Vasco Dagama
Member
- Jan 18, 2012
- 52
- 10
Habari zenu.
Nina rafiki yangu (mfanyakazi mwenzangu) yamemfika yakumfika.
Amenisimulia visa vingi na mambo mengi ambayo nimemwonea huruma.
Ni msichana wa umri wa miaka 25, alikuwa na boyfriend wake chuo akazaa nae na akamkimbia
akalea mtoto peke yake......ni story ndefu ngoja niifupishe...............
akakutana na mwanaume wa mtu japokuwa yule mwanaume anasema alikwenda kwake ili kuondoa stress
kuwa mkewe (hawajafunga ndoa) anavyosema ana matatizo chungu mbovu..........................
msichana ana stress za kulea mtoto na kuachwa na mwanaume na akapewa mapenzi moto moto
mpaka akafikia kumtukana yule mwanamke mwenzie bila kujali na akaona kaolewa kabisa maana mwanaume alikuwa
anasema kasafiri kumbe yuko kwake.
Kisa chenyewe ni juzi wakiwa wote kwenye matembezi jamaa kaanguka ghafla na kupelekwa hospitali madaktari
wakampima kila kitu wakagundua ni HIV+ na msichana yuko hapo...............amekuja kwangu analia anaomba ushauri
afanya nini sasa kwa wakati huu??!! Nimekosa cha kumwambia
Najua hapa ni kisima cha ushauri naombeni mnisaidie ushauri........kupima kasema atakwenda kupima lakini anasema anaona anakwenda kuconfirm tu maana anajua aliyofanya na huyo jamaa ni mengi sana.
Asante
Nina rafiki yangu (mfanyakazi mwenzangu) yamemfika yakumfika.
Amenisimulia visa vingi na mambo mengi ambayo nimemwonea huruma.
Ni msichana wa umri wa miaka 25, alikuwa na boyfriend wake chuo akazaa nae na akamkimbia
akalea mtoto peke yake......ni story ndefu ngoja niifupishe...............
akakutana na mwanaume wa mtu japokuwa yule mwanaume anasema alikwenda kwake ili kuondoa stress
kuwa mkewe (hawajafunga ndoa) anavyosema ana matatizo chungu mbovu..........................
msichana ana stress za kulea mtoto na kuachwa na mwanaume na akapewa mapenzi moto moto
mpaka akafikia kumtukana yule mwanamke mwenzie bila kujali na akaona kaolewa kabisa maana mwanaume alikuwa
anasema kasafiri kumbe yuko kwake.
Kisa chenyewe ni juzi wakiwa wote kwenye matembezi jamaa kaanguka ghafla na kupelekwa hospitali madaktari
wakampima kila kitu wakagundua ni HIV+ na msichana yuko hapo...............amekuja kwangu analia anaomba ushauri
afanya nini sasa kwa wakati huu??!! Nimekosa cha kumwambia
Najua hapa ni kisima cha ushauri naombeni mnisaidie ushauri........kupima kasema atakwenda kupima lakini anasema anaona anakwenda kuconfirm tu maana anajua aliyofanya na huyo jamaa ni mengi sana.
Asante