Ni kijana mdogo tu ambae kimsingi anahitaji msaada kwa wenye uwezo wa kusaidia. Mie, nimejaribu hadi pale nilipoweza na kinachohitajika kwa sasa ni yeyote mwenye uwezo na moyo kusaidia pale ambapo nae ataweza. Kimsingi, yeye anasoma kwenye moja ya hivi vyuo vilivyopo DSM akisoma Certificate ni Tourism Management. Kwa bahati mbaya, amesimamishwa masomo kutokana na kukosa ada kwani tangu aanze, amelipa shilingi laki moja tu. Hivyo basi waungwana na wandugu; kwa yeyote atakayeweza kumsaidia apate angalau hiki kibarua cha uandikishaji wa sensa; basi amsaidie ili chochote kitu atakachopata akapeleke huko chuoni. Kutokana na elimu yake (kidato cha nne) bila shaka ana sifa za kuwa karani katika zoezi hili.
Kwavile hana simu; basi ningependa kuweka hapa namba ya kaka yake ambayo ni 0716 67 09 79.
Kwavile hana simu; basi ningependa kuweka hapa namba ya kaka yake ambayo ni 0716 67 09 79.