"THE PROBLEMS CANNOT BE SOLVED BY THE SAME LEVEL OF THINKING THAT CREATED THEM - YOU GUYS YOU ARE TIRED"
big THUMB commander
Wanyalukolo hongereni,kwa uchaguzi wenu.
WEWE Kama sio MAGAMBA sijui! Muda aliopewa pale wa DK 15 kuelezea yote hayo hautoshi..Maana Wana magamba wana VIROJA laki 9 na nusu...Alichofanya pale ni Summary tu! ww hujui soma Nyakati wala hujui fanya interpretation, Uwezo wako utakuwa Mdogosana kama wana Magamba ndio maana huja muelewa....! Pole sana, ww unafanya tafsiri za Mwili na sio za kiakili na kiroho!Mheshimiwa Msigwa hasemi huo uzalishaji uongezwe vipi. Kasema yeye mwenyewe kwamba CCM hawawezi kutatua matatizo maana wao ndio "wametuweka kwenye mess hii, you guys are tired." Sasa suluhisho lake yeye ni nini?
Ameshambulia wazinzi na wanaotembea na wake za watu (shambulizi kwa Mwigulu mwenye sifa hiyo, ambae ndie alisema CHADEMA waombewe) lakini hapo hapo amekosoa majadaliano ya "khanga na ngonjera." Yale yale ya vijembe!
Kwenye theology kuna matundu kwenye hoja zake. Amesema hakuna nadharia ya maombi katika uchumi wala theology na kwamba Mtume Paulo alisema "asiyefanya kazi na asile," sio aombewe. Ni kweli, lakini Kristo Yesu alisema tuige mfano wa ndege wa angani, "ndege wao hawapandi wala hawavuni wala hawahifadhi chochote kwenye ghala lakini Baba wa Mbinguni anawalisha." Kesheni Mkiomba. Kwa hiyo hata Biblia hapa haina majibu.
Amesema serikali haisikilizi ushauri wa ma professa. Ushauri gani? Toa mfano!
Yeye ni mpinzani, hajaja hapa kuisifia serikali, ana wajibu wa kuipinga. Ok. Na CCM wana kosa gani kutokukusifia wewe, kwani CCM ni upinzani wenzako?
Asilimia 42% ya watoto wamedumaa ubongo, unadai. Sawa. Sasa hapa Waziri wa Fedha iandike vipi bajeti ili watoto wasidumae akili, atenge fungu la kulisha watoto samaki mashuleni kuwapanua akili?
Na mwisho, kama unadai CCM hawawezi kuwa solution kwa sababu ndio chanzo cha tatizo kwa nini unawasihi CCM hao hao walete suluhisho? Amedai watu wa "stretch their brains," lakini yeye hajatupanulia mjadala.
Najisikia fahari sana, nilichangia kwa kiasi kikubwa ushindi wa huyu mheshimiwa mbunge. Nilisafiri kutoka Dar kwenda kupiga kura kwa maana nilijiandikisha Iringa lkn kipindi uchaguzi unakaribia nilikuwa nililazimika kukatisha shughuli zangu ili kura yangu isiharibike. Pili nilishiriki kuhamasisha vijana kubaki kulinda kura nikitumia uzoefu wangu tulivyolinda kura za Wilfred Lwakatale mwaka 2000. Vijana walihamasika kweli, nakumbuka kijana about 38 years alisema yuko tayari kupigwa na polisi hadi kufa kwa maana ana ukimwi muda mrefu na CCm wamekula hela waathirika. Alisema hivyo kuonyesha kuwa hakuwa tayari kuona matokeo yanachakachuliwa, si unajua CCM bila kuwatia presha matokeo huwa yanabadilishwa. Mchungaji Msigwa hanifahamu na wala sitaki anijue ila popote ninapokuwa mimi huwa niko tayari kujitoa kuhakikisha anapatikaina mtu ambaye ni sahihi. Nikiwa naangalia anvyochangia najivunia kura yangu na muda wangu wa kulinda kura.
Ni kweli kabisa ana muda mchache kabisa. Sasa kama una dakika 15 tu kwa nini uzitumie kutueleza vijembe vya mtu kalala na mke wa mwingine?WEWE Kama sio MAGAMBA sijui! Muda aliopewa pale wa DK 15 kuelezea yote hayo hautoshi..
Wewe MAGAMBA lazima..Sasa Hapo kitu gani hambacho hujaelewa....Wenzio wote tumemuelewa! Pole sana kaka. ww kama sio MAGAMBA basi Baba yako au babu au Mama au BIBI ndio magamba! Chadema Oyeeee!Ni kweli kabisa ana muda mchache kabisa. Sasa kama una dakika 15 tu kwa nini uzitumie kutueleza vijembe vya mtu kalala na mke wa mwingine?
Kama una dakika 15 kwa nini usiende moja kwa moja kwenye pointi badala ya kuzitumia kueleza habari za Waraka wa Pili wa Paulo, Mtume kwa Wathesalonike? Well kama unataka theology za uchumi kwenye biblia basi Yesu Kristo alisema ndege hawafanyi kazi na wako poa tu, chakula chetu ni neno la Mungu, sio mkate! Sasa Yesu na Paulo nani mkuu?
Kwa nini uzitumie dakika 15 zako kulichekesha bunge kwa kusema 42% ya watoto wa Tanzania wamedumaa akili? Sasa Waziri wa Fedha afanye nini kuwawahi akili zingali changa, ajenge chekecheka za Kata?
Una dakika 15 then hit the point, sio kutuambia nimeongea na Professa, wanasema serikali haitaki ushauri wake, ushauri gani? Toa specifics!
"wote tumemuelewa," wote wewe na nani? Jiongelee mwenyewe! We mgeni hapa, au? Huna wherewithal ya kujibu hoja yangu zaidi ya kusema mimi ni magamba, whatever the heck that means? Mimi ni independent observer, kama umezoea straitjacket fanaticism ya kwamba lazima uwe aidha CCM au CHADEMA then huwezi ku process ninayoyasema, I get beyond CCM and CHADEMA.Wewe MAGAMBA lazima..Sasa Hapo kitu gani hambacho hujaelewa....Wenzio wote tumemuelewa!
MHH so wewe ni MCHUNGAJI au MATHEMATICIAN? Kama upo kwenye Kundi hilo basi elezea tukupatie either Mistari from Bible ambayo inaendana na alichoongea Mh. Msigwa au Tukupatie Formula ukokotoe alichoongea Mchungaji. Choose One! Chadema Oyeeee!!"wote tumemuelewa," wote wewe na nani? Jiongelee mwenyewe! We mgeni hapa, au? Huna wherewithal ya kujibu hoja yangu zaidi ya kusema mimi ni magamba, whatever the heck that means? Mimi ni independent observer, kama umezoea straitjacket fanaticism ya kwamba lazima uwe aidha CCM au CHADEMA then huwezi ku process ninayoyasema, I get beyond CCM and CHADEMA.
Jamaa alipigili msumari! Very nice Presentation, Nikipata muda nitaiwekea Subtitle za Kiingereza, Na sehemu alizo Ongea Kiingereza nitaweka Kiswahili,Ili hata siku mzungu akiiona hii video ajue Huku kuna watu wanaelewa things sema System ndio mbovu,Ujue nje ya TZA watu wanafikiria sisi ni mbumbumbu kwa haya yanayofanywa na CCM!So wajiona vitu kama hivi watujua kuwa tupo fit ila System ndio MBOVU.Asante sana dizdap,hiki kipande kilinipita nimerudia mara tano kusikiliza kwa makini. Very intelligent thinking and presentation o ideas from Msigwa,the sad thing is CCM members of parliament and the government leaders have no ears