Uncle Jei Jei
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,684
- 2,157
Mbarikiwe wote Wana JF! Leo nakuja kwenu kuomba ushauri, natumaini kwa kutumia uzoefu,ujuzi na Upendo mtanipa suruhisho! Nimienzi kama mitatu hivi tulitofautiana na msichana niliyetegemea angekuja kuwa mama wa watoto wangu siku za usoni! Tulidumu takribani miaka mitano kwani tulianza mahusiano tukiwa bado A'level! Kisa cha kutofautiana,mara nyingi nilifuma chatings za mahaba na mwanaume mwingine! Lakin pamoja na hayo hakuacha kuniheshimu! Kilichoniumiza mpaka tukanuniana ni siku moja kabla ya kuachana nilimuomba tutoke out akakubali,lakini cha ajabu mda ulipofika hakupokea simu zangu wala kujibu sms zangu mpaka ilipofika jioni akaniambia alikuwa na mama yake...lakini baada ya kufanya uchunguzi jioni hiyo hiyo(kwani baadae tulionana) niligumdua alitoka na huyo jamaa yake. Hii ni kutokana na sms za siku hiyo tangu wanapanga pa kukutania na msg aliyomshukuru kwa "campani"ya siku hiyo!! Nilipomuuliza hizo sms ni za nani na kwanini aliamua kunidanganya,hakuwa na usemi zaidi ya kutetemeka(nilichukua simu yake ghafla). Mpaka leo anasema nilimsingizia na hataki tuliongelee hilo ila ananilaum tu kuwa nimemuacha kwa sababu nimepata mwingine! Bado nampenda na anaonyesha nia ya kuwa na mimi, ila nahofia atakosa uaminifu ndani ya ndoa! MSAADA WENU PLZ..!