Ng'azagala
JF-Expert Member
- Jun 7, 2008
- 1,286
- 221
Akutwa na ngozi ya mtu
na Kenneth Mwazembe, Mbozi
MKAZI wa Kijiji cha Halungu, wilayani Mbozi, Yalesi Mganji, anashikiliwa na polisi mjini Vwawa kwa tuhuma za kuuza ngozi ya binadamu.
Mganji, alikamatwa jana na kupelekwa kituo cha polisi alipokuwa akitafuta mnunuzi wa ngozi za binadamu.
Mfanyabiashara Ringson Chaula ambaye aliwahi kufanikisha ukamataji wa wachuna ngozi 1998, alisema jana kuwa Mganji alikwenda ofisini jana alfajiri na kumtaka anunue ngozi ya binadamu.
Chaula ambaye aliandaliwa kununua ngozi mwaka 1998 ikiwa ni mtego wa polisi, anahisiwa kufanya biashara hiyo, ndiyo maana alifuatwa na wauzaji wa ngozi hizo wakiamini atanunua.
Baada ya kijana huyo kumweleza nia yake hiyo, alimchukua mtuhumiwa huyo akisaidiana na walinzi wake kumpeleka kituo cha polisi.
Watu hawa wanazidi kunichafua, juzi wanawake wawili walikuja kuniuzia mimba ili wakijifungua wanipe watoto, niliwakatalia, sasa leo wanataka kuniuzia ngozi ya binadamu, alilalama Chaula.
Hata hivyo, Mganji alipohojiwa alisema hayupo peke yake, kwani alitumwa na Damson Nkota, ili apatane bei na Chaula kisha waende wakamchune mtu waliyemuandaa.
Mlinzi wa Chaula, aliyejitambulisha kwa jina la Emmanuel Mwakitwange, alisema kijana huyo alifika ofisini hapo akidai anamtafuta Chaula, ili amuuzie mali.
Polisi wamethibitisha kuwpao kwa tukio hilo na kusema kwamba taarifa zitatolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa ambaye alikuwa kwenye mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa.
Vitendo vya uchunaji ngozi viliibuka wilayani hapa mwaka 1998 na kushika kasi, hali iliyowatisha watu wengi.
hivi tunatarajia neema kwa kila mtanzania ikiwa kuna matendo ya kishirikina kama haya? mara mauaji ya Albino, mara vichanga nk. kwa watu waishio vijijini,(Africa) haya mambo ya kishirikina/giza ni kizingiti kikubwa sana cha maendeleo, watu bado wanafikiri kuna option kama hii ya kuleta maendeleo (bado tupo enzi gani sijui!) lazima kwakweli watu tushirikiane na serikali kupambana na ujinga huu kwa dhati
na Kenneth Mwazembe, Mbozi
MKAZI wa Kijiji cha Halungu, wilayani Mbozi, Yalesi Mganji, anashikiliwa na polisi mjini Vwawa kwa tuhuma za kuuza ngozi ya binadamu.
Mganji, alikamatwa jana na kupelekwa kituo cha polisi alipokuwa akitafuta mnunuzi wa ngozi za binadamu.
Mfanyabiashara Ringson Chaula ambaye aliwahi kufanikisha ukamataji wa wachuna ngozi 1998, alisema jana kuwa Mganji alikwenda ofisini jana alfajiri na kumtaka anunue ngozi ya binadamu.
Chaula ambaye aliandaliwa kununua ngozi mwaka 1998 ikiwa ni mtego wa polisi, anahisiwa kufanya biashara hiyo, ndiyo maana alifuatwa na wauzaji wa ngozi hizo wakiamini atanunua.
Baada ya kijana huyo kumweleza nia yake hiyo, alimchukua mtuhumiwa huyo akisaidiana na walinzi wake kumpeleka kituo cha polisi.
Watu hawa wanazidi kunichafua, juzi wanawake wawili walikuja kuniuzia mimba ili wakijifungua wanipe watoto, niliwakatalia, sasa leo wanataka kuniuzia ngozi ya binadamu, alilalama Chaula.
Hata hivyo, Mganji alipohojiwa alisema hayupo peke yake, kwani alitumwa na Damson Nkota, ili apatane bei na Chaula kisha waende wakamchune mtu waliyemuandaa.
Mlinzi wa Chaula, aliyejitambulisha kwa jina la Emmanuel Mwakitwange, alisema kijana huyo alifika ofisini hapo akidai anamtafuta Chaula, ili amuuzie mali.
Polisi wamethibitisha kuwpao kwa tukio hilo na kusema kwamba taarifa zitatolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa ambaye alikuwa kwenye mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa.
Vitendo vya uchunaji ngozi viliibuka wilayani hapa mwaka 1998 na kushika kasi, hali iliyowatisha watu wengi.
hivi tunatarajia neema kwa kila mtanzania ikiwa kuna matendo ya kishirikina kama haya? mara mauaji ya Albino, mara vichanga nk. kwa watu waishio vijijini,(Africa) haya mambo ya kishirikina/giza ni kizingiti kikubwa sana cha maendeleo, watu bado wanafikiri kuna option kama hii ya kuleta maendeleo (bado tupo enzi gani sijui!) lazima kwakweli watu tushirikiane na serikali kupambana na ujinga huu kwa dhati