Mimibaba
JF-Expert Member
- Jul 1, 2009
- 4,557
- 1,291
Hapo juu kwa sithole # 12 si kweli.
Umuoe lakini usikwepe majukumu.
Mimi nilioa at 33 mke wangu akiwa 19 kijijini kabisa 30 yrs ago. Nilimpeleka shule ya ushonaji (ya kiveta veta) mara tu nilipomleta mjini. Ndugu zangu wote 4 ambao walikuwa wamekamilisha masomo yao vyuo vikuu wakati huo, walinitenga kwa kuoa mwanamke asiye na elimu; nikayakubali tu kwani dhamiri yangu iliniambia nafanya kitu sahihi.
Baada ya masomo nikampa mtaji ajitegemee kwa ushonaji, alifanya hivyo. Sasa hivi nimestahafu ananilisha na watoto ambao wanakamilisha masomo yao anawalipia kwa kazi ya ushonaji.
Juu ya sexual life usipime maana ukweli unabaki kuwa gari bovu halikokotwi na gari bovu, thanx to to the age difference; tunafaidi sana na tupo wawili tu nyumbani kwani watoto wana maisha yao na watoto wao. Wajukuu are just friends.
Ndugu zangu wa vigezo vya shule kichwani kati ya 4, mmoja tu amedumu na ndoa, watoto wa ndugu zangu wengine na ndugu zangu wote wanamuangalia huyu mke wangu kama mama yao wakuwashauri.
Tofauti ya umri ina faida moja kubwa unaweza kumfinyanga mwenzio kwa matakwa ya kuendana na maisha yako; mama analea watoto wake full time na kujenga mshimano wa familia (No house girls). Hasara yake ipo 1. atakosa nafasi nzuri ya kusoma, lakini elimu haijawasaidia wengi hasa kwenye kujitegemea. 2. Mwanzoni atajiona yuko out of place kwa udogo wake; baadae anajua na kushika nafasi yake kwenye nyumba kama mama kwa matakwa yenu.
MUHIMU NI WEWE UJUE WAJIBU WAKO UMUELEWE NA UMPE KILA MSAADA ANAOSTAHILI. UWE NA DHAMIRA YA MUDA MREFU YA KUKABIRI CHANGAMOTO AMBAZO LAZIMA ZITAKUWEPO.
Samahani kwa maelezo marefu lakini that is my experience you can share it with me.
Umuoe lakini usikwepe majukumu.
Mimi nilioa at 33 mke wangu akiwa 19 kijijini kabisa 30 yrs ago. Nilimpeleka shule ya ushonaji (ya kiveta veta) mara tu nilipomleta mjini. Ndugu zangu wote 4 ambao walikuwa wamekamilisha masomo yao vyuo vikuu wakati huo, walinitenga kwa kuoa mwanamke asiye na elimu; nikayakubali tu kwani dhamiri yangu iliniambia nafanya kitu sahihi.
Baada ya masomo nikampa mtaji ajitegemee kwa ushonaji, alifanya hivyo. Sasa hivi nimestahafu ananilisha na watoto ambao wanakamilisha masomo yao anawalipia kwa kazi ya ushonaji.
Juu ya sexual life usipime maana ukweli unabaki kuwa gari bovu halikokotwi na gari bovu, thanx to to the age difference; tunafaidi sana na tupo wawili tu nyumbani kwani watoto wana maisha yao na watoto wao. Wajukuu are just friends.
Ndugu zangu wa vigezo vya shule kichwani kati ya 4, mmoja tu amedumu na ndoa, watoto wa ndugu zangu wengine na ndugu zangu wote wanamuangalia huyu mke wangu kama mama yao wakuwashauri.
Tofauti ya umri ina faida moja kubwa unaweza kumfinyanga mwenzio kwa matakwa ya kuendana na maisha yako; mama analea watoto wake full time na kujenga mshimano wa familia (No house girls). Hasara yake ipo 1. atakosa nafasi nzuri ya kusoma, lakini elimu haijawasaidia wengi hasa kwenye kujitegemea. 2. Mwanzoni atajiona yuko out of place kwa udogo wake; baadae anajua na kushika nafasi yake kwenye nyumba kama mama kwa matakwa yenu.
MUHIMU NI WEWE UJUE WAJIBU WAKO UMUELEWE NA UMPE KILA MSAADA ANAOSTAHILI. UWE NA DHAMIRA YA MUDA MREFU YA KUKABIRI CHANGAMOTO AMBAZO LAZIMA ZITAKUWEPO.
Samahani kwa maelezo marefu lakini that is my experience you can share it with me.