Leo ni siku ya amani duniani katika kuazimisha siku hii.,napenda wana JF waenzi japo kwa muda wa siku moja( yaani leo hii au 31 november ) kwa kudumisha amani ambayo misingi yake ilishafanywa imara kutoka katika kauli mbiu ya chama tawala cha ccm. Kwa kulizingatia hilo nategemea leo hii ndani ya JF amani itatawala na sitegemei kuona watu wakiendeleza kutuma post zenye misingi ya ubinafsi, ubaguzi na chuki. Kwani ubinafsi ni chanzo cha ubaguzi, ubaguzi ambao uzalisha chuki na baadae chuki hiyo huvunja amani. Imefika wakati watu lazima tufahamu na tukubali kuwa kuwepo kwa wewe ndiko kulikonifanya mimi kuwepo na maisha yangu mimi yawe ni kitu cha msingi katika maisha yako wewe. Siasa haimaanishi mfarakano ingawa wakati mwingine tunafikia hapo na wala upinzani katika siasa hauna maana ya kupinga ila kuwa na mawazo mbadala ingawa upinzani wetu umejikita katika kupinga pekee. Haya ni ya msingi na lazima yapewe mazingatio yanayostahili.,TAMBUA maisha yangu yanasehemu katika maisha yako na kwa mfano huu ni CCM inayoifanya CHADEMA iishi.