Ustaadh
JF-Expert Member
- Oct 25, 2009
- 413
- 19
Kuna jamaa yangu alinisimulia kisa cha abiria mmoja ambaye alikanyagwa mguu na abiria mwenzake kwenye daladala lililoshona abiria. Abiria aliyekanyagwa alipoinua macho yake kuangalia aliyemkanyaga, akabaini ni jitu la miraba minne. Akaingiwa na hofu, ujasiri ukamtoka akaishia kusema "Kaka, samahani mguu wako uko juu ya mguu wangu." Alitakiwa kueleza jinsi alivyokanyagwa badala yake akaishia kuomba radhi!
Watanzania tumeshakuwa kama huyo jamaa aliyekanyagwa, tunaibiwa rasilimali, watu wanafoji vyeti, umri, nchi inaendeshwa kama shamba la bibi na mambo kibao ya kusikitisha, hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya wahusika nasi tunabakia kuwaomba radhi watawala kwa kusema "samahani mguu wenu uko juu ya mguu wetu".
Ifike mahali ama tuseme "mnatukanyaga" au tunyamaze milele!
Watanzania tumeshakuwa kama huyo jamaa aliyekanyagwa, tunaibiwa rasilimali, watu wanafoji vyeti, umri, nchi inaendeshwa kama shamba la bibi na mambo kibao ya kusikitisha, hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya wahusika nasi tunabakia kuwaomba radhi watawala kwa kusema "samahani mguu wenu uko juu ya mguu wetu".
Ifike mahali ama tuseme "mnatukanyaga" au tunyamaze milele!