makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Kama kuna Wabunge ambao wameudhi,wamekera,na kuwachefua Watanzania kwenye Mkutano wa Bunge uliomalizika hivi majuzi ni Anne Kilango Malecela. Mama huyu anayejipambanua kuwa ni mkereketwa na mpambanaji wa Ufisadi amejidhihirisha kuwa si lolote wala chochote baali ni mnafiki,mwongo na mbumbumbu asiyejua lolote kuhusu umuhimu wa Katiba ya Nchi.
Kitendo cha Anne Kilango kukomaa na kung'ang'ania kurudisha kipengele cha kuwaondoa Wakuu wa Wilaya(DCs)kwenye Mswada wa mchakato wa Katiba mpya kimemshushia hadhi kwa asilimia kubwa pamoja na kwamba kwa Wabunge wenzake wa CCM alionekana kuwa ni shujaa wa karne.
Nilimwangalia wakti akiwasilisha hoja yake ya kuwarudisha ma-DC kwenye mchakato wa Mswada wa Katiba Mpya. Anne Kilango aliongea kwa jazba huku mishipa ikiwa imemtoka,mate yakiruka huku na kule toka mdomoni na midomo akiipanua kama vile kile alichokuwa anatetea kina maslahi yoyote kwa Watanzania. Huyu mama alionekana KUMKOSEA ADABU HATA RAIS wake ambaye kwa ushauri wa vyama vya siasa na wadau mbalimbali aliliona hilo ya KUWA WAKUU WA WILAYA NI MAKADA WA CCM na wasingefaa kuhusishwa na mchakato huu kwani LAZIMA WATAEGEMEA KWENYE MASLAHI YA CHAMA CHAO CCM. Hapa Rais Kiwete ALITANGULIZA MASLAHI YA TAIFA NA SIYO CHAMA! Kwa kitendo hiki Anne Kilango Malecela alimpinga Rais na Mwenyekiti wa Chama chake na hivyo kuonyesha dharau ya wazi kabisa!! Lakini kwa vile alikuwa anatetea maslahi ya CCM na Wabunge wenzake hoja yake iliungwa mkono na Wabunge wote wa CCM.
Sasa basi mimi nasema hivi, Anne Kilango Malecela amejichongea. Lazima afuate nyayo za mmewe Samwel Malecela ifikapo 2015 au kama itatokea Uchaguzi kabla ya hapo. Kama Anne Kilango huwa anapitiapitia kwenye ukumbi huu wa JF basi ajue kuwa hizo ndiyo salamu. ASITEGEMEE KURUDI BUNGENI TENA BAADA YA KIPINDI HICHI. Namwambia asahau. Huyu mama asifikiri Watanzania wa sasa ni wale ambao mmewe Mzee Malecela aliwahi kuwaambia,THEY CAN GO TO HELL baada ya kubanwa maswali Bungeni kuhusiana na usafiri wa Treni miaka ile ya Mwalimu.
Anne Kilango Malecela hizo ndiyo salamu za mjomba. Huwezi kuleta dharau zako Bungeni kwa kutetea wakuu wa Wilaya kwa kutanguliza maslahi binafsi na Chama Chako cha Magamba ili wakusaidie wakti wa uchaguzi kuchakachua kura zetu. Sasa ujue kuwa pamoja na kuwatetea ma-DC lazima uondoka Bungeni.
Wasalaam.
Kitendo cha Anne Kilango kukomaa na kung'ang'ania kurudisha kipengele cha kuwaondoa Wakuu wa Wilaya(DCs)kwenye Mswada wa mchakato wa Katiba mpya kimemshushia hadhi kwa asilimia kubwa pamoja na kwamba kwa Wabunge wenzake wa CCM alionekana kuwa ni shujaa wa karne.
Nilimwangalia wakti akiwasilisha hoja yake ya kuwarudisha ma-DC kwenye mchakato wa Mswada wa Katiba Mpya. Anne Kilango aliongea kwa jazba huku mishipa ikiwa imemtoka,mate yakiruka huku na kule toka mdomoni na midomo akiipanua kama vile kile alichokuwa anatetea kina maslahi yoyote kwa Watanzania. Huyu mama alionekana KUMKOSEA ADABU HATA RAIS wake ambaye kwa ushauri wa vyama vya siasa na wadau mbalimbali aliliona hilo ya KUWA WAKUU WA WILAYA NI MAKADA WA CCM na wasingefaa kuhusishwa na mchakato huu kwani LAZIMA WATAEGEMEA KWENYE MASLAHI YA CHAMA CHAO CCM. Hapa Rais Kiwete ALITANGULIZA MASLAHI YA TAIFA NA SIYO CHAMA! Kwa kitendo hiki Anne Kilango Malecela alimpinga Rais na Mwenyekiti wa Chama chake na hivyo kuonyesha dharau ya wazi kabisa!! Lakini kwa vile alikuwa anatetea maslahi ya CCM na Wabunge wenzake hoja yake iliungwa mkono na Wabunge wote wa CCM.
Sasa basi mimi nasema hivi, Anne Kilango Malecela amejichongea. Lazima afuate nyayo za mmewe Samwel Malecela ifikapo 2015 au kama itatokea Uchaguzi kabla ya hapo. Kama Anne Kilango huwa anapitiapitia kwenye ukumbi huu wa JF basi ajue kuwa hizo ndiyo salamu. ASITEGEMEE KURUDI BUNGENI TENA BAADA YA KIPINDI HICHI. Namwambia asahau. Huyu mama asifikiri Watanzania wa sasa ni wale ambao mmewe Mzee Malecela aliwahi kuwaambia,THEY CAN GO TO HELL baada ya kubanwa maswali Bungeni kuhusiana na usafiri wa Treni miaka ile ya Mwalimu.
Anne Kilango Malecela hizo ndiyo salamu za mjomba. Huwezi kuleta dharau zako Bungeni kwa kutetea wakuu wa Wilaya kwa kutanguliza maslahi binafsi na Chama Chako cha Magamba ili wakusaidie wakti wa uchaguzi kuchakachua kura zetu. Sasa ujue kuwa pamoja na kuwatetea ma-DC lazima uondoka Bungeni.
Wasalaam.