Angetile osia ameshindwa kuongoza tff

kazikubwa

JF-Expert Member
Oct 8, 2010
597
143
Kama kuna mtu ameandika historia mbaya ya uongozi wa soka hapa nchini ni huyu bwana. Katika kipindi chake akiwa kama katibu ameshindwa kuwa thabiti na kusababisha migongano ya hapa na pale kati ya Klabu na TFF au kati ya Klabu na Klabu.

Matatizo aliyosababisha kwa uchache ni kama yafuatayo:
1. Kukosekana kwa waamuzi thabiti wa soka na kupanga waamuzi hasa wa mechi za Yanga kwa upendeleo
2. Kuwepo kwa usimamizi mbaya wa soka na fedha za TFF
3. Kuwa na maandalizi duni kwa timu zetu za Taifa

Na wenzangu ongezeeni hapo chini. Cha msingi kwake ni kujiuzulu ili kuleta imani kwa wapenzi wa soka na kujijengea heshima kabla ya kulazimishwa kufanya hivyo.
 
Kama kuna mtu ameandika historia mbaya ya uongozi wa soka hapa nchini ni huyu bwana. Katika kipindi chake akiwa kama katibu ameshindwa kuwa thabiti na kusababisha migongano ya hapa na pale kati ya Klabu na TFF au kati ya Klabu na Klabu.

Matatizo aliyosababisha kwa uchache ni kama yafuatayo:
1. Kukosekana kwa waamuzi thabiti wa soka na kupanga waamuzi hasa wa mechi za Yanga kwa upendeleo
2. Kuwepo kwa usimamizi mbaya wa soka na fedha za TFF
3. Kuwa na maandalizi duni kwa timu zetu za Taifa

Na wenzangu ongezeeni hapo chini. Cha msingi kwake ni kujiuzulu ili kuleta imani kwa wapenzi wa soka na kujijengea heshima kabla ya kulazimishwa kufanya hivyo.

Kinachomlinda huyu jamaa ni kufanyakazi na waandishi wa habari kwa kipindi kirefu akiwa ni Mhariri, na ndio maana wanashindwa kumwandika mwenzao. Na hii ndio sababu hasa ya akina Tenga kumweka hapo ili kuzima madudu yao yasitoke magazetini, ila huyu jamaa ni kimeo hasa.
Hebu ona hata tatizo la ucheleweshaji wa ratiba ya ligi kuu, wakati ndio kazi kuu ya TFF ukiondoa maandalizi ya timu ya Taifa, inayoendelea kuporomoka kwenye viwango kila kukicha.
Jambo la muhimu alilofanya tangu aingie madarakani ni yeye kwenda kutibiwa India kutokana na matatizo ya kichwa, lakini mambo mengine yote amekuwa akichemsha tu, na hakuna wa kumkosoa kwani kila mwandishi ni rafiki yake au vijana wake aliokuwa akiwatuma kazi alipokuwa mhariri.
 

Kinachomlinda huyu jamaa ni kufanyakazi na waandishi wa habari kwa kipindi kirefu akiwa ni Mhariri, na ndio maana wanashindwa kumwandika mwenzao. Na hii ndio sababu hasa ya akina Tenga kumweka hapo ili kuzima madudu yao yasitoke magazetini, ila huyu jamaa ni kimeo hasa.
Hebu ona hata tatizo la ucheleweshaji wa ratiba ya ligi kuu, wakati ndio kazi kuu ya TFF ukiondoa maandalizi ya timu ya Taifa, inayoendelea kuporomoka kwenye viwango kila kukicha.
Jambo la muhimu alilofanya tangu aingie madarakani ni yeye kwenda kutibiwa India kutokana na matatizo ya kichwa, lakini mambo mengine yote amekuwa akichemsha tu, na hakuna wa kumkosoa kwani kila mwandishi ni rafiki yake au vijana wake aliokuwa akiwatuma kazi alipokuwa mhariri.

Sijafanya uchunguzi sana lakini naweza kukubaliana na wewe kwa kuwa moja kati ya sifa kuu za uongozi mbovu ni migogoro isiyoisha
 
poa nami nakubaliana na wewe jamaa hili ni mzigo mkubwa sana tff ila mkataba wake unaisha january 2013 sizani kama ataongezewa mkataba mwingine na rais ajae.
 
Kama kuna mtu ameandika historia mbaya ya uongozi wa soka hapa nchini ni huyu bwana. Katika kipindi chake akiwa kama katibu ameshindwa kuwa thabiti na kusababisha migongano ya hapa na pale kati ya Klabu na TFF au kati ya Klabu na Klabu.

Matatizo aliyosababisha kwa uchache ni kama yafuatayo:
1. Kukosekana kwa waamuzi thabiti wa soka na kupanga waamuzi hasa wa mechi za Yanga kwa upendeleo
2. Kuwepo kwa usimamizi mbaya wa soka na fedha za TFF
3. Kuwa na maandalizi duni kwa timu zetu za Taifa

Na wenzangu ongezeeni hapo chini. Cha msingi kwake ni kujiuzulu ili kuleta imani kwa wapenzi wa soka na kujijengea heshima kabla ya kulazimishwa kufanya hivyo.

Niliwahi kuuliza huyu jamaa amepataje Ukatibu mkuu wa TFF? Nadhani ni moja ya MAAJABU yaliyowahi kulikumba Soka la bongo ambalo hatutalisahau maisha ni Angetile kuwa katibu mkuu wa TFF ......... Mimi naungana mkono na wewe kabisa kama nchi hii ina watu walioshindwa na hawafai kuongoza sekta zinazohusiana na jamii jamaa huyu anaongoza, jamaa anapwaya sana ni mwepesi, na anaonyesha kuwa na maslahi binafsi na klabu ya Yanga, sikatai mapenzi ya mtu, lakini kwa Angetile ni bomu kwa hali yoyote hawezi kugombea tena mkataba wake ukiisha na akarudi madarakani,
 
Mimi natofautiana na wengi hapa.Labda tujiulize maswali kwamba Angetile ameshindwa kuongoza TFF kama Entity au ameshindwa kuongoza soka la Tanzania kama sector.Kwa sababu unapoongela failures za TFF huwezi kuacha kuongelea failures kwa soka la Tanzania.Na kwa maoni yangu mimi kushuka(failures) za soka la TZ/TFF ni mfumo zaidi kuliko mtu mmoja na kwa watu ambao tupo kwenye soka la Tanzania tunaweza sema TFF kuna transparency zaidi kuliko kipindi chochote nilichokiona,lakini hii inawezekana kutoka na kipindi tulichopo.
TFF ipo kwa kushirikiana na serikali kuendeleza policy(kama zipo) za kuendeleza na kunyanyua kiwango cha soka letu,vitu kama michezo ya UMITASHUTA,UMISETA ndio ilikuwa chimbuko la wanamichezo wetu sio kwa soka tu hata michezo mingine.
Kwa hiyo nafikiri tusiangalie tu failures za Angetile kama yeye bali TFF kama chombo kwa upande mmoja na serikali kwa uapnde mwingine.Na tuache ugonjwa tulio nao waTanzania wa Usimba na UYanga
 
Mimi natofautiana na wengi hapa.Labda tujiulize maswali kwamba Angetile ameshindwa kuongoza TFF kama Entity au ameshindwa kuongoza soka la Tanzania kama sector.Kwa sababu unapoongela failures za TFF huwezi kuacha kuongelea failures kwa soka la Tanzania.Na kwa maoni yangu mimi kushuka(failures) za soka la TZ/TFF ni mfumo zaidi kuliko mtu mmoja na kwa watu ambao tupo kwenye soka la Tanzania tunaweza sema TFF kuna transparency zaidi kuliko kipindi chochote nilichokiona,lakini hii inawezekana kutoka na kipindi tulichopo.
TFF ipo kwa kushirikiana na serikali kuendeleza policy(kama zipo) za kuendeleza na kunyanyua kiwango cha soka letu,vitu kama michezo ya UMITASHUTA,UMISETA ndio ilikuwa chimbuko la wanamichezo wetu sio kwa soka tu hata michezo mingine.
Kwa hiyo nafikiri tusiangalie tu failures za Angetile kama yeye bali TFF kama chombo kwa upande mmoja na serikali kwa uapnde mwingine.Na tuache ugonjwa tulio nao waTanzania wa Usimba na UYanga

Kaka 2naanzia kwa TFF then ndo SOKA kwa ujumla, kifupi Osiah kabla hajaingia TFF alikuwa mbele kuipgia kelele taasisi hii lakn alipopewa mwana alee AIBU TUPU. Kwanza hajiheshim akiwa kama kiongozi wa TFF, hatukatai kuwa inawezekana karibia kila Mtanzania ana itikadi yake ya Usimba na Uyanga lakn unapopewa dhamana ya kuongoza taasisi kama TFF jaribu kuwa na busara kidogo. Angetile Yanga ikishinda akifika Bar anamwaga ofa huku anatamka maneno ya kishabiki kwa Yanga. Osiah haingii hata robo ya uwezo wa katibu aliyemtangulia, Mwakalebela.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom