Angalia kwa makini vijana hawa.....

Mdau

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,789
470
Ati,hivi hawa vijana walikua wanamaanisha nini???

attachment.php



12121.jpg
 
Nadhani umefika wakati sasa mtu anapotoa malalamiko yake akatumia lugha fasaha na inayoeleweka kwa watu wote, Kutumia maneno kama "tatizo ni Serikali ya Kishkaji ya Kikwete inaweza kutafsirika tofauti na ulivyokusudia na matokeo yake hata uliotegemea wakuunge mkono wakakutupa kwa sababu tu hawajakuelewa.

Nawasilisha.
 
Nakereka nikiona maandamano ya vyuo vikuu. Mara wawalalamikie, mara wawasifie viongozi, unafiki mtupu
 
Nakereka nikiona maandamano ya vyuo vikuu. Mara wawalalamikie, mara wawasifie viongozi, unafiki mtupu

tatizo wengi wa wasomi wa vyuo wameingia vyuoni kwa uwezo mkubwa wa kukariri
na uwezo wa kuwa wadadisi na wafikilivu, waelewa wenye akili ya kujitegemea kuwaza
saa ingine hapo walikaririshwa tu wafanye hivyo
hiyo imepelekea hata wawapo kwenye mambo nyeti kama hayo hujikuta kuwa
wanalalamikia wasichokijua, na wanakijua wasichokilalamikia
wanavaa wakati wa kuvua, na wanavua wakati wa kuvaa
 
Lakini tatizo hapo ni nini wakuu, unajua hawa tunao waita wasomi na tuna wakosoa sana utadhani wengi wetu hatujapitia huko. nina hakika asilimia kubwa hu jf tumepitia huko huko, hivyo wapo wanaofuata mkondo kumuunga jk na wapo wanao jua kusimamia na kudai haki zao
 
mimi nadhani msomi ndiye mtu wa kwanzza anayepaswa kujitambua....tatizo hapa nchini kwetu,wasomi wengi wanajitambua "negatively",badala ya kufanya mema na kusaidia wananchi,waningia kwenye mkumbo wa maisha ya kujilimbikizia mali, whether kwenye siasa au mambo mengine..
 
vijana hawa walikua Diamond Jubilee tena...
 
wasomi wetu waoga wa kusema ukweli,na hii imetokana na elimu yetu ya kusomea vyeti tu na si elimu ya kujiwezesha kuwa mwenyewe katika maisha.
 
Nakereka nikiona maandamano ya vyuo vikuu. Mara wawalalamikie, mara wawasifie viongozi, unafiki mtupu

Mkuu sio wote wanaisapoti serikali. Kama ilivyo kwa jamii yeyote, wanafiki hawakosekani. CCM inawatumia wanafunzi wanafiki wenye njaa ya mkate au sifa kuwasaliti wenzao. Hawa ndo wanaojikomba kwa viongozi na kubinafsisha elimu yao. Haihitaji hata certificate ya VETA kugundua kuwa CCM hakuna cha maana wanachokifanya nchi hii hivyo ukiona mwenye degree/msomi anaisifia na hata kumchangia mgombea wake ujue kuna ..........
 
mimi nadhani msomi ndiye mtu wa kwanzza anayepaswa kujitambua....tatizo hapa nchini kwetu,wasomi wengi wanajitambua "negatively",badala ya kufanya mema na kusaidia wananchi,waningia kwenye mkumbo wa maisha ya kujilimbikizia mali, whether kwenye siasa au mambo mengine..

Wasomi wetu hawajitambui kama ulivyosema thats why hata wahadhiri badala ya kukata nyanga wanakimbilia siasa. Jamaa wameonyesha kero zao lakini bado hawajatoa demo ya kutosha ili kufikisha ujumbe wao. Maana kubeba bango hakutoshi na matendo yanatakiwa. Shida za watz ndizo zinaleta undumilakuwili wa watu. Huku wanataka na huku wanataka. Chagua chema kwa tz bora.
 
Mtatiro atawamiss sana jimbo la UBUNGO....
 
tatizo wengi wa wasomi wa vyuo wameingia vyuoni kwa uwezo mkubwa wa kukariri
na uwezo wa kuwa wadadisi na wafikilivu, waelewa wenye akili ya kujitegemea kuwaza
saa ingine hapo walikaririshwa tu wafanye hivyo
hiyo imepelekea hata wawapo kwenye mambo nyeti kama hayo hujikuta kuwa
wanalalamikia wasichokijua, na wanakijua wasichokilalamikia
wanavaa wakati wa kuvua, na wanavua wakati wa kuvaa

Mkuu Anyisile hauko sahihi sana kwa ulichoandika. baada ya kuangalia hiyo picha ilikupasa urudishe kumbukumbu zako nyuma na kujiuliza; Picha hiyo ilipigwa lini? Ilipigwa chuo gani? Nini lilikuwa suala la msingi mpaka hao wakaandamana? Maana ya ujumbe uliopo hapo ndani ya mabango? Nini yalikuwa matokeo ya ujumbe wa bango hilo na maandamano/mgomo wao?

Usikurupuke tu kudharau wakati unaonyesha ni bingwa wa kusahau( unamatatizo makubwa). Nani kakwambia kuwa walikaririshwa wafanye hivyo? Rudia kuyasoma mabango yote mawili, halafu tumia akili yako kuyatafsiri maudhui yake

Labda kukukumbusha wewe nawale wengine wanaotafsiri vibaya ni kuwa picha hiyo ilipigwa pale UDSM-Main campus wanachuo walikuwa wakilalamikia kutopewa pesa zao toka Bodi ya Mikopo.

Hawa wasomi walitumia fikra zao kiusahihi katika kutafuta chanzo cha matatizo waliyonayo. Japo kwa nje tatizo laonekana ni Bodi ya Mikopo, lakini kiuhalisia tatizo la msingi lilikuwa serikali ambayo watendaji wake walichaguliwa ama kupewa vyeo kwakuwa ni marafiki wa Jakaya Kikwete au walimsaidia kuingia madarakani (connect na yule mama aliyekuwa anahusika na kashfa za EPA akapelekwa kwenye Bodi hiyo).

Japo walisalitiwa na yule Raisi wa TAHLISO (ambaye ni kada CCM) na kisha kufukuzwa, ukweli umebaki vilevile hadi leo ya kwamba "TANZANIA TUMEPATA MATATIZO MAKUBWA SANA KATIKA AWAMU HII YA NNE HATA WENGINE KUSHINDWA KUWAJIBISHWA JAPO NI WEZI, KWASABABU TU NI WASHIKAJI (MARAFIKI,VIBARAKA,etc) wa KIKWETE".

Need I say more?

Naomba tujiulize wanafunzi hao walikuwa waongo?
 
Nakereka nikiona maandamano ya vyuo vikuu. Mara wawalalamikie, mara wawasifie viongozi, unafiki mtupu

Pengine huelewi changamoto zinawapata wanafunzi wa vyuo vikuu! Wakati fulani mwaka jana, nilianza kuona idadi ya wanafunzi wanakuja kuniomba msaada wa fedha ya chakula inaongezeka, nikawa nimewauliza kulikoni, ndio nikagundua hawakuwa wamewekewa pesa yao ya mkopo kwa muda mrefu. Baada ya wiki tatu, wanafunzi waliandamana na wiki moja baadae waliwekewa hela na kulaumiwa mno.

Wanafunzi wanaotaka mikoani wasio na ndugu Dar wanateseka sana mikopo inapocheleweshwa, na hata wangekuwa 'watakatifu' kiasi gani, inawabidi wajiunge na mgomo kama upo.

Uongozi wa vyuo nao unawatesa na kuwanyanyasa wanafunzi kwa namna ambayo wale walioko nje ya hivi vyuo ni vigumu kuelewa. Nafahamu nyakati wanafunzi wamevurujiwa usajili wao kutokana na kumbu kumbu hovyo za utawala. Siku chache kabla ya mitihani wanaambiwa hawawezi kufanya mitihani kwani hawajalipa. Kupata ufafanuzi ulichukuwa muda na alnusura ilete kutokuelewana.

Lakini yote tisa, jamani hawa ni wanafunzi wa vyuo vikuu, they are supposed to be mature enough and thinkers at that to the extent they have an opinion about what is happening in their own environment, if this opinion is not respected, they may take to voting, going for a strike. Hivi vimoto moto vya matatizo ya vyuo vikuu ndio yamezalisha midahalo ambayo iliwajenga baadhi ya wanafunzi hao na kuonyesha vipaji ambavyo leo hii ndio viongozi wa taifa, (ingawaje wengine wanakuja kukumbatia ufisadi)
 
Mkuu Anyisile hauko sahihi sana kwa ulichoandika. baada ya kuangalia hiyo picha ilikupasa urudishe kumbukumbu zako nyuma na kujiuliza; Picha hiyo ilipigwa lini? Ilipigwa chuo gani? Nini lilikuwa suala la msingi mpaka hao wakaandamana? Maana ya ujumbe uliopo hapo ndani ya mabango? Nini yalikuwa matokeo ya ujumbe wa bango hilo na maandamano/mgomo wao?

Usikurupuke tu kudharau wakati unaonyesha ni bingwa wa kusahau( unamatatizo makubwa). Nani kakwambia kuwa walikaririshwa wafanye hivyo? Rudia kuyasoma mabango yote mawili, halafu tumia akili yako kuyatafsiri maudhui yake

Labda kukukumbusha wewe nawale wengine wanaotafsiri vibaya ni kuwa picha hiyo ilipigwa pale UDSM-Main campus wanachuo walikuwa wakilalamikia kutopewa pesa zao toka Bodi ya Mikopo.

Hawa wasomi walitumia fikra zao kiusahihi katika kutafuta chanzo cha matatizo waliyonayo. Japo kwa nje tatizo laonekana ni Bodi ya Mikopo, lakini kiuhalisia tatizo la msingi lilikuwa serikali ambayo watendaji wake walichaguliwa ama kupewa vyeo kwakuwa ni marafiki wa Jakaya Kikwete au walimsaidia kuingia madarakani (connect na yule mama aliyekuwa anahusika na kashfa za EPA akapelekwa kwenye Bodi hiyo).

Japo walisalitiwa na yule Raisi wa TAHLISO (ambaye ni kada CCM) na kisha kufukuzwa, ukweli umebaki vilevile hadi leo ya kwamba "TANZANIA TUMEPATA MATATIZO MAKUBWA SANA KATIKA AWAMU HII YA NNE HATA WENGINE KUSHINDWA KUWAJIBISHWA JAPO NI WEZI, KWASABABU TU NI WASHIKAJI (MARAFIKI,VIBARAKA,etc) wa KIKWETE".

Need I say more?

Naomba tujiulize wanafunzi hao walikuwa waongo?


ilikua ni 2007...
 
Mkuu Anyisile hauko sahihi sana kwa ulichoandika. baada ya kuangalia hiyo picha ilikupasa urudishe kumbukumbu zako nyuma na kujiuliza; Picha hiyo ilipigwa lini? Ilipigwa chuo gani? Nini lilikuwa suala la msingi mpaka hao wakaandamana? Maana ya ujumbe uliopo hapo ndani ya mabango? Nini yalikuwa matokeo ya ujumbe wa bango hilo na maandamano/mgomo wao?

Usikurupuke tu kudharau wakati unaonyesha ni bingwa wa kusahau( unamatatizo makubwa). Nani kakwambia kuwa walikaririshwa wafanye hivyo? Rudia kuyasoma mabango yote mawili, halafu tumia akili yako kuyatafsiri maudhui yake

Labda kukukumbusha wewe nawale wengine wanaotafsiri vibaya ni kuwa picha hiyo ilipigwa pale UDSM-Main campus wanachuo walikuwa wakilalamikia kutopewa pesa zao toka Bodi ya Mikopo.

Hawa wasomi walitumia fikra zao kiusahihi katika kutafuta chanzo cha matatizo waliyonayo. Japo kwa nje tatizo laonekana ni Bodi ya Mikopo, lakini kiuhalisia tatizo la msingi lilikuwa serikali ambayo watendaji wake walichaguliwa ama kupewa vyeo kwakuwa ni marafiki wa Jakaya Kikwete au walimsaidia kuingia madarakani (connect na yule mama aliyekuwa anahusika na kashfa za EPA akapelekwa kwenye Bodi hiyo).

Japo walisalitiwa na yule Raisi wa TAHLISO (ambaye ni kada CCM) na kisha kufukuzwa, ukweli umebaki vilevile hadi leo ya kwamba "TANZANIA TUMEPATA MATATIZO MAKUBWA SANA KATIKA AWAMU HII YA NNE HATA WENGINE KUSHINDWA KUWAJIBISHWA JAPO NI WEZI, KWASABABU TU NI WASHIKAJI (MARAFIKI,VIBARAKA,etc) wa KIKWETE".

Need I say more?

Naomba tujiulize wanafunzi hao walikuwa waongo?
nashukuru san amkuu lakini nadhani huo ni ukweli japo wewe umeona kuwa nimeangalia sana upande mmoja na kukurupuka kutoa mawazo yangu, pengine siwezijua wewe uko upande gani katika hilo uwazi uko pale pale kuwa wasomi wa tanzania ni wababaishaji tu, hilo hatuwezi kulivika nguo lionekane kama unavyotaka, unafiki wetu wa kutaka kuvuna wakati hatujapanda, na kutaka kupanda ambacho hatutavuna ndiyo ulikutawala wewe katika mawazo yako na kuona wakati wasomi walizalisha lililo jema katika nchi hii,
ni miongoni mwa wasomi wanaotete ughafidhuna, ufirauni na umafia wa serikali ya kinduli ya ccm pamoja na uozo wake ambao hata mtoto wa darasa la saba hataki kuuona vipi kwako wewe na mimi?
tafakali!!! wasomi wetu ni mamluki na wanafiki sana
 
Jamani vijana hawa walikua sahihi, JK hawezi kulivua wa kujivua GAMBA!!!!!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom