Jana VINEGA wa Antivirus wakiongozwa na kinega mwandamizi SUGU (joseph wa sae),walidhihirisha kuwa hiphop bado ipo juu na haiwezi kufa kama baadhi ya wadau wanavyodai,Vinega waliingia uwanja wa sokoine saa moja jioni na walianza MAPACHA,DAN MSIMAMO,BOO NAko,HARDMARD,SISTA P,ISANGA FAMILY,ADILI,SALU T,MABAGA FRESH,SOGGY DOGGY ANTER, na wa mwisho alikuwa Sugu ambaye alipanda stage saa 3;28 usiku mpaka saa 4;15 usiku.Wasanii wengi walitumia beats wala si playback,watu waliparty mpaka basi na shangwe ilikuwa kubwa sana.HIPHOP mpango mzima.