Pape
JF-Expert Member
- Dec 11, 2008
- 5,488
- 79
wana JF,
Kuna jirani yangu ambaye alikuwa anauhusiano wa kimapenzi na mke wa mtu. Ameniambia kwamba mwanamama huyo ndiye aliye mshawishi wawili hao wawe wapenzi bila kujali mumewe (ndoa yake). Baada ya miezi 5 mwanamama huyo alipata ujauzito na alipojifungua mtoto alifanana kabisa na rafiki yangu. Mume wa mwanamke wala hakuhoji!!
Baada ya muda wapenzi hao waliendelea na kamchezo! Mama huyo akapata ujauzito tena na mtoto wa pili alifanana na huyu rafiki yangu! Huyu rafiki yangu yeye aliogopa na kuamua kuhama mji kwani alihofia usalama wake kwa mume wa yule mwanamama.
Alikaa mkoa wa jirani takribani miaka mi tano! Rafiki yangu huyo baada ya muda alirejea tena jijini Arusha na kukuta katika kipindi chote hicho yule mwanamama na mumewe hawajapata mtoto mwingine.
Yule mwanamama alianza tena tabia yake kwa kumhakikishia kwamba mumewe hana tatizo na hawezi jua kuhusu uhusiano wao! Punde yule mama akashika ujauzito! Alipojifungua mtoto wa tatu alifanana sana na huyu rafiki yangu.
Ndipo huyu rafiki yangu aliamua kufuatilia kwakaribu ili ajue undani zaidi na ndipo alipogungua kwamba mwanamama huyo na mumewe walikuwa wamepanga mchezo wote kwani jogoo la mumewe 'haliwiki'
Sasa wana JF, huyu kijana hajaoa lakini anauhakika wa 100% kwamba watoto wale watatu ni wake...
Je, anayohaki ya kuwadai watoto hao kuwa ni wa kwake?
Je, afanyeje ili aweze kutendewa haki?
Kuna jirani yangu ambaye alikuwa anauhusiano wa kimapenzi na mke wa mtu. Ameniambia kwamba mwanamama huyo ndiye aliye mshawishi wawili hao wawe wapenzi bila kujali mumewe (ndoa yake). Baada ya miezi 5 mwanamama huyo alipata ujauzito na alipojifungua mtoto alifanana kabisa na rafiki yangu. Mume wa mwanamke wala hakuhoji!!
Baada ya muda wapenzi hao waliendelea na kamchezo! Mama huyo akapata ujauzito tena na mtoto wa pili alifanana na huyu rafiki yangu! Huyu rafiki yangu yeye aliogopa na kuamua kuhama mji kwani alihofia usalama wake kwa mume wa yule mwanamama.
Alikaa mkoa wa jirani takribani miaka mi tano! Rafiki yangu huyo baada ya muda alirejea tena jijini Arusha na kukuta katika kipindi chote hicho yule mwanamama na mumewe hawajapata mtoto mwingine.
Yule mwanamama alianza tena tabia yake kwa kumhakikishia kwamba mumewe hana tatizo na hawezi jua kuhusu uhusiano wao! Punde yule mama akashika ujauzito! Alipojifungua mtoto wa tatu alifanana sana na huyu rafiki yangu.
Ndipo huyu rafiki yangu aliamua kufuatilia kwakaribu ili ajue undani zaidi na ndipo alipogungua kwamba mwanamama huyo na mumewe walikuwa wamepanga mchezo wote kwani jogoo la mumewe 'haliwiki'
Sasa wana JF, huyu kijana hajaoa lakini anauhakika wa 100% kwamba watoto wale watatu ni wake...
Je, anayohaki ya kuwadai watoto hao kuwa ni wa kwake?
Je, afanyeje ili aweze kutendewa haki?