Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 6,376
- 6,720
Kwa wanaokumbuka gea kubwa aliyoingia nayo waziri wa Ardhi maendeleo na makazi profesa Anna Tibaijuka wanajiuliza: je ilikuwa ni nguvu ya soda au amezimwa na mafisadi kama siyo bosi wake? Maana siku hizi hasikiki akitoa taarifa ya viwanja alivyorejesha au kuamuru virejeshwe. Je amekatiwa chake akaamua kuuchuna au ametishwa na washirika wa bosi wake? Kweli Tanzania ni nchi ya sanaa. Leo tunaye anayewika Dk Harrison Mwakyembe. Kesho utasikia kanywea hafurukuti kama rafiki yake Samuel Sitta waliyeungana kusaliti ukombozi wa taifa kwa tamaa ya vyeo uchwara. Je nini kimemsibu Anna Tibaijuka?