babayah67
JF-Expert Member
- Mar 28, 2008
- 493
- 79
Jana nilipata bahati ya kuusikiliza mkutano wa Dr Slaa uliofanyika katika viwanja vya MwembeYanga. Mkutano ulianza vizuri na wote waliopata nafasi ya kuzungumza walizungumza kwa ufanisi mzuri saana HADI pale ilipobaki dakika tano za mwisho. Zilipobaki dakika tano za mwisho Dr Slaa aliwaoomba wagombea ubunge wa majimbo mbalimbali ya mkoa wa Dar wasimame kuwasalimia wananchi na kuwaomba kura zao. Wagombea ubunge wa majimbo ya Ubungo, Ukonga, Kinyerezi na Kigamboni, walisimama na kila mmoja aliutumia muda wake vizuri saana kuhamasisha watu na kuwaomba kura zao ziende kwa Dr Slaa. Ilipofika zamu ya mgombea ubunge kwa jimbo la Temeke, alianza kuongea mambo ambayo nahisi hata Dr Slaa yalimkwaza. Huyu bwana alianza kwa kumshambulia JK moja kwa moja kwa kusema kuwa yote mabaya yanayofanywa na JK yanatokana na kuwa hakufunzwa vizuri na mama yake. Na akatumia hata methali isemayo asofunzwa na wazazi hufunzwa na ulimwengu. Kwa mtazamo wangu naona huyu mgombea hakumtendea haki JK na hasa Mama yake kwa kumjumlisha katika masuala ambayo huyo mama hahusiki katika masuala ya kisiasa ya mwanae. Nisingempinga kama angemtukana JK bila kumhusisha mama yake. NDIO MAANA NINA WASIWASI HUENDA HUYU JAMAA AKAWA SI CHADEMA KINDAKINDAKI, ASIJE AKAWA NA LENGO LA KUVURUGA USHINDI WA CHADEMA DAR na TZ Kwa ujumla.