eRRy
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 1,125
- 204
Source:LIVE - Global PublishersDokta Said wa zahanati moja iliyopo Magomeni, Dar es Salaam, amenaswa akimtoa mimba mwanamuziki wa kundi moja la Muziki wa Taarab, Mwanaidi Madani (kama inavyoonekana pichani).
The Biggest IQ, Ijumaa Wikienda liliendesha uchunguzi wa kisayansi wiki iliyopita na kumnasa Dk. Said akimshughulikia Mwanaidi katika kukiua kitoto kisicho na hatia tumboni.
Mwanamuziki huyo alipozungumza na gazeti hili Ijumaa iliyopita alijibu: Mimi nilikwenda kwa dokta kusafisha tumbo, lakini polisi walinikamata wakadai nimetoa mimba.
Vyanzo vyetu vilitonya kuwa tukio la Dk. Said kumtoa mimba Mwanaidi si la mara ya kwanza, kwani amekubuhu kwa mchezo huo.
Haa, huyo dokta mbona ndiyo mchezo wake? Alisema mama mmoja aliyekuwa ameshika kiuno nje ya zahanati hiyo.
:A S check_03: