Dumelambegu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,052
- 257
Haka kanchi sasa kanaelekea kubaya. Ni juzi tu nimesikia Lyatonga Mrema ametunukiwa udokta na jamaa fulani kutoka Afrika Kusini. Sherehe ya kutunukiwa udokta ilihudhuriwa na Mrema mwenyewe na mkewe pamoja na huyo jamaa nae akiwa na mkewe. Cha ajabu leo kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku mtangazaji wa TBC amemtaja Mrema kama Dr. Lyatonga Mrema. Mambo hayo! Itafika mahali waheshimiwa wote bungeni watakuwa ni madokta. Kwa sasa Mhe. Mrema na Mhe. Mwakyembe sasa ni ngoma droo.