Mbelwa Germano
JF-Expert Member
- May 7, 2011
- 789
- 289
Kama kuna jambo kubwa ambalo Watanzania wengi limewaathiri kifikra ni utawala wa CCM. Monopolization chini ya CCM imewafanya watu wengi ndani ya Taifa hili kuwa na fikra tegemezi, kukosa muda wa kutafakari mara mbili, kuwa wepesi wa kuhukumu na kukubali kuishi kwa mazoea.
Jambo hili bado limewaathiri hata wana-mageuzi nchini, wana-CHADEMA, baadhi ya wana-CDM wamekuwa wepesi kutekwa fikra zao, wepesi kuhukumu na kukubali kurudi kule ambako NCCR ya Mrema ilipotea.
Wanafikiri kuwa na fikra na mitazamo tofauti ndani ya chama ni chanzo cha vurugu na misuguano. Wameshindwa kutafsiri maana halisi ya migogoro na kuhisi kwamba wako mstari wa mbele kuepusha migogoro na kusahau kwamba wanajenga migogoro, wamelewa na mafanikio ya ghafla.
Wengi wanahisi kwamba wanaweza kuishi na kudumu nje ya demokrasia bila kuweka utaratibu wa kidemokrasia. Wamekataa kuishi kwa kudadisi bali wamekubali kuishi kwa kuhisi. Wamekataa kupima afya ya fikra zao na kutumia propaganda na maneno rahisi kuhalalisha agenda zao.Hatuwezi kamwe kufika kwa mtindo huu.
Lazima kwanza wajifunze kuwekeza kwenye siasa za akili na maarifa na hivi ndivyo chama chenye demokrasia pevu hufanya. Ukikataa njia ya majadiliano chini ya hoja kinzani ni kuhalalisha udhaifu na uwezo mdogo wa kifikra.
Zipo tofauti kubwa za kimtazamo na kifikra kati ya Mbowe, Dr.Slaa na Zitto lakini tofauti hizi haziwezi kuwa na athari iwapo zinafuata misingi na kanuni za chama. Leo ukiongelea kuhusu Zitto watasema umetumwa, ukitoa mapendekezo Dr. Slaa agombee uenyekiti wa chama watasema umetumwa, je nani ambaye atazungumza kuhusu Zitto na watasema hajatumwa.
Zitto ni Naibu Katibu Mkuu wa chama, nilitegemea wakati wa matukio makubwa ya chama Mwenyekiti wa chama angewaeleza wana-mageuzi kwa nini Zitto hayupo lakini hili halifanyiki. Ni wangapi waliwahi kuhoji ni kwa nini? Au tumeridhika na jibu rahisi ni MSALITI. Rejea NCCR ya Mrema na tafakari tafsiri halisi ya mgogoro. Hili ni tatizo. Na tatizo lipo ndani ya chama. Kama tumekataa hoja na na fikra kinzani kama moja ya kanuni za kidemokrasia basi tusitarajie kuishi kwa muda mrefu ndani ya ulingo wa siasa za kiushindani.
Kamwe wana-CDM tusibweteke na mafanikio ya sasa, bado tuna kazi kubwa ya kujenga chama. Mabadiliko ndani ya chama ni Muhimu.
Jambo hili bado limewaathiri hata wana-mageuzi nchini, wana-CHADEMA, baadhi ya wana-CDM wamekuwa wepesi kutekwa fikra zao, wepesi kuhukumu na kukubali kurudi kule ambako NCCR ya Mrema ilipotea.
Wanafikiri kuwa na fikra na mitazamo tofauti ndani ya chama ni chanzo cha vurugu na misuguano. Wameshindwa kutafsiri maana halisi ya migogoro na kuhisi kwamba wako mstari wa mbele kuepusha migogoro na kusahau kwamba wanajenga migogoro, wamelewa na mafanikio ya ghafla.
Wengi wanahisi kwamba wanaweza kuishi na kudumu nje ya demokrasia bila kuweka utaratibu wa kidemokrasia. Wamekataa kuishi kwa kudadisi bali wamekubali kuishi kwa kuhisi. Wamekataa kupima afya ya fikra zao na kutumia propaganda na maneno rahisi kuhalalisha agenda zao.Hatuwezi kamwe kufika kwa mtindo huu.
Lazima kwanza wajifunze kuwekeza kwenye siasa za akili na maarifa na hivi ndivyo chama chenye demokrasia pevu hufanya. Ukikataa njia ya majadiliano chini ya hoja kinzani ni kuhalalisha udhaifu na uwezo mdogo wa kifikra.
Zipo tofauti kubwa za kimtazamo na kifikra kati ya Mbowe, Dr.Slaa na Zitto lakini tofauti hizi haziwezi kuwa na athari iwapo zinafuata misingi na kanuni za chama. Leo ukiongelea kuhusu Zitto watasema umetumwa, ukitoa mapendekezo Dr. Slaa agombee uenyekiti wa chama watasema umetumwa, je nani ambaye atazungumza kuhusu Zitto na watasema hajatumwa.
Zitto ni Naibu Katibu Mkuu wa chama, nilitegemea wakati wa matukio makubwa ya chama Mwenyekiti wa chama angewaeleza wana-mageuzi kwa nini Zitto hayupo lakini hili halifanyiki. Ni wangapi waliwahi kuhoji ni kwa nini? Au tumeridhika na jibu rahisi ni MSALITI. Rejea NCCR ya Mrema na tafakari tafsiri halisi ya mgogoro. Hili ni tatizo. Na tatizo lipo ndani ya chama. Kama tumekataa hoja na na fikra kinzani kama moja ya kanuni za kidemokrasia basi tusitarajie kuishi kwa muda mrefu ndani ya ulingo wa siasa za kiushindani.
Kamwe wana-CDM tusibweteke na mafanikio ya sasa, bado tuna kazi kubwa ya kujenga chama. Mabadiliko ndani ya chama ni Muhimu.