Mkuu kumbukumbu ya Shibuda iko sana, nilicho na uhakika ni kuwa safari hii hawezi kuteuliwa he has to be tested for at least two years ila kuchuku form ni haki ya kila mwanachama.Hivi huyu bwana amesoma na kuelewa lini itikadi ya CDM? Kwamba katika masaa 72 tayari ameiva kupeperusha bendera ya chama! Hiyo rushwa aliyoiona CCM ni wakati wa uchaguzi wa kuteliwa au ilikuepo kila siku?
Hivi amengia CDM kusimamia na kutetea itikadi au kugombea ubunge?
Sijui kama CDM wanakumbu kumbu na Shibuda! na je CDM haina wapiganaji waliokuwepo huko wakitetea itikadi za chama tena kwa ngeu hadi leo huyu bwana afikie hatua ya kuruhusiwa kuchukua fomu!
Kwenye bold Chadema hatuhadaiki kirahisi namna hiyo labda anawahadaa nyie CCM.Ninaimani Chadema has grown up enough kutotegemea makapi ya CCM na wanachama maslahi ambao ni wa ganga njaa!, inamaana asipopitishwa, atarudi alikotoka!. Huyu imekula kwake!. Amechukua fomu ili kuwahadaa Chadema kuwa yeye ndio chaguo la wana Meru hivyo akipitishwa, atazoa kura zote za Sioi hivyo Chadema itashinda kiulaini!. Mwambieni apeleke njaa yake kule kule kwa waendekeza njaa CCM, Chadema ni kwa wapiganaji!.