Pape
JF-Expert Member
- Dec 11, 2008
- 5,488
- 79
Jamani kweli hii ni njia panda kwangu, nilimfuma boyfriend wangu akiwa na mrembo mwingine, kwa upendo wangu nilimfuata na kumuuliza je hapa ndiyo safari uliyoniaga ya kuwa utakuwa mkoani for some weeks? Basi badala ya kuanza kunielezea kwanini amenidanganya kuwa yupo safari angali namuona na binti mwingine kwa bar!alianza kunipiga na kuniona kama mimi ni mgomvi kwa kumuuliza kwanini unanidanganya na kuwa na wanawake wengine? Je hii ni sahihi kwa alichokifanya kwangu? Naombeni ushauri wenu nami nitaufanyia kazi
Chanzo: Gonga hapa!
Chanzo: Gonga hapa!