Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Nikiitizama ramani ya Tanganyika huru huwa najiuliza makusudi ya mbunifu wa mipaka yake.
Unaweza kuona wazi kuwa ni nchi liyopewa nafasi kwa upendeleo mkubwa. Pengine aliyekuwa akigawa mipaka hiyo alikuwa mbabe kuliko wengine na kuamua kujigawia pande lenye utajiri mwingi.
Tizama kuanzia Tanga pale juu, jamaa akachora mstari ulionyooka. Alipofika usawa wa ml Kilimanjaro, akakunja kona kidogo na kuchota mlima huo kisha akasonga mbele kuelekea juu. Alipofika Ziwa Victoria, akapasua huku sehemu kubwa zaidi ikiwa ndani. Akaelekea magharibi kwa ajili ya kuchukua usawa wa ziwa Tanganyika. Akapasua katikati mpaka mwisho, pala akakunja kuelekea mashariki kidogo. Alipofika usawa wa ziwa Nyasa, akakata kona kulilenga. Nalo akapasua katikati, alipofika mwisho wa ziwa hilo akasema sasa inatosha. Akakata kuelekea mashariki huku akichora kwa kulipualipua kuelekea mpaka bahari ya Hindi.
Mgawaji huyu alikuwa mjanja kuliko wengine? au mbabe kuwazidi wenzake? Akaacha Tanganyika yenye kila aina ya utajiri na neema. Leo tunacheza ngoma kushangilia miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika masikini.
Wakoloni walitubeba lakini mpaka leo tumeshindwa kubebeka.
Unaweza kuona wazi kuwa ni nchi liyopewa nafasi kwa upendeleo mkubwa. Pengine aliyekuwa akigawa mipaka hiyo alikuwa mbabe kuliko wengine na kuamua kujigawia pande lenye utajiri mwingi.
Tizama kuanzia Tanga pale juu, jamaa akachora mstari ulionyooka. Alipofika usawa wa ml Kilimanjaro, akakunja kona kidogo na kuchota mlima huo kisha akasonga mbele kuelekea juu. Alipofika Ziwa Victoria, akapasua huku sehemu kubwa zaidi ikiwa ndani. Akaelekea magharibi kwa ajili ya kuchukua usawa wa ziwa Tanganyika. Akapasua katikati mpaka mwisho, pala akakunja kuelekea mashariki kidogo. Alipofika usawa wa ziwa Nyasa, akakata kona kulilenga. Nalo akapasua katikati, alipofika mwisho wa ziwa hilo akasema sasa inatosha. Akakata kuelekea mashariki huku akichora kwa kulipualipua kuelekea mpaka bahari ya Hindi.
Mgawaji huyu alikuwa mjanja kuliko wengine? au mbabe kuwazidi wenzake? Akaacha Tanganyika yenye kila aina ya utajiri na neema. Leo tunacheza ngoma kushangilia miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika masikini.
Wakoloni walitubeba lakini mpaka leo tumeshindwa kubebeka.