata mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 51 ambaye alifanya shambulio hilo.
Polisi walisema pia kwamba mwanaume huyo pia aliwatishia kuwapiga risasi watu wengine wawili waliotaka kumzuia asifanye shambulio hilo.
Dokta Tiller alikuwa miongoni mwa madaktari wachache wa Marekani ambao walikuwa tayari kutoa mimba zenye miezi zaidi ya mitano.
Dokta Tiller alikuwa akiandamwa na makundi ya watu wanaopinga utoaji mimba ambao walikuwa wakiandamana mara kwa mara kuelekea kwenye kliniki yake.
Mwaka 1986 kliniki yake ilipigwa bomu kwenye paa lake na kusababisha uharibifu mkubwa.
Mwaka 1993 Dokta Tiller alipigwa risasi kwenye mikono yake yote miwili nje ya kliniki yake na mwanaume mmoja ambaye baadae alikamatwa na kuhukumiwa kwenda jela miaka 11.
Katika tukio hilo mke wake alikuwa kwenye kundi la kwaya ya kanisa wakati shambulizi hilo lilipotokea.
Polisi walisema kwamba wanachunguza kuona kama shambulizi la jana linahusiana na kundi lolote la watu wanaopinga utoaji mimba.
Watu saba wakiwemo madaktari watatu wameishafariki hadi sasa nchini Marekani kutokana na vurugu za kupinga utoaji wa mimba.
Dokta George Tiller, 67, aliuliwa kwa kupigwa risasi moja asubuhi ya jumapili katika kanisa la kilutheri la mjini Wichita, Kansas.
Dokta Tiller alikuwa mtaalamu wa kutoa mimba za miezi mingi ambazo kwa kawaida kichanga kilichopo tumboni huwa kina uwezo wa kuendelea kukua hata kikiwa nje ya tumbo la uzazi kwa msaada wa mashine.
Polisi wa Marekani wamesema kwamba wamemkamata mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 51 ambaye alifanya shambulio hilo.
Polisi walisema pia kwamba mwanaume huyo pia aliwatishia kuwapiga risasi watu wengine wawili waliotaka kumzuia asifanye shambulio hilo.
Dokta Tiller alikuwa miongoni mwa madaktari wachache wa Marekani ambao walikuwa tayari kutoa mimba zenye miezi zaidi ya mitano.
Dokta Tiller alikuwa akiandamwa na makundi ya watu wanaopinga utoaji mimba ambao walikuwa wakiandamana mara kwa mara kuelekea kwenye kliniki yake.
Mwaka 1986 kliniki yake ilipigwa bomu kwenye paa lake na kusababisha uharibifu mkubwa.
Mwaka 1993 Dokta Tiller alipigwa risasi kwenye mikono yake yote miwili nje ya kliniki yake na mwanaume mmoja ambaye baadae alikamatwa na kuhukumiwa kwenda jela miaka 11.
Katika tukio hilo mke wake alikuwa kwenye kundi la kwaya ya kanisa wakati shambulizi hilo lilipotokea.
Polisi walisema kwamba wanachunguza kuona kama shambulizi la jana linahusiana na kundi lolote la watu wanaopinga utoaji mimba.
Watu saba wakiwemo madaktari watatu wameishafariki hadi sasa nchini Marekani kutokana na vurugu za kupinga utoaji wa mimba.