Antibiotics

Fahamu tu ya kwamba hutakiwi kunywa antibiotics bila kuandikiwa na daktari. Sasa ukienda kwake ndio atakueleza zaidi
 
Ni dawa za kuua vijidudu vya magonjwa aina ya bacteria.
ni kama amoxilin, PPF nk
 
ANTIBIOTICS ni dawa zinazopigana na vijidudu vidogovidogo vinavyoitwa bacteria. Zipo za aina mbili, zinazozuia bacteria asikue na kuzaliana, yaani bacteriostatic, na zile zinazoua kabisa bacteria yaani bactericidal.
Kuna aina nyingi sana za antibiotics na kila moja wapo ina aina fulani ya bacteria ambazo huwadhibiti kwa ufanisi zaidi, na nyengine hazidhuru kabisa baadhi ya bacteria.
Kuna ambazo zinadhuru ama kuua aina nyingi sana za bacteria na hizi kitaalam wanaziita broad spectrum antibiotics, mfano ni kama ceftriaxone na wenzake.
Ili kudhibiti ukomavu wa dawa wa bacteria, inashauriwa watu wasitumie dawa hizi ila kwa ushauri wa daktari, na pale ngonjwa anapopewa dawa hizi, basi ahakikishe anamaliza dose/atumie dawa kama alivyoshauriwa na wataalamu.
Hili ni somo refu sana, ila kwa kifupi nimeeleza ni nini antibiotics.
Ahsante
 
Back
Top Bottom