Apigwa Risasi Kanisani!

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,810
Daktari mtaalamu wa kutoa mimba za miezi zaidi ya mitano wa nchini Marekani ameuliwa kwa kupigwa risasi akiwa kanisani.

2134298.jpg


Dokta George Tiller, 67, aliuliwa kwa kupigwa risasi moja asubuhi ya jumapili katika kanisa la kilutheri la mjini Wichita, Kansas.

Dokta Tiller alikuwa mtaalamu wa kutoa mimba za miezi mingi ambazo kwa kawaida kichanga kilichopo tumboni huwa kina uwezo wa kuendelea kukua hata kikiwa nje ya tumbo la uzazi kwa msaada wa mashine.

Polisi wa Marekani wamesema kwamba wamemkamata mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 51 ambaye alifanya shambulio hilo.

Polisi walisema pia kwamba mwanaume huyo pia aliwatishia kuwapiga risasi watu wengine wawili waliotaka kumzuia asifanye shambulio hilo.

Dokta Tiller alikuwa miongoni mwa madaktari wachache wa Marekani ambao walikuwa tayari kutoa mimba zenye miezi zaidi ya mitano.

Dokta Tiller alikuwa akiandamwa na makundi ya watu wanaopinga utoaji mimba ambao walikuwa wakiandamana mara kwa mara kuelekea kwenye kliniki yake.

Mwaka 1986 kliniki yake ilipigwa bomu kwenye paa lake na kusababisha uharibifu mkubwa.

Mwaka 1993 Dokta Tiller alipigwa risasi kwenye mikono yake yote miwili nje ya kliniki yake na mwanaume mmoja ambaye baadae alikamatwa na kuhukumiwa kwenda jela miaka 11.

Katika tukio hilo mke wake alikuwa kwenye kundi la kwaya ya kanisa wakati shambulizi hilo lilipotokea.

Polisi walisema kwamba wanachunguza kuona kama shambulizi la jana linahusiana na kundi lolote la watu wanaopinga utoaji mimba.

Watu saba wakiwemo madaktari watatu wameishafariki hadi sasa nchini Marekani kutokana na vurugu za kupinga utoaji wa mimba.
 
Amepokea ujira gani na nyie bana? Sasa hao walomuua wanatofauti gani na yeye? Wote ni wauwaji ..period!
 
Amepokea ujira gani na nyie bana? Sasa hao walomuua wanatofauti gani na yeye? Wote ni wauwaji ..period!
alikuwa muuaji huyo.....kutoa mimba ni uuaji...na hao waliomuua nao wauaji....jino kwa jino
 
Amepokea ujira gani na nyie bana? Sasa hao walomuua wanatofauti gani na yeye? Wote ni wauwaji ..period!
Hata kama wamemuua, yeye hakuwa daktari pekee anayetoa mimba. Tuseme alikuwa maarufu na alikweka kazi hii hadharani.

Wapo madkatri wengi sana Marekani na wataalamu wazuri wa kuua vichanga. Yanatakiwa mapinduzi/ mabadiliko ya kiroho juu ya mtazamo wa kutoa mimba.

Kama hakuna mabadiliko ndani ya nafsi za watu... basi hawa madaktari watauawa sana! Nadhani ni vema mabadiliko yakaanzia kwa akina mama wenye vichanga hivi.
 
Not all member are Great Thinker!

Say: "Shall we tell you of those who lose most in respect of their deeds?-
"Those whose efforts have been wasted in this life, while they thought that they were acquiring good by their works?"
They are those who deny the Signs of their Lord and the fact of their having to meet Him (in the Hereafter): vain will be their works, nor shall We, on the Day of Judgment, give them any weight.
That is their reward, Hell, because they rejected Faith, and took My Signs and My Messengers by way of jest.


Q 18:103-106
 
Mods naona mmelala..'Wamasai' wamevamia disko huku..lol
 
Last edited:
“Our deepest fear is not that we are inadequate. Our deepest fear is that we are powerful beyond measure.

It is our light, not our darkness that most frightens us. We ask ourselves, Who am I to be brilliant, gorgeous, talented, fabulous? Actually, who are you not to be?

You are a child of God. Your playing small does not serve the world. There is nothing enlightened about shrinking so that other people won't feel insecure around you.

We are all meant to shine, as children do. We were born to make manifest the glory of God that is within us. It's not just in some of us; it's in everyone. And as we let our own light shine, we unconsciously give other people permission to do the same.

As we are liberated from our own fear, our presence automatically liberates others.”
 
Aliua viumbe ambavyo havisemi (vilivyomo tumboni mwa dada na mama zetu), na sasa umefika wakati wake....... Wacha naye aonje joto ya kifo.... na kama kuna moto, aungueeeeehhh mpaka basiiii
 
Back
Top Bottom