Ambassador
JF-Expert Member
- Jun 2, 2008
- 933
- 75
Kuna dada mmoja nilitokea kumzimia sana miaka ya nyuma lakini pamoja na kumuimbisha nyimbo zote zikiwemo maarufu kama "akanana" hakuelewa somo. Aliamini kwamba alikuwepo mwingine ambaye yeye alimpenda kwa dhati bila kuwa muwazi kama kweli alikuwepo au ilikuwa imani yake tu. Nilimsumbua sana. Kwa kweli aliupeleka puta moyo wangu mpaka nikakosa raha ya maisha kabisaaa! Ililnichukua muda kumfuta kabisa akilini mwangu alipoondoka kwenda nje na wazazi wake.
Huyo dada karejea nchini na jana kanipigia simu tukutane kwenye mgahawa mmoja jijini. Nilipomuuliza namba yangu kaipataje alisema cha muhimu ni kwamba namba yangu anayo, suala la ameipataje halina umuhimu wowote kwa sasa.
Niliamua kuitika wito. Kwa kweli dada huyo kapendeza sana kuliko hata alivyokuwa wakati ule namlilia. Tulikaa nae takriban masaa matatu na kwa kweli tuliongea mambo mengi sana. Kwa ufupi alinieleza kwamba ametambua kwamba nilikuwa na mapenzi ya kweli kwake na sasa yuko tayari kuwa na mimi. Isingekuwa nimeshaoa ningemkubalia mara moja! Pamoja na kumueleza kuwa sasa nina familia alisisitiza kwamba awe hata girl friend wangu.
Huyu dada ana nia gani na mimi kama si kunivunjia ndoa? Ni kweli nilimpenda sana lakini kwa sasa ninae wangu mwandani.
Huyo dada karejea nchini na jana kanipigia simu tukutane kwenye mgahawa mmoja jijini. Nilipomuuliza namba yangu kaipataje alisema cha muhimu ni kwamba namba yangu anayo, suala la ameipataje halina umuhimu wowote kwa sasa.
Niliamua kuitika wito. Kwa kweli dada huyo kapendeza sana kuliko hata alivyokuwa wakati ule namlilia. Tulikaa nae takriban masaa matatu na kwa kweli tuliongea mambo mengi sana. Kwa ufupi alinieleza kwamba ametambua kwamba nilikuwa na mapenzi ya kweli kwake na sasa yuko tayari kuwa na mimi. Isingekuwa nimeshaoa ningemkubalia mara moja! Pamoja na kumueleza kuwa sasa nina familia alisisitiza kwamba awe hata girl friend wangu.
Huyu dada ana nia gani na mimi kama si kunivunjia ndoa? Ni kweli nilimpenda sana lakini kwa sasa ninae wangu mwandani.