Mtaka Haki
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 492
- 149
Mfanyabiashara acharangwa mapanga katika vurugu za siasa
NA MWANDISHI WETU
11th October 2010
Vurugu zinazohusishwa na masuala ya kisiasa zimezuka katika mji mdogo wa Malampaka uliopo wilayani hapa Mkoa wa Shinyanga na kusababisha mfanyabiashara mmoja kujeruhiwa kwa kucharangwa kwa mapanga.
Vurugu hizo zinadaiwa kuwahusisha wafuasi wa vyama vya siasa wanaodaiwa kumvamia na kumcharanga kwa mapanga mfanyabiashara huyo, Charles Njige maarufu kwa jina la Mwanangolo wakimtaka ateremshe bendera ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) iliyokuwa inapeperushwa nje ya duka lake.
Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 5:30 asubuhi na kusababisha shughuli za kijamii kusimama kwa muda wa saa tano katika mji huo.
Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu mjini humo, Njige alisema kuwa akiwa dukani mwake, yalifika magari mawili yanayomilikiwa na mmoja wa wagombea ubunge wa Jimbo la Maswa Magharibi (jina tunalihofadhi) yakiwa na mabango ya picha yake na kuteremka watu watatu kila mmoja akiwa na panga.
Alisema watu hao ambao anawatambua (majina tunayo) waliingia moja kwa moja dukani kwake na kumweleza kuwa wako katika operesheni ya kuteremsha bendera zote za Chadema zinazopeperushwa katika mji huo na kudai yalikuwa ni maagizo ya mgombea ubunge huyo.
Aliongeza kusema kuwa baada ya kukataa kutekeleza agizo hilo, waliteremsha bendera hiyo na kuichanachana kisha kumcharanga kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake. Alisema kuwa alijitahidi kupambana nao huku akipiga yowe kuomba msaada. " Watu waliokuwa karibu na duka langu waliposikia kelele hizo, walifika na kuanza kupambana na watu hao kwa kutumia nondo, fimbo na mapanga na walizidiwa nguvu na hivyo kufanikiwa kutoroka wa kutumia magari hayo, " alisema.
Aliongeza kuwa baadaye alikwenda Kituo cha Polisi cha Malampaka kutoa taarifa za uvamizi huo, lakini alielezwa na askari mmoja mwenye cheo cha Koplo kuwa hawawezi kwenda kudhibiti vurugu hizo kwani walikuwa wamebaki askari wawili kituoni hapo na wengine walikwenda kwenye majukumu mengine hivyo kukosa msaada wa kituo hicho.
Mfanyabiashara huyo alisema majira ya saa 9:00 mchana gari la polisi lenye namba PT 638 lilifika likiwa na baadhi ya askari na kumkamata kiongozi wa vurugu hizo na kumuweka chini ya ulinzi katika kituo hicho.
Hata hivyo, alisema kundi la watu wapatao 300 walivamia kituo hicho huku wakipiga kelele za kutaka mtuhumiwa huyo aachiwe ili waweze kumshughulikia.
Alisema polisi waliwatawanya na kueleza kuwa hatua za kisheria zitachukua mkondo wake kwa watu wote waliohusika katika vurugu hizo na kuteremsha bendera za Chadema.
Inadaiwa kuwa mmoja wa viongozi waandamizi wa chama kimoja alisema chama chake kitaendelea na operesheni ya kushusha bendera za Chadema.
Polisi wilayani Maswa walithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kushikiliwa kwa mtuhumiwa aliyeongoza vurugu hizo kwa mahojiano zaidi.
Tangu kuanza kwa kampeni za kuelekea Uchaguzi Mkuu, wafuasi wa chama kimoja wilayani Maswa wamekuwa wakituhumiwa kuwafanyia fujo wagombea na wafuasi wa Chadema.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Kapteni mstaafu James Yamungu, alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kulaani kitendo hicho. Yamungu alisema chanzo chake ni mfuasi wa chama kimoja kuchana bendera ya Chadema.
" Nimewaagiza wafike ofisini kwangu na taarifa za tukio hilo nitazitoa baadaye.
Viongozi wa Chadema wa Wilaya ya Maswa hawakupatikana jana kuzungumzia suala hilo kwa kile kilichoelezwa kuwa walikuwa katika shughuli za kampeni.
Ofisa mmoja mwandamizi wa Jeshi la Polisi wilayani Maswa, jana alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kukataa kuzungumzia kwa undani kwa madai kuwa si msemaji.
Ofisa huyo alisema mtuhumiwa anayeshikiliwa huenda akafikishwa mahakamani leo kujibu mashtaka.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Daud Siasi, alipotafutwa jana kuzungumzia tukio hilo, simu yake ilikuwa ikiita bila majibu.
Source: Nipashe Oct 11
NA MWANDISHI WETU
11th October 2010
Vurugu zinazohusishwa na masuala ya kisiasa zimezuka katika mji mdogo wa Malampaka uliopo wilayani hapa Mkoa wa Shinyanga na kusababisha mfanyabiashara mmoja kujeruhiwa kwa kucharangwa kwa mapanga.
Vurugu hizo zinadaiwa kuwahusisha wafuasi wa vyama vya siasa wanaodaiwa kumvamia na kumcharanga kwa mapanga mfanyabiashara huyo, Charles Njige maarufu kwa jina la Mwanangolo wakimtaka ateremshe bendera ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) iliyokuwa inapeperushwa nje ya duka lake.
Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 5:30 asubuhi na kusababisha shughuli za kijamii kusimama kwa muda wa saa tano katika mji huo.
Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu mjini humo, Njige alisema kuwa akiwa dukani mwake, yalifika magari mawili yanayomilikiwa na mmoja wa wagombea ubunge wa Jimbo la Maswa Magharibi (jina tunalihofadhi) yakiwa na mabango ya picha yake na kuteremka watu watatu kila mmoja akiwa na panga.
Alisema watu hao ambao anawatambua (majina tunayo) waliingia moja kwa moja dukani kwake na kumweleza kuwa wako katika operesheni ya kuteremsha bendera zote za Chadema zinazopeperushwa katika mji huo na kudai yalikuwa ni maagizo ya mgombea ubunge huyo.
Aliongeza kusema kuwa baada ya kukataa kutekeleza agizo hilo, waliteremsha bendera hiyo na kuichanachana kisha kumcharanga kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake. Alisema kuwa alijitahidi kupambana nao huku akipiga yowe kuomba msaada. " Watu waliokuwa karibu na duka langu waliposikia kelele hizo, walifika na kuanza kupambana na watu hao kwa kutumia nondo, fimbo na mapanga na walizidiwa nguvu na hivyo kufanikiwa kutoroka wa kutumia magari hayo, " alisema.
Aliongeza kuwa baadaye alikwenda Kituo cha Polisi cha Malampaka kutoa taarifa za uvamizi huo, lakini alielezwa na askari mmoja mwenye cheo cha Koplo kuwa hawawezi kwenda kudhibiti vurugu hizo kwani walikuwa wamebaki askari wawili kituoni hapo na wengine walikwenda kwenye majukumu mengine hivyo kukosa msaada wa kituo hicho.
Mfanyabiashara huyo alisema majira ya saa 9:00 mchana gari la polisi lenye namba PT 638 lilifika likiwa na baadhi ya askari na kumkamata kiongozi wa vurugu hizo na kumuweka chini ya ulinzi katika kituo hicho.
Hata hivyo, alisema kundi la watu wapatao 300 walivamia kituo hicho huku wakipiga kelele za kutaka mtuhumiwa huyo aachiwe ili waweze kumshughulikia.
Alisema polisi waliwatawanya na kueleza kuwa hatua za kisheria zitachukua mkondo wake kwa watu wote waliohusika katika vurugu hizo na kuteremsha bendera za Chadema.
Inadaiwa kuwa mmoja wa viongozi waandamizi wa chama kimoja alisema chama chake kitaendelea na operesheni ya kushusha bendera za Chadema.
Polisi wilayani Maswa walithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kushikiliwa kwa mtuhumiwa aliyeongoza vurugu hizo kwa mahojiano zaidi.
Tangu kuanza kwa kampeni za kuelekea Uchaguzi Mkuu, wafuasi wa chama kimoja wilayani Maswa wamekuwa wakituhumiwa kuwafanyia fujo wagombea na wafuasi wa Chadema.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Kapteni mstaafu James Yamungu, alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kulaani kitendo hicho. Yamungu alisema chanzo chake ni mfuasi wa chama kimoja kuchana bendera ya Chadema.
" Nimewaagiza wafike ofisini kwangu na taarifa za tukio hilo nitazitoa baadaye.
Viongozi wa Chadema wa Wilaya ya Maswa hawakupatikana jana kuzungumzia suala hilo kwa kile kilichoelezwa kuwa walikuwa katika shughuli za kampeni.
Ofisa mmoja mwandamizi wa Jeshi la Polisi wilayani Maswa, jana alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kukataa kuzungumzia kwa undani kwa madai kuwa si msemaji.
Ofisa huyo alisema mtuhumiwa anayeshikiliwa huenda akafikishwa mahakamani leo kujibu mashtaka.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Daud Siasi, alipotafutwa jana kuzungumzia tukio hilo, simu yake ilikuwa ikiita bila majibu.
Source: Nipashe Oct 11