ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,972
- 1,649
Baada ya kupata ujauzito alihangaika kujua 'sex' ya mtoto kama akiwa wa kiume basi afunge uzazi maana tayari alishakuwa na mtoto wa kike. Baada ya kufanya vipimo vya ultr-sound, akaambiwa mtoto atakayezaliwa atakuwa wa kiume. Kumbe masikini hicho kipimo hakikuwa sahihi.
Siku ya kujifungua, akamwambia daktari kwamba wakati wa operesheni ya kumtoa mtoto, ni vyema amfunge na uzazi kabisa. Bila hiana siku ya operesheni daktari akamfunga kizazi mara alipomaliza kumzalisha kwa 'siza' kama wenyewe mnavyosema.
Ajabu ni pale mdada alipogundua kuwa mtoto alomzaa ni wa kike, ilihali alielezwa mwanzo na mtaalamu kuwa kachanga kangezaliwa ka kiume. Huu ni mwaka wa tatu sasa, mdada amebaki na huzuni kwa kujua kuwa hawezi tena kuzaa, na huo ndo umekuwa mwisho wa hamu yake ya kupata walau mtoto wa kiume ktk ndoa yake na mumewe.
Jamani mtoto ni mtoto tu, hata kama jamii zituzungukazo zinapenda zaidi vitoto vya kiume, hao wa kike imeonekana wengi ndo wenye kusaidia familia zao kuliko hao wa kiume. Mpende mtoto wako irrespective of her sex, jamani.
Siku ya kujifungua, akamwambia daktari kwamba wakati wa operesheni ya kumtoa mtoto, ni vyema amfunge na uzazi kabisa. Bila hiana siku ya operesheni daktari akamfunga kizazi mara alipomaliza kumzalisha kwa 'siza' kama wenyewe mnavyosema.
Ajabu ni pale mdada alipogundua kuwa mtoto alomzaa ni wa kike, ilihali alielezwa mwanzo na mtaalamu kuwa kachanga kangezaliwa ka kiume. Huu ni mwaka wa tatu sasa, mdada amebaki na huzuni kwa kujua kuwa hawezi tena kuzaa, na huo ndo umekuwa mwisho wa hamu yake ya kupata walau mtoto wa kiume ktk ndoa yake na mumewe.
Jamani mtoto ni mtoto tu, hata kama jamii zituzungukazo zinapenda zaidi vitoto vya kiume, hao wa kike imeonekana wengi ndo wenye kusaidia familia zao kuliko hao wa kiume. Mpende mtoto wako irrespective of her sex, jamani.