Mgombea ubunge wa CUF katika uchaguzi wa 2010 jimbo la KIGOMA KASKAZINI ndugu OMAR MUSA MKWALULO amekamatwa leo mchana na polisi jijini Dar es salaam.
Bwana mkwalulo alipigiwa simu na ofisa wa takukuru mkoa wa kigoma jana akiwa ifakara.
Alimjulisha ofisa huyo kuwa yuko ifakara na ndipo ofisa huyo wa TAKUKURU alimjulisha bwana mkwalilo kuwa aende kwa ofisa wa TAKUKURU wilaya ya kilombero ili akasaini fomu maalum ambazo hazikuelezwa ni za namna gani.
Bwana mkwalulo hakuweza kwenda kwa sababu tayari alikuwa ndani ya basi akirejea dar es salaam.
Alipofika dar es salaam bwana mkwalilo akampigia yule ofisa wa takukuru mkoa wa kigoma kumjulisha kuwa hakuweza kushuka kwenye gari ili kumuona ofisa wa takukuru wa kilombero, ikabidi ofisa huyo wa kigoma amuombe bwana mkwalilo aende takukuru makao makao makuu dar es salaam na kuwa akifika tu atapewa fomu maalum ambazo lazima azijaze.
Katika hali ya kushangaza leo majira ya mchana bwana mkwalilo alipoenda takukuru makao makuu dar es salaam aliwekwa chini ya ulinzi mkali na akaelezwa kuwa atasafirishwa hadi kigoma ambako ana mashtaka ya kutoa na kupokea rushwa aliyoyatenda wakati wa uchaguzi mkuu mwaka jana.
Alipohoji kwa nini takukuru mkoa wa kigoma hawakumuita moja kwa moja hadi kigoma ili kuondoa mawindo waliyokuwa wakimfanyia alijibiwa kuwa hayo ni maagizo kutoka juu.
Bwana omar mkwalulo ni mfanyabiashara mkubwa sana jijini dar es salaam, mwaka 2010 aliingia kwenye mchakato wa kura za maoni CCM jimbo la kigoma kaskaz akafanyiwa mizengwe hadi akashindwa na ndipo akafanya maamuzi ya kuhamia CUF.
Alipohamia CUF ujumbe wa CCM ukiongozwa na baadhi ya viongozi wakubwa ulikwenda kigoma ili kusuluhisha na kumshawishi asiende CUF lakini akashindikana.
Bwana mkwalulo aliingia kwenye kinyang'anyiro hicho cha ubunge na kupambana na zitto na mgombea wa CCM na mwisho wa siku zitto aliibuka kidedea huku kura alizopata mkwalulo ukijumlisha na za mgombea wa CCM zilizidi zile za zitto na hiyo ina maana kuwa iwapo asingehamia CUF na kugawa kura za CCM , mgombea wa CCM angeibuka kidedea.
Uchaguzi mkuu ulipoisha mwaka jana mkwalulo alifuatwa na maafisa wa TRA mara kadhaa na kumbambikizia kuwa halipi kodi lakini aliwapa vithibitisho vyote kuwa analipa kodi kwa uhakika na TRA wakakosa cha kumkamatia.
Hivi sasa serikali ya CCM inawatumia takukuru ili kujaribu kulipiza kisasi kwa mkwalulo na haijulikani watafanikiwa kwa kiasi gani.
Chanzo cha kuaminika cha habari hii kimewasiliana na omar musa mkwalulo akiwa SALENDER BRIDGE chini ya ulinzi mkali na amesema hajui ni makosa yapi ya kuchukua na kutoa rushwa kwani anasema hajawahi kutoa wala kupokea rushwa wakati wa uchaguzi.
Vyanzo kutoka CUF vinaeleza kuwa mawakili wa chama na naibu katibu mkuu JULIUS MTATIRO wanahaha kuona namna gani wanaweza kumtafutia dhamana mgombea huyu na kisha aende mwenyewe kigoma kukabiliana na mashtaka husika.
Wanasiasa wanaendelea kushughulikiwa.
Bwana mkwalulo alipigiwa simu na ofisa wa takukuru mkoa wa kigoma jana akiwa ifakara.
Alimjulisha ofisa huyo kuwa yuko ifakara na ndipo ofisa huyo wa TAKUKURU alimjulisha bwana mkwalilo kuwa aende kwa ofisa wa TAKUKURU wilaya ya kilombero ili akasaini fomu maalum ambazo hazikuelezwa ni za namna gani.
Bwana mkwalulo hakuweza kwenda kwa sababu tayari alikuwa ndani ya basi akirejea dar es salaam.
Alipofika dar es salaam bwana mkwalilo akampigia yule ofisa wa takukuru mkoa wa kigoma kumjulisha kuwa hakuweza kushuka kwenye gari ili kumuona ofisa wa takukuru wa kilombero, ikabidi ofisa huyo wa kigoma amuombe bwana mkwalilo aende takukuru makao makao makuu dar es salaam na kuwa akifika tu atapewa fomu maalum ambazo lazima azijaze.
Katika hali ya kushangaza leo majira ya mchana bwana mkwalilo alipoenda takukuru makao makuu dar es salaam aliwekwa chini ya ulinzi mkali na akaelezwa kuwa atasafirishwa hadi kigoma ambako ana mashtaka ya kutoa na kupokea rushwa aliyoyatenda wakati wa uchaguzi mkuu mwaka jana.
Alipohoji kwa nini takukuru mkoa wa kigoma hawakumuita moja kwa moja hadi kigoma ili kuondoa mawindo waliyokuwa wakimfanyia alijibiwa kuwa hayo ni maagizo kutoka juu.
Bwana omar mkwalulo ni mfanyabiashara mkubwa sana jijini dar es salaam, mwaka 2010 aliingia kwenye mchakato wa kura za maoni CCM jimbo la kigoma kaskaz akafanyiwa mizengwe hadi akashindwa na ndipo akafanya maamuzi ya kuhamia CUF.
Alipohamia CUF ujumbe wa CCM ukiongozwa na baadhi ya viongozi wakubwa ulikwenda kigoma ili kusuluhisha na kumshawishi asiende CUF lakini akashindikana.
Bwana mkwalulo aliingia kwenye kinyang'anyiro hicho cha ubunge na kupambana na zitto na mgombea wa CCM na mwisho wa siku zitto aliibuka kidedea huku kura alizopata mkwalulo ukijumlisha na za mgombea wa CCM zilizidi zile za zitto na hiyo ina maana kuwa iwapo asingehamia CUF na kugawa kura za CCM , mgombea wa CCM angeibuka kidedea.
Uchaguzi mkuu ulipoisha mwaka jana mkwalulo alifuatwa na maafisa wa TRA mara kadhaa na kumbambikizia kuwa halipi kodi lakini aliwapa vithibitisho vyote kuwa analipa kodi kwa uhakika na TRA wakakosa cha kumkamatia.
Hivi sasa serikali ya CCM inawatumia takukuru ili kujaribu kulipiza kisasi kwa mkwalulo na haijulikani watafanikiwa kwa kiasi gani.
Chanzo cha kuaminika cha habari hii kimewasiliana na omar musa mkwalulo akiwa SALENDER BRIDGE chini ya ulinzi mkali na amesema hajui ni makosa yapi ya kuchukua na kutoa rushwa kwani anasema hajawahi kutoa wala kupokea rushwa wakati wa uchaguzi.
Vyanzo kutoka CUF vinaeleza kuwa mawakili wa chama na naibu katibu mkuu JULIUS MTATIRO wanahaha kuona namna gani wanaweza kumtafutia dhamana mgombea huyu na kisha aende mwenyewe kigoma kukabiliana na mashtaka husika.
Wanasiasa wanaendelea kushughulikiwa.