Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,266
- 33,039
Madirisha yaliyoachwa wazi ndiyo yaliyookoa maisha ya mwanamke huyu | Saturday, July 23, 2011 7:36 PM Unaweza usiamini kwamba madirisha yaliyokuwa yameachwa wazi ndiyo yaliyookoa maisha ya mwanamke mmoja nchini China ambaye alijirusha toka ghorofa ya tano. |
Mwanamke huyo mkazi wa Shanghai nchini China alijirusha mwenyewe toka ghorofa ya tano lakini alinusurika maisha yake kutokana na kujipigiza kwenye madirisha kadhaa yaliyokuwa yameachwa wazi. Kutokana na kujipigiza kwenye madirisha wakati akiporomoka toka ghorofa ya tano, spidi ya kuanguka kwake chini ilipungua na hivyo kumfanya apate majeraha kidogo na hivyo maisha yake kunusurika. Mwanamke huyo alijirusha mwenyewe mbele ya watu wengi waliokuwa wamejazana chini kumshuhudia mwanamke huyo akijiandaa kujirusha. Sababu ya kujirusha inaaminika kuwa kuna mtu alikuwa akimtisha mwanamke huyo na kupelekea mwanamke huyo aamue kujirusha mwenyewe kupitia kwenye dirisha la ghorofa ya tano. Mwanamke huyo ambaye jina lake halikutajwa, alifanya kitendo hicho ikiwa ni siku chache baada ya kugundulika anasumbuliwa na ugonjwa unaoitwa schizophrenia ambao humfanya mtu awe kama amechanganyikiwa na mwenye mashaka mashaka. Mwanamke huyo amelazwa hospitali na hali yake inaendelea vizuri. Gonga Linki chini kwa picha za kuanguka toka ghorofa ya tano za mwanamke huyo. |
<tbody>
</tbody>
Unaweza usiamini kwamba madirisha yaliyokuwa yameachwa wazi ndiyo yaliyookoa maisha ya mwanamke huyu wa nchini China ambaye alijirusha toka ghorofa ya tano.
<tbody>
</tbody>