Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,359
Dk. Karl Peters (kati) akiwa na wenzake Dk. Karl Juhlke na Joachim Graf. Huyu Dk. Karl Peters ndiye aliyewaingiza mkenge babu zetu wakati wa kuingia ukoloni wa Ujerumani nchini kwa kuingia katika mikataba ya kilaghai na watawala wetu wa jadi
Mbwela, Chifu wa Wazigua mkoani Tanga, ndiye aliyekuwa mtawala wa jadi wa kwanza kutia saini mkataba na Dk. Karl Peters mwaka 1884.
Nimeikuta hii michuzi blog, inasikitisha sana. Hii ilikuwa 1884 miaka 126 iliyopita karibu karne 1 na robo. Maskini Mbwela alikuwa hajasoma hivyo hata hiyo sahihi sidhani kama ilikuwa ya kwake na hata kama ilikuwa ya kwake katu hakujua anachosaini.
Sisi tumesoma, tumesafiri sana, tunauelewa, Hivyo mwaka 2110 kizazi kijacho kitasemaje kuhusu Loliondo, Buzwagi, Bulyanhulu, Geita, Kahama na Ardhi wanayopewa wageni kwa kisngizio cha Kilimo kwanza? Na chochote watakachosema, kutakuwa na sababu ipi ya kusema vinginevyo?