Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,728
- 2,256
Pole sana mkuu Timbala kwa kuingizwa mkenge.JAMANI WANA JF HABARI,
Mimi nafanya kazi kwenye taasisi moja kubwa tuu na mshahara wangu mzuri tuu najimudu vyema. Wakati naanza kazi nikakutana na mdada mmoja ambaye alitokea kunipenda ghafla nikajikuta nimeshaingia kingi bila kujijua. Maskini ya Mungu kumbe ni mke wa mtu na hakuwa na pete na mimi kwa ugeni wangu sikulijua hilo. When i realised that nilijuta sana na bahati nzuri jama hakujua, maana sijui ingekuwaje.
Huyo dada alivyogundua kuwa nimejua akawa analia lia tuuuu na kunibembeleza kuwa huko kwa mumewe hapati chochote jamaa hovyo. Akawa ananisifia kuwa endapo nitamwacha atajiua, hivyo tuwe wapenzi kisiri siri. Nikaamua kumuacha step by step, bila yeye kujua. Nikawa napunguza frequency za kukutana na yeye taratibu. Alivyoona vile akaenda akamchukua mfanyakazi mwenzangu pale ofisini akawa substitute yangu. Baadaye akaanza kuniponda tena na majungu kibao, mpaka sasa anaendelea kufanya hivyo huku akijua kuwa mimi najua hilo na anaona sawa.
Jamani dunia imekwisha, nimetafakari sana hivi ningefumaniwa na mumewe ningekuwa wapi sasa!!! Mtuoneee huruma jamani akina dada muwe na uzalendo muwe wawazi. Am tired and i dont trust a woman naona bora niishi kivyangu vyangu tuu.
Sasa hivi kwa akina dada wengine maofisini, hata walioolewa kutembeza "biashara" kwa ajili ya kipato ishakuwa fair game kwao.
Katika mazingira yaliyopo huyo dada kwa vile anaendelea na "biashara" hapo hapo kazini atawakoroga sana ili" biashara" yake ishamiri.
Cha kufanya ni mtonye bosi -halafu utafute kazi nyingine, na kwa hali iliyopo wewe inawezekana hauko peke yako kuingizwa mkenge hapo ofisini.