Anakataa kuzaa, eti mpaka baada ya kumaliza Masters!

Yo Yo mi naona huyu binti hampendi jamaa ako hii ni zuga tu unajua kama shori hakupendi atakutafutia visababu vidogo vidogo ili ushindwe mwambie jamaa apige chini tu mashori wapo kibao.
 
Yo yo acha kuwa na mtazamo finyu! suala la huyo dada kusoma ni suala la mtu binafsi na future yake (ni maisha ya mtu hapa unazungumzia) na kati ya vitu ambavyo mimi binafsi sipendi kuingiliwa ni pamoja na maisha yangu binafsi, to me my first priority is me & myself! siwezi kuruhusu eti mchumba alazimishe kuharibu mipangilio yangu eti kisa mtoto, wakati majority hata si waaminifu, wewe utakatisha mambo yako kisa mimba na mtoto, yeye huku akiwa kakutia mimba still anaendelea na mambo yake kwani habebi tumbo wala hanyonyeshi, yeye anapata PhD, wewe ndio unaanza kurudi kwenye masters, then kesho aseme hukusoma kama yeye, mara akuletee watoto wa nje. Mie ningemuona hy dada namwambie akomae na msimamo wake, huyo mume akiona anchelewa mbona visichana vya x-std 7 ambavyo havina wazo laolote la kuendelea hata na kozi ya ushonaji viko kibao tu mtaani, atafute kamoja aoe ili azae hata 10 akitaka! halafu mke wa ndoa usijali ana mvuto gani ukitaka mivuta tafuta machangu hao alwayz wana mvuto! mambo ya kuangalia sura na shepu hata kama mke mwenyewe mzigo yamepitwa na wakati kaka! get up

He he he..

Ahh nyie mnaongeaga tu..Hivi wewe umeona wapi watu wanaaihirisha ndoa kwa miaka 4? Miaka 4 ni mingi sana aisee na kama ni katoto katakuwa kanaenda nursery school tena kanaweza hata kujua kusoma na kuandika...! hi hi hi

Jamaa kutaka mtoto inamaanisha jamaa ndo amefika Kigoma mwisho wa reli, anataka kuanzisha ka-familia na yeye aitwe baba..na mamsapu pembeni ..ila mdada ndio hivyo..stimu hazipo..anachelea kusema ukweli. Suala la kusema mdada ajitangulize maono yake ndio dalili ya kutompenda msela..hakuna kingine..kama unampenda..shori anayemzimia mtu hawezi kurusha hilo suala kwa miaka 4..huo utakuwa ujuha flani ivi..
 
kwani jamani...inaruhusiwa kuzaa na mchumba wako au mke wako??....nadhani jamaa anapanick upuuzi tuu...wewe huwezi kuzaa na mchumba...anatakiwa azae na mkewe...hapo naona shorty yupo smart...ila kama ungeniambia short hataki kuolewa na kuwa mke kabla hajachukuwa masterz then ningesema mshkaji atafute demu mwingine aoe kisha azae naye

kingine ambacho najaribu kujiuliza...kwani mwanaume ukiwa na 30yrs ndio mwisho wa kuzaa?...au anataka kutuambia kuwa right time ya mwanaume kuzaa ni 30yrs?....

nachokiona hapa ni kuwa dada yetu amakuwa smart kuliko mshkaji ambaye hata mie naona anataka kumzalisha dada yetu bila ndoa kisha aoe mtu mwingine then dada yetu awe na mtoto asiye na malezi ya pande mbili......PATAMU HAPO.

USHAURI.....kijana kama unampenda binti...toa mahari, funga ndoa...then watoto na mipango mingine itakuwa ndani ya ndoa yenu...mkitaka kuzaa watoto 1, 2, 10, 20 etc na mkitaka kuzaa kabla ya masters, au hata baada ya kuwa mawaziri....yooote ni maamuzi yenu wanandoa.....usipende shortcut za mambo serious na maisha ya wenzako,....NI MTAZAMO TU
 
kwani jamani...inaruhusiwa kuzaa na mchumba wako au mke wako??....nadhani jamaa anapanick upuuzi tuu...wewe huwezi kuzaa na mchumba...anatakiwa azae na mkewe...hapo naona shorty yupo smart...ila kama ungeniambia short hataki kuolewa na kuwa mke kabla hajachukuwa masterz then ningesema mshkaji atafute demu mwingine aoe kisha azae naye

kingine ambacho najaribu kujiuliza...kwani mwanaume ukiwa na 30yrs ndio mwisho wa kuzaa?...au anataka kutuambia kuwa right time ya mwanaume kuzaa ni 30yrs?....

nachokiona hapa ni kuwa dada yetu amakuwa smart kuliko mshkaji ambaye hata mie naona anataka kumzalisha dada yetu bila ndoa kisha aoe mtu mwingine then dada yetu awe na mtoto asiye na malezi ya pande mbili......PATAMU HAPO.

USHAURI.....kijana kama unampenda binti...toa mahari, funga ndoa...then watoto na mipango mingine itakuwa ndani ya ndoa yenu...mkitaka kuzaa watoto 1, 2, 10, 20 etc na mkitaka kuzaa kabla ya masters, au hata baada ya kuwa mawaziri....yooote ni maamuzi yenu wanandoa.....usipende shortcut za mambo serious na maisha ya wenzako,....NI MTAZAMO TU

Kama huyo dada amekataa kuzaa inamaana chances are high kuwa amekataa vyote
 
kwani uyo jamaa ameambiwa akifikisha miaka 35 hataweza kuzaa tena? angekuwa mwanamke ningeelewa.

Kama hawawezi kuelewana kwa suala dogo kama hilo, je wakiingia kwenye ndoa itakuwaje

By the way wanatakaje mtoto na huku hawajaoana?

Anaweza kuzaa,naona huyu ndugu anaehitaji mtoto amekaa akafikiria musktaka bali wa maisha yake akaona siku zina songea na umri wa kuishi nao unapungua,so naona ameona asiondoke kwenye hii dunia pasipo kuacha mtoto.

Na mshauri jamaa atafute mwanamke ambae atakuwa ni mke wake then ndio wazaae nae.Unajua kuna madhara mengi sana kuzaa mtoto nje ya ndoa mwishowe mtoto hanakosa malezi ya pande zote mbili.
 
Wangapi wanazaa wakiwa college jamani na wanaendelea na kitabu kama kawa? Huyu binti anatafuta njia ya kumkataa jamaa ndo maana kampa miaka 4 akivumilia hiyo atawepewa tena 6 hehehehe
 
Mambo ya kuoana watu mumepishana miaka 10 sijui yamesha pitwa na wakati. Tell your bro to wait or move on.

nakubaliana nawe kwa mengine lakini hili sio. Miaka sio issue saana. Yaani mtu ana 35 akioa wa 25 imepitwa na wakati? Mkiwa wate 30s utaona jinsi atakavyokuwa anazeeka faster kabla yako then unaanza za huku na kule.

Ungesema reasonable age difference.
 
Wangapi wanazaa wakiwa college jamani na wanaendelea na kitabu kama kawa? Huyu binti anatafuta njia ya kumkataa jamaa ndo maana kampa miaka 4 akivumilia hiyo atawepewa tena 6 hehehehe

na huyo bwana nae asiwe king'ang'anizi lazima usomi wake umsaidie pia kusoma alama za nyakati, kama binti ni myeyushaji atamjua tu si lazima apige ramli, na kama nia ni kusoma tu ila wanapendana atamvumilia tu, kwani upendo wa kweli huvumilia!
 
kwani uyo jamaa ameambiwa akifikisha miaka 35 hataweza kuzaa tena? angekuwa mwanamke ningeelewa.

Kama hawawezi kuelewana kwa suala dogo kama hilo, je wakiingia kwenye ndoa itakuwaje

By the way wanatakaje mtoto na huku hawajaoana?

Ah mie nna la kusema hapa? Ntalipataje wakati weye ami ushamaliza yooote?

Very well said, broda!
 
Ajaribu kumwambia kwanza anataka kumuoa then aone kama bibie atamwambia amsubiri hadi amalize Masters! Au kabila lao hao hawana kitu kinachoitwa ndoa?
 
nakubaliana nawe kwa mengine lakini hili sio. Miaka sio issue saana. Yaani mtu ana 35 akioa wa 25 imepitwa na wakati? Mkiwa wate 30s utaona jinsi atakavyokuwa anazeeka faster kabla yako then unaanza za huku na kule.

Ungesema reasonable age difference.

Mkuu age ndiyo is not a matter. Ila ninacho sema mimi unaangalia on a person to person basis. Mkuu hapa hauoni jamaa kaona anachelewa but the girl yeye anaona bado muda anao na anataka kusoma? Kama anaona anachelewa atatute binti ambae kamaliza mambo yote ya shule na pia kama yupo tayari kumsubiria amsubirie. SIkumaanisha mkuu kuwa mkipishana miaka kumi msioane ila ni obvious hapa kuwa jamaa anaona muda kwake umeenda na binti kwake anaona time is on her side.
 
Jamaa yako inaonesha anakuwa mgumu sana kusoma alama za nyakati..Kwa kifupi huyo shori hamzimii msela kiivo na ndio maana jamaa anapomletea mambo ya kuzaa sijui kutotoa..anamchek kidaini huku moyoni akijisemea ' huyu vipi!!? '

Mi nawajua sana mademu mazee, akiwa hakuzimii na wala haoni future na wewe ataleta gunia la visingizio..Kwa kifupi shori ameegesha tu kwa mshikaji kujikinga mvua na mvua ikiisha anatambaa..
100% nakuunga mkono,miguu,kichwa na kiwiliwili,huyo demu ameshamuona jamaa mzigo wa kinyesi haubebeki.Jamaa ajue kuwa hiyo master ndio utenganisho wao,aaamini aasiaaamini ukweli ndio huo.
 
kwani jamani...inaruhusiwa kuzaa na mchumba wako au mke wako??....nadhani jamaa anapanick upuuzi tuu...wewe huwezi kuzaa na mchumba...anatakiwa azae na mkewe...hapo naona shorty yupo smart...ila kama ungeniambia short hataki kuolewa na kuwa mke kabla hajachukuwa masterz then ningesema mshkaji atafute demu mwingine aoe kisha azae naye

kingine ambacho najaribu kujiuliza...kwani mwanaume ukiwa na 30yrs ndio mwisho wa kuzaa?...au anataka kutuambia kuwa right time ya mwanaume kuzaa ni 30yrs?....

nachokiona hapa ni kuwa dada yetu amakuwa smart kuliko mshkaji ambaye hata mie naona anataka kumzalisha dada yetu bila ndoa kisha aoe mtu mwingine then dada yetu awe na mtoto asiye na malezi ya pande mbili......PATAMU HAPO.

USHAURI.....kijana kama unampenda binti...toa mahari, funga ndoa...then watoto na mipango mingine itakuwa ndani ya ndoa yenu...mkitaka kuzaa watoto 1, 2, 10, 20 etc na mkitaka kuzaa kabla ya masters, au hata baada ya kuwa mawaziri....yooote ni maamuzi yenu wanandoa.....usipende shortcut za mambo serious na maisha ya wenzako,....NI MTAZAMO TU
Naomba nenda uchagani ukaone wapenzi wengi wanazaa wakiwa wachumba na kufunga ndoa wakiwa na wajukuu japo maadili ya dini hayaruhusu,tembea uone.
 
Pengine binti anahofia kutokuolewa akizaa kabla ya ndoa. Mwambie rafiki yako amwoe huyo binti kwanza na atakubali tu kuzaa akiwa kwenye ndoa kuliko kuzaa akiwa kwenye uchumba.
 
Heri kutofautiana mapema kuliko kubahatisha relationship. Yanini ulazimishe lifestyle? Kakuona sio type yake,nawe tafuta type yako uishi kwa furaha.
 
mkuu ni mipangilio ya jamaa akifikisha umri fulani aachane na kuzaa.....imagine unazaa una 40 huyo mtoto atakuita baba au babu? pia kumbuka life expactancy ya mtanzania ni miaka 37 kama sijakosea....


Mkuu kulingana na UN life expectancy kwa male ni 51 na female ni 54 (kwa TZ) so hapo ni too much exaggeration,

suala lilikuwa ndoa+mtoto.....
kama ni hivyo na bado binti akakataa, basi hakuna kitu apo, jamaa atambae tu
 
Mimi nimemshauri wakati akimsubiria bibie amalize masters yake na yeye anahitaji mtoto basi atafute wa kumzalia na wakubaliane na bibie......maana naona jamaa ananyanyaswa...


Sina uhakika kama nimesoma vizuri.....si ni wachumba?watazaaje sasa!Wasubiri wafunge ndoa ndo wazae.Si ndo taratibu au?
Sorry kama siendi na wakati !
 
Kama huyo dada amekataa kuzaa inamaana chances are high kuwa amekataa vyote

Huyu binti anatengeneza mazingira ya kumkatisha tamaa jamaa na huyu binti tayari katika kichwa chake anayo plan yake na anajua wazi jamaa hawezi vumilia kwa 4yrs na sasa jamaa ana 30 lazima atakata tamaa ni bora amweke wazi na jamaa awe na msimamo.
 
Siku atakapoambiwa nasafiri kikazi kwenda mkoa wiki mbili na yeye akae na mtoto wa miezi mitatu atafanyaje? Huyo demu yuko sahihi ila jamaa yetu ndo kimeo. Ndoa za kupulizia zilikuwa zamani, mwambie jamaa awe makini,atavurugwa na huyo demu bure.
 
kwani jamani...inaruhusiwa kuzaa na mchumba wako au mke wako??....nadhani jamaa anapanick upuuzi tuu...wewe huwezi kuzaa na mchumba...anatakiwa azae na mkewe...hapo naona shorty yupo smart...ila kama ungeniambia short hataki kuolewa na kuwa mke kabla hajachukuwa masterz then ningesema mshkaji atafute demu mwingine aoe kisha azae naye
mkuu hukunisoma.....nilisema jamaa anataka ndoa+kuzaa....upo? kitu ambaco yeye anataka ni wafunge ndoa then wazae sasa kwa 4yrs muhanga anaona kama ni mateso kisa masters......

kingine ambacho najaribu kujiuliza...kwani mwanaume ukiwa na 30yrs ndio mwisho wa kuzaa?...au anataka kutuambia kuwa right time ya mwanaume kuzaa ni 30yrs?....
mkuu nani ana mpango wa kuitwa babu na watoto wake? miaka hii maisha mafupi......
 
Back
Top Bottom