Angalia uzushi wa DailyNnews. Wameanza tena...

Kwani Daily news wanadhani hatuna taarifa za mkuu wao huyo kulalamikiwa na waandishi wake wa kiike kuwa mwanzoni mwa miaka ya 2000 alikuwa akiwanyanyasa kijinsia kiasi cha malalamiko hayo kupelekwa serikalini? Labda ni kwasababu Nguruwe alikuwa akipewa kazi ya kulinda shamba la mihogo.
Tafadhali ondokana na kulalamika. Kama una takwimu ziweke wazi huu ndio wakati wa kuwajua kwa undani wale ambao wanawania uongozi wa nchi yetu. Asiogopwe mtu na asionwewe mtu. Tujuzane kwa kujenga hoja na si masihara.
 
slaa%26Rose.jpg

Sijui kwa nini alimwacha huyu bila talaka...
 
Hizo ni hadithi za alinacha!!!! Unganeni tu hao daily news lakini hampati kitu hapa hatudanganyiki!!!!!!!!!!!! Je, huyo mwandishi wenu anaijua sheria ya ndoa inasemaje? Kama walishatalikiana sisi hatujui

uamuzi ni kumpatia madaraka dr. Slaa mambo mengine baadaye! Ikulu patakatifu je wanayofanya akina jk na timu yake yanakubalika ikulu? Wa-tz tuache uvivu wa kufikiria.
 
hivi si hawa hawa daily news walisema slaa hatakuwa raisi, tena wakasema kwa kujiamini. Sasa wana wasiwasi gani kuwa ataingia ikulu akiwa mchafu na josephine kama fist lady akiwa na pete mbili moja ya mahimbo na nyingine ya slaa.

Kweli kama huu ndio uandishi wa habari, nchi imekwisha, hivi mtu utaandikaje utumbo kama huo na kuitetea ccm sasa sijui makala inahusu nini as such, mara pope, mara ccm mara sijui uchafu gani jeee. Na je si kesi iko mahakamani? Kuanza kumhukumu slaa kwa kesi iliyopo mahakamani kuwa ni mwizi, si kuingilia uhuru wa mahakama? Jaji mkuu uko wapi

waache watapetape si unajua tena mfa maji!!! Pete ya mahimbo tutaichoma moto au tutaitupilia mbali. Ikulu ni ya dr. Slaa safari hii.
 
Two wrongs do not make it right. Hakuna shaka wote ni waovu.
LeopoldByongje, hivi hujagundua kwamba mnavyozidi kumwandama Dr. ndivyo umaarufu wake unavyozidi kupaa na mgombea wenu anavyozidi kukataliwa na wananchi. Endeleeni tu lakini mkae mkijua kuwa tarehe 31, Octoba wananchi watatoa hukumu yao na onyo kwenu ni kutojaribu kuchakachua/kuiba hizo kura hizo kura kama kawaida yenu. Sasa twasubiri hao wastaafu wenu nao waingie ulingoni tuwape vidonge vyao, duh raha ilioje !
 
LeopoldByongje, hivi hujagundua kwamba mnavyozidi kumwandama Dr. ndivyo umaarufu wake unavyozidi kupaa na mgombea wenu anavyozidi kukataliwa na wananchi. Endeleeni tu lakini mkae mkijua kuwa tarehe 31, Octoba wananchi watatoa hukumu yao na onyo kwenu ni kutojaribu kuchakachua/kuiba hizo kura hizo kura kama kawaida yenu. Sasa twasubiri hao wastaafu wenu nao waingie ulingoni tuwape vidonge vyao, duh raha ilioje !
Acha kuota wewe...
 
Suala hili ilipaswa liwe la kibinafsi na si la kitaifa. Inabidi tuangalie masuala yanayohusu taifa na ndiyo tuyajadili. Lakini kwa vile Mheshimiwa Silaa anataka kuongoza nchi ni budi awe mwangalifu katika nyendo zake binafsi asije kujichanganya na kulichanganya taifa.

Mwalimu Nyerere alitutahadhalisha kuwa IKULU ni mahala patakatifu. Si pahala pa kuficha wahuni au pango la walanguzi.Hapo ndipo hoja ya uwajibikaji inaibuliwa. Hapa hoja ni je mtu huyu huwa hafanyi utafiti au uchunguzi kabla ya kufanya maamuzi? Je hana washauri wazuri?

Maisha yake binafsi iwapo yatajaa utata na akawa haeleweki au atabiriki si ajabu watu wakakosa imani naye. Kumbuka kulikuwa na mjadala hapa janvini watu wakichambua maisha ya Dr Silaa hususan kutokuwa na makazi yanayoeleweka. Ziliibuliwa taarifa kuwa huyu Mheshimiwa anaishi Guest house ukipenda Hotel. Hivi ni viashiria kuhusu aiba na tasiwira ya maisha ya kiongozi wetu mtarajiwa.

Hapa inabidi watu waanze kuhoji kulikoni Mtu ambaye anatushawishi tumkabidhi nchi je anaaminika na ni mkweli? Je anaweza kulinda kwa dhati masilahi ya wengi? Je anaweza kusimamia haki? Je anachukizwa na dhuluma? Na mambo kama hayo.

Katika Biblia kuna hadithi ya Mfalme aliyemtamani na hatimaye kutembea na mke wa jemadari wake. Jemadari huyo akiwa vitani huku nyuma mfalme anajinafasi na mkewe hadi yule mama kapata uja uzito.

Baada ya kugunda hilo Mfalme akamuita haraka jemadari arejee nyumbani. Alipofika akamwambia apumzike japo kwa siku chache. Jemadari alitii lakini hakukubali kulala ndani nyumbani kwake kwa vile aliamini haikuwa vyema yeye astarehe wakati wapiganaji wenzake wanakufa huko vitani. Hivyo hakukutana kimwili na mkewe. Mfalme alipobaini kuwa mtego aliouweka haukunasa alimrejesha mstari wa mbele na akafanya kila liwezekanalo jemadari huyo akauawa.

Hapa tunaoneshwa dhuluma kwa kutumia madaraka. Iwapo mgombea huyo ana ugonjwa huo si ajabu akiingia ikulu akaendeleza tabia hiyo. Kwanza hakuhojiwa wakati wa Kampeini kuhusu tabia hiyo ili aiache. Pili pale ambapo wanaotaka kuhoji iwe kwa nia njeam au mbaya wanibuka watu kumtetea asisemwe au asihojiwe kwa sababu chungu nzima.

Lakini tukumbuke kuwa Mheshimiwa Silaa pia ana rekodi ya kutokuwa makini na masuala ya Unyumba na Nyumba. Zipo taarifa kuwa alizaa na mwanamke mwingine watoto wawili lakini huyo Mzazi mwenzie eti hawakuwa wachumba!!! Nasema taarifa kama hizi zinatuonesha kuwa pamoja na uzuri na mvuto nk. mambo haya yanaweza kutia doa machoni mwa wapiga kura. Wanasema mchelea mwana kulia ulia mwenyewe. Tusilee ugonjwa. Kwa wapenzi wa Dr. Silaa mpeni ushauri ajirekebishe Muda bado anao.

Kazi kwenu

Nafikiri kabla hamjamwambia Dk Slaa ajirekebishe naomba mjirekebishe ninyi ambao mnaoonekana ni wapuuzi,guesthouse are you real sure msipende kuwa washabiki kwa mambo msiyoyajua.

Ngoja tutaona haya mnayoyaandika; na kwa taarifa niliyo nayo jamaa anataka ku-withdraw kesi maana CCM ameshawaona ni wazushi na ukweli anao yeye mwenyewe.

Ningewashauri jambo msilolijua ni kama usiku wa giza acheni ushabiki wa kipuuzi mngeijua sheria ya ndoa mliyoelezwa hapo juu mngetulia subiri muone mahakama itajibu nini wangekuwa makini wansingetupilia mpaka tarehe 15 sasa itakula kwao.
 
Hivi ikatokea CHADEMA/Slaa akaingia ikulu jamaa naona watawahi wenyewe ubungo asubuuhi na familia zao kurudi makwao, hawatangoja.....
Waulize wale wapinzani wa Kikwete ambao hawakudhani atakwenda ikulu na wakabaki wakishabikia wakina Sumaye na Salim nini kiliwapata!
 
Mwandishi wa Daily News amesahau yaliyomkuta mwandishi wa uganda ben Bell miaka ya sabini wakati wa utawala wa IDD AMINI NAYEYE ANATAKA KWENDA UHAMISHONI ASUBIRI WAO WANAAMIONIN KUWA JK ATASHINDA ATHUBUTU JK NA CCM YAKE AMEFICHA MOTO KWENYE MAJANI MAKAVU
 
slaa%26Rose.jpg

Sijui kwa nini alimwacha huyu bila talaka...

inahuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu kweli hayo ni maisha yake binafsi tunaangalia matunda tutayofaidi kutokana na kazi nzuri anayofanyia jamii ya watanzania
 
Suala hili ilipaswa liwe la kibinafsi na si la kitaifa. Inabidi tuangalie masuala yanayohusu taifa na ndiyo tuyajadili. Lakini kwa vile Mheshimiwa Silaa anataka kuongoza nchi ni budi awe mwangalifu katika nyendo zake binafsi asije kujichanganya na kulichanganya taifa.

Mwalimu Nyerere alitutahadhalisha kuwa IKULU ni mahala patakatifu. Si pahala pa kuficha wahuni au pango la walanguzi.Hapo ndipo hoja ya uwajibikaji inaibuliwa. Hapa hoja ni je mtu huyu huwa hafanyi utafiti au uchunguzi kabla ya kufanya maamuzi? Je hana washauri wazuri?

Maisha yake binafsi iwapo yatajaa utata na akawa haeleweki au atabiriki si ajabu watu wakakosa imani naye. Kumbuka kulikuwa na mjadala hapa janvini watu wakichambua maisha ya Dr Silaa hususan kutokuwa na makazi yanayoeleweka. Ziliibuliwa taarifa kuwa huyu Mheshimiwa anaishi Guest house ukipenda Hotel. Hivi ni viashiria kuhusu aiba na tasiwira ya maisha ya kiongozi wetu mtarajiwa.

Hapa inabidi watu waanze kuhoji kulikoni Mtu ambaye anatushawishi tumkabidhi nchi je anaaminika na ni mkweli? Je anaweza kulinda kwa dhati masilahi ya wengi? Je anaweza kusimamia haki? Je anachukizwa na dhuluma? Na mambo kama hayo.

Katika Biblia kuna hadithi ya Mfalme aliyemtamani na hatimaye kutembea na mke wa jemadari wake. Jemadari huyo akiwa vitani huku nyuma mfalme anajinafasi na mkewe hadi yule mama kapata uja uzito.

Baada ya kugunda hilo Mfalme akamuita haraka jemadari arejee nyumbani. Alipofika akamwambia apumzike japo kwa siku chache. Jemadari alitii lakini hakukubali kulala ndani nyumbani kwake kwa vile aliamini haikuwa vyema yeye astarehe wakati wapiganaji wenzake wanakufa huko vitani. Hivyo hakukutana kimwili na mkewe. Mfalme alipobaini kuwa mtego aliouweka haukunasa alimrejesha mstari wa mbele na akafanya kila liwezekanalo jemadari huyo akauawa.

Hapa tunaoneshwa dhuluma kwa kutumia madaraka. Iwapo mgombea huyo ana ugonjwa huo si ajabu akiingia ikulu akaendeleza tabia hiyo. Kwanza hakuhojiwa wakati wa Kampeini kuhusu tabia hiyo ili aiache. Pili pale ambapo wanaotaka kuhoji iwe kwa nia njeam au mbaya wanibuka watu kumtetea asisemwe au asihojiwe kwa sababu chungu nzima.

Lakini tukumbuke kuwa Mheshimiwa Silaa pia ana rekodi ya kutokuwa makini na masuala ya Unyumba na Nyumba. Zipo taarifa kuwa alizaa na mwanamke mwingine watoto wawili lakini huyo Mzazi mwenzie eti hawakuwa wachumba!!! Nasema taarifa kama hizi zinatuonesha kuwa pamoja na uzuri na mvuto nk. mambo haya yanaweza kutia doa machoni mwa wapiga kura. Wanasema mchelea mwana kulia ulia mwenyewe. Tusilee ugonjwa. Kwa wapenzi wa Dr. Silaa mpeni ushauri ajirekebishe Muda bado anao.

Kazi kwenu

:mad::smow:
Usihukumu ili nawe usije ukahukumiwa. Sioni mantiki ya hoja hizo. Mosi huyu bwana kasema yule ni mchumba wake tu, sio mkewe. Sheria ya ndoa haitambui uchumba (not legaly binding agreement). Pili uchumba ni kipindi cha walio katika kusudio la ndoa kuchunguzana. Labda utukumbushe kesi yoyote duniani ambapo mchumba alitiwa hatiani kwa kosa la kuoa? Kama kuzaa watoto wawili na mama mwingine ni discualification ya uongozi, let JK be the first to step out, Riziwani na Mdogo wake (mratibu wa kampeni pale upanga), si watoto wa kuzaa wa mama Salma (toa boriti kwenye jicho lako!!!!!!).
Kiongozi wa watu huaminiwa na watu wake, hupendwa na watu wake, tembelea karatu upate majibu ya maswali yako.
 
Two wrongs do not make it right. Hakuna shaka wote ni waovu.

Problem of Tanzanians they always think of life after crossing the bridge, without knowing how best they could cross it.
Guys are you real serious, who says Dr. Slaa Get married to Josephine? Kuweni makini na hoja uchumba si ndoa. Daily news na wote wenye fikra mgando acheni fikra za kizinzi.
 
Back
Top Bottom