AL-Jazeera News TV Channel ya Kiswahili

1) Hapa si wakija ma Investor wanaitwa mafisadi.

2) Maandamano ya kila siku ya chadema unafikiri yana tija? kusudio lake si kuvunja nguvu za Kikwete alizozitoa kutafuta ma investor. Unafikiri wenye mitaji yao ya uhakika watakuja hapa, kila kukicha maandamano?


thats bull shit.............think big
 
itakuwa vizuri sana,kwani hawa jamaa hawafichi ki2u,ndio maana nchi za magharibi hawaipendi.
 
Nisingependa Hasan Marine aende huko maana ataleta longolongo...........
 
Usalama wa Taifa vipi hapo mbona inapelekwa Nairobi wakati hta hapo siyo katikati ya hizi nchi. Kwa nini wanawalenga waislam na siyo watu wote but its good and i love it.
 
1) Hapa si wakija ma Investor wanaitwa mafisadi.

2) Maandamano ya kila siku ya chadema unafikiri yana tija? kusudio lake si kuvunja nguvu za Kikwete alizozitoa kutafuta ma investor. Unafikiri wenye mitaji yao ya uhakika watakuja hapa, kila kukicha maandamano?

Pole kwa kutoelewa,wawekezaji tunao wakubali sisi ni matapeli tu,kama hawakati hawapewi,mifano ipo mingi angalia Reli walikuwapo wa canada hawakupewa,wawekezaji makini katika serikali yetu hawapewi,kiwanda cha magurudumu arusha walikuwapo wajerumani lakini walizungushwa kisa kuna wakubwa walitaka kampuni ya yana wapewe hawa ni wahindi wakishirikiana na viongozi wetu,kuandamana na kupinga watu wa namna hii ni muhimu lazivyo tutaangamia kabisa.hawa jamaa wana mipango yao na si CDM iliyowakimbiza.
 
1) Hapa si wakija ma Investor wanaitwa mafisadi.

2) Maandamano ya kila siku ya chadema unafikiri yana tija? kusudio lake si kuvunja nguvu za Kikwete alizozitoa kutafuta ma investor. Unafikiri wenye mitaji yao ya uhakika watakuja hapa, kila kukicha maandamano?
naamini hujui unachozungumza
 
kwanini kila kitu Kenya.. na sio TZN! ... kiswahili fasaa kinaongelewa Unguja .. kwanini wakiweke kenya!?!!
 
kwanini kila kitu Kenya.. na sio TZN! ... kiswahili fasaa kinaongelewa Unguja .. kwanini wakiweke kenya!?!!

Ni nani anayeweza ku-judge kuwa kiswahili kipi ni fasaha?
Inawezekana wale wa malindi Kenya, wakasema cha kwao ndio fasaha.
Au tunatumia vigezo gani kuita kiswahili, fasaha?
 
Ni nani anayeweza ku-judge kuwa kiswahili kipi ni fasaha?
Inawezekana wale wa malindi Kenya, wakasema cha kwao ndio fasaha.
Au tunatumia vigezo gani kuita kiswahili, fasaha?

Sishangai kuona Al Jazeera wanakwenda nairobi kwa sababu zifuatazo,
1. Kuna utani au kauli inasema Kiswahili kilizaliwa Unguja, kikakua Tanzania bara, Kikakomaa Kenya na kikafa Uganda.

2. Wakenya wako agressive sana katika duru za kimataifa hivyo basi wanaweza kuwa wame lobby na kuwashawishi hao Aljazeera wfikikiri kuwa lugha hiyo inaongewa sana kenya kuliko nchi nyingine hapa ulimwenguni.

3. Wakenya walivyo agressive wanaweza wakatumia uwongo wowote kama vile wanavyosema mlima Kilimanjaro uko nchini kwao hivyo basi kupata watalii wengi kuliko Tanzania.

4. Wa-Tanzania wanapenda sana kuongea kwenye magenge na forums mbalimbali kuliko kutenda. Angalia hata huko America na Ulaya waalimu wengi wa lugha ya Kiswahili kwenye idara za African History na wakenya. Sisi maprofesa wetu wamebweteka tu.

5. Baada ya matatizo yaliyoletwa na matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2008 wa Kenya bado wa-Tanzania hatukuchukua fursa za kugombea biashara ya watalii kutoka kenya na hata Shillingi ya Kenya haikutetereka dhidi ya Shilingi ya Tanzania.

6. Sisi Tanzania kwa sasa investimate climate yetu si nzuri kabisa kwani uwekezaji unaonekana ni ufisadi.

7. hali ya umeme ni tete kiasi kwamba mwekezaji inamfanya ajiulize mara mbili kuwa je utility costs za tanzania zitamwezesha ku break even

8. Hata watendaji wa JK walio madarakani wengi ni waoga kupitisha maamuzi mapya hasa ya uwekezaji kwani wanaogopa yasije yakawakuta kama ya akina basil Mramba, Gray, Mgonja na Yona.

Tuwe wapole kwa miaka 4 iliyobakia hadi tuone serikali ijayo whether inatoka opposiition au chama kilichopo. Other wise musitegemee lolote kwani makosa ya 2005 hayatakuja futika katika historia ya uchumi wa Tanzania
 
Sishangai kuona Al Jazeera wanakwenda nairobi kwa sababu zifuatazo,

7. hali ya umeme ni tete kiasi kwamba mwekezaji inamfanya ajiulize mara mbili kuwa je utility costs za tanzania zitamwezesha ku break even

...Tuwe wapole kwa miaka 4 iliyobakia hadi tuone serikali ijayo whether inatoka opposiition au chama kilichopo. Other wise musitegemee lolote kwani makosa ya 2005 hayatakuja futika katika historia ya uchumi wa Tanzania

Na sio suala la umeme tu, ndugu yangu.
Sisi tunapenda sana kujisifia hata kama kitu tunarachojisifia kipo duni au kidogo.
Sasa wewe angalia metropole ya Dar es salaam halafu linganisha na Nairobi. Changanya na hali ya hewa ya ubaridi ya Nairobi, halafu linganisha na Joto la Dar. Hebu angalia tu huduma za supermarkets, linganisha na Nairobi. Mimi naamini foreigners wengi wanajisikia more comfortable in Nairobi than in Dar. Na hicho huwa ni kigezo tosha kwa investor anapotaka kuwekeza.

Tanzania ilitakiwa kufanya juhudi za makusudi ili kuupanua mji wa Arusha uwe jiji la kisasa lenye miundo mbinu bab kubwa, hapo ndipo tungeweza kushindana na wakenya, kwa sababu sisi tungeongeza sifa za ziada za ukarimu, amani na kuwa karibu na vivutio vikubwa vya utalii. Lakini hili la kukaa na kujisifia na Dar yetu na kutegemea wawekezaji waipendelee Dar kuliko Nairobi, hiyo tunapoteza muda tu. Dar haijakaa ki-city city sana. It is more of a very large village.
 
Habari nzuri lakini hapa watanzania tunapigwa bao sababu tumekalia siasa tu

Watanzania kingereza tunapigwa bao na kenya tunajisifia tuna lugha yetu kiswahili
Haya channel za kiswahili nayo wakenya wanatupiga bao iwe ni BBC ina hawa Aljazera HQ ni Nairobi.

Why not Tanzania?
Why not Dar Es Salaam
Or why not Zanzibar?

Mkuu kwa huu umeme wa kijiko cha chai kweli kuna mtu atatamani kuja wekeza hapa? TZ twajizika wenyewe kwa kutokufanya jitihada za makusudi kutatua tatizo la umeme. Hata wawekezaji waliopo (CTI) wanalia!:smow:
 
Hawa wakenya wanatuacha kwa kila kitu, sisi tumekalia siasa tu!
 
Nimeishasema mara nyingi kwamba hii nji yetu inasafari ndefu sana. Sababu? Labda ni ile siasa ya Ujamaa na Kujitegea ya miaka ile, au..... hata sijui haki ya nani. Hebu fikiria, Idhaa ya kiswahili ya K'mataifa inaanzishwa na kuwekwa Nairobi, wakati Tanzania ambapo kiswahili ndio Lingua Franca yetu tumebaki kushikana makoo. Kuna mkuu ameongelea suala la LOBBYING, nadhani hilo neno halipo vichwani mwa viongozi wetu.
 
Iwapo suala ni uislamu na sio Lugha basi waislamu wala hatuna haja na Aljazeera.Hiki kituo kihabari kinafanana sana na BBC na CNN,nasubiri kusoma wikileak ya nani anayewafadhili.Na ilikuwaje wapinzani wakubwa wa US kule Iraq walishikwa na kuuliwa muda mfupi tu baada ya mahojiano yao na Aljazeera.Mfano ni AbuMussa Alzarqawi.
Habari zao nyingi kuhusu haki za wanawake na watoto na maazimio ya UN.hizi wala si habari zenye manufaa kwa waislamu.Nawaje tu na wataondoka kama wenzao akina BBC-kiswahili.
 
bwahahahahaha !!
kwa umemem gani waanzishe kituo cha tv? chadema ndio wanasababisha tuwe na mgao? na foleni kila siku?
tumia akili kufikiri na sio tumbo

Mwenye kufikiri utumbo na uharo ni wewe, hivi vituo vyote vya tv vilivyopo hapa sasa hivi mbona tunaviona hewani saa zote? hata umeme ukikatika, tuliobahatika kuwa na solar, bado tunaziona tv? au huyajui hao. Unanshangaza!
 
Mwenye kufikiri utumbo na uharo ni wewe, hivi vituo vyote vya tv vilivyopo hapa sasa hivi mbona tunaviona hewani saa zote? hata umeme ukikatika, tuliobahatika kuwa na solar, bado tunaziona tv? au huyajui hao. Unanshangaza!

Hivi hukusikia trip ya MD wa Tanesco (Bwana Mhando) pale TBC ...... kikubwa alicholalamikiwa na TBC ni kukatikakatika kwa umeme. Ukweli ni kuwa mazingira yetu ya uwekezaji si mazuri ukianzia na ukosefu wa umeme wa uhakika kwa siku 365 za mwaka, unfriendly financial institutions, uwezo wa watu wetu (kiutendaji na kiujuzi) n.k....
 
Mheshimiwa Anfaal,
Kwa hiyo unataka kutuambia Wa-Misri na Wa-Tunisia na wengine wanao hangaika ma utawala mbovu wangekaa tu kimya wanaonewa na majizi yaliyojilimbikizia mali eti kwa sababu wakiandamana mahoteli yatakosa wateja? Kama tuna waabudu wawekezaji kiasi hicho tumekwisha.
 
Habari njema sana, Aljazeerah naipenda sana baada ya Russia Today halafu ndio hao maCNN&BBC..ingekuwa professional yangu utangazaji ningeshatuma CV baada ya kuona tangazo hili...
 
Mheshimiwa Anfaal,
Kwa hiyo unataka kutuambia Wa-Misri na Wa-Tunisia na wengine wanao hangaika ma utawala mbovu wangekaa tu kimya wanaonewa na majizi yaliyojilimbikizia mali eti kwa sababu wakiandamana mahoteli yatakosa wateja? Kama tuna waabudu wawekezaji kiasi hicho tumekwisha.

Very true .....wakati mwingine ni vizuri kulipa gharama sasa for the better future ya vizazi vyetu vijavyo.
 
Back
Top Bottom