Wa Nyumbani
JF-Expert Member
- Mar 31, 2011
- 438
- 65
Wiki moja baada ya harusi, Jamaa akaanza kurudi nyumbani akiwa ananuka sigara. Mke wake akakasirika na kumweleza kuwa mbona kabla ya harusi alisema havuti sigara? Kesho yake jamaa akarudi amelewa sana. Mke wake akazidi kukasirika na kulalama.
'Ulisema hunywi pombe, mbona unakunywa?"
Siku iliyofuata kukazuka zogo mtaani. Mwanamke alipokwenda kwenye tukio akakuta jamaa amefumaniwa na mke wa mtu. Mke akabaki ameduwaa!
Mwanamke mmoja jirani yake akamwambia,
"Shoga usishangae, huyu mume wako ni mtu wa vituko hapa mtaani. Hivi alivyokuoa tunaona amepunguza vituko, ni mlevi kupindukia, mvuta bangi na ni mzinzi mkubwa. Ametembea na wanawake karibu wote hapa mtaani. Usituone hivi, wenzako tunajuta!!"
'Ulisema hunywi pombe, mbona unakunywa?"
Siku iliyofuata kukazuka zogo mtaani. Mwanamke alipokwenda kwenye tukio akakuta jamaa amefumaniwa na mke wa mtu. Mke akabaki ameduwaa!
Mwanamke mmoja jirani yake akamwambia,
"Shoga usishangae, huyu mume wako ni mtu wa vituko hapa mtaani. Hivi alivyokuoa tunaona amepunguza vituko, ni mlevi kupindukia, mvuta bangi na ni mzinzi mkubwa. Ametembea na wanawake karibu wote hapa mtaani. Usituone hivi, wenzako tunajuta!!"