Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,395
Hebu tuchukulie kwamba, umepata taarifa kuwa, kuna dada binamu wa mumeo ambaye alikuwa ameolewa na kuachika amefariki. Na amefariki kwa ukimwi. Wewe na mumeo mnakwenda kushiriki kwenye mazishi. Mnapofika huko unasikia minong'ono kuwa huyo binamu alikuwa ni hawara wa mumeo, na hata mtoto wake wa mwisho inasemekana ni wa mumeo.
Kumbukumbu zako zinaonesha kwamba, mumeo alikuwa karibu sana na binamu yake huyo na alikuwa akimpa misaada mingi tangu aachike na hata kipindi cha kuumwa kwake alikuwa mstari wa mbele kumsaidia.
Baada ya mazishi unafanya uchunguzi wa kimya kimya na hatimaye unathibitisha pasi na shaka yoyote kwamba, jambo hilo lina ukweli kwa asilimia 100.
Hebu niambie kama ni wewe umepata taarifa kama hizo ungefanyaje?
Kumbukumbu zako zinaonesha kwamba, mumeo alikuwa karibu sana na binamu yake huyo na alikuwa akimpa misaada mingi tangu aachike na hata kipindi cha kuumwa kwake alikuwa mstari wa mbele kumsaidia.
Baada ya mazishi unafanya uchunguzi wa kimya kimya na hatimaye unathibitisha pasi na shaka yoyote kwamba, jambo hilo lina ukweli kwa asilimia 100.
Hebu niambie kama ni wewe umepata taarifa kama hizo ungefanyaje?